Ni kweli, kitu cha kwanza nilichofanya ni kushukuru kwa hicho kidogo nilichopata.
Kitu cha pili ni kukubali matokeo, kuwa japo CCM ni chama cha siasa, na chama cha siasa ni mali ya wanachama, hao wanachama hawafani, kuna wanachama ambao ni wanachama tuu, kuna wanachama ambao ni wakuja tuu, na kuna wanachama ambao wao ndio wenyewe wenye chama chao na kujifunza ili mtu ushinde kura za maoni CCM, ni lazima uwaone hao wenyewe wenye chama chao!, mimi sikumuona mtu yoyote na matokeo yake ndio ile kura moja
Hivyo nilipaswa kujipanga upya, ili uchaguzi unaofuata, nitupe tena karata yangu nikiwa nimejipanga nikiwa kamili gado.
Kwa vile ni wale CCM wa Nyerere type, hatuko tayari kufanya hizo mambo, hivyo nikakubali matokeo na kujikalia pembeni kwa kuendelea kulitumikia taifa katika maeneo mengine.
P.
Mwalimu Paskali,
naweza kuelewa mtazamo wako na kukubaliana nawe kwa kiasi,
lakini hapo ulipoeleza kwamba i
li ushinde kura za maoni CCM ni lazima uwaone wenyewe hao wenye chama chao, nao sio sahihi. mimi sikua na chochote na sina chochote cha kuwaoffer wajumbe ispokua utumishi na uongozi uliotukuka. kata zaidi ya 25, wajumbe zaidi ya 1000 ni vigumu mno kuwin sapoti yao wote. ni kuchagua sapoti ya kundi moja au mawili miongoni mwao.
binafsi wakati naomba ridhaa ya wana ccm katika nafasi ya ubunge kwa mara ya kwanza, nilikua simfahamu kiongozi yoyote wa ccm, hata mwenyekiti wa ccm kwenye tawi langu tu kule kijijini, japo nilikua nayafahamu karibu matawi yote jimboni kwangu baada ya kutamani kuomba nafasi hiyo.
Na sikua mjumbe wala kiongozi wa ngazi yoyote wa ccm kote nchini nilipokua naishi, na kwahivyo sikua nawafahamu hao unaodai ndio wenye chama chao. Mimi nimethibitisha mwenyewe pasina shaka yoyote kwamba, mwanachama yeyote wa ccm anaethubutu kwa chochote ndani ya CCM, anaweza kupata fursa anayoitaka bila mbambamba za ambao wanatisha wengine kwa dhana hiyo ya kwamba chama kina wenyewe.
Chama ni cha kwetu sote.
Leo hii mathalani,
napigiwa cm na kupata messages kutoka kwa wanachama na viongozi mpaka nacheka mwenyewe, nakujiuliza hivi kulikoni? kwamba hawa watu mbona wakati natia nia mara ya kwanza na hata ya pili hawakunifahamu hivi, kulikoni leo? sikukata tamaa na sintakata tamaa hata iweje
Kura yako 1 ilipaswa kua utambulisho wako muhimu sana mwalimu Paskali,
kwasababu ungerudi mara ya pili ungewauliza wajumbe ni nani asiekujua? na kwa majigambo zaidi hata kujitambulisha kwako kulifaa kua mimi ndie
yule wa kura moja kura za maoni za ubunge2020.
Nashauri ikiwa utaona inafaa kwamba,
Kuna uchaguzi wa ndani ya chama mwaka ujao,
tafadhali,
ikikupendeza,
usiache kuomba nafasi yoyote ya uongozi uipendayo kwenye chama chako,
hata kua mjumbe tu wa kamati ya siasa ya tawi tu. Nina hakika utapata mwanga na fursa zaidi ya kuona namna bora ya kupenyeza mawazo, mapendekezo na maoni yako ambayo daima huwa ni mazuri tu, lakini pia kupata fursa ya kushauri namna bora ya kuimarisha demokrasia ndani ya ccm.
hakuna sababu ya kujiweka pembeni bali kupambana na kuhakikisha kwamba fursa zilizopo ndani ya vyama vya siasa zinapambaniwa kwa usawa, uwazi na haki, lakini dhana za kua eti chama fulani kina wenyewe zinafutika kwenye fikra za wanachama wa chama husika.
vyama vya siasa ni mali ya umma na wanachama wake wote.