Mwamba huyu hapa

Msimu uliopita baada ya Chadrack Boka kuwa majeruhi, Nickson Kibabage ndiyo alikuwa mbadala wake! jambo ambalo liliifanya Yanga kuwa dhaifu sana kwenye huo upande.
Upande wa kulia nao Yao Kwasi alipoumia, tulishuhudia Dennis Nkane naye akichezeshwa kwenye hiyo namba! Na yeye alikuwa ni uchochoro tu!

Hivyo kwa usajili wa beki mwenye nidhamu na uzoefu kama Mohamed Hussein (Zimbwe Jr), utakuwa ni msaada mkubwa sana kwa timu ya Wananchi.
Rai yangu kwa viongozi; wahakimishe Israel Mwenda naye anabaki ili kumpa changamoto Yao Kwasi aliyekuwa majeruhi kwa muda mrefu.

Natambua kuna watu watauponda huu usajili! Ila kwa sisi ambao tumewahi kucheza na pia kuwa makocha, tunatambua fika siri ya mafanikio ya Yanga kwa miaka kadhaa sasa imejificha kwenye eneo hili la kusajili wachezaji wa kujazia mapengo yaliyo jitokeza wakati wa msimu.

Hongereni sana uongozi wa timu ya wananchi Young Africans πŸ’›πŸ’šπŸ’ͺ
Nauona tena ubingwa msimu huu. Siyo kwa hiki kikosi mlicho kisuka.
 
Katikati ya msimu: Hakuna mchezaji wa Simba anayeingia kwenye kikosi cha Yanga
Mwisho wa msimu: Mwamba huyu hapa
Vijana wa upande hawajitambui sampuli yao ni yule alielia kwenye harusi ya ali kamwe
 
YANGA tunajua kukera na hatuna jambo dogo huu msimu mpya muwe tayali Mashabiki kununua jezi 🀣🀣

JEZI IMEANDIKWA NAWADAI SIMBA Bilioni 87.

Mtanunua au?
 
Mbona risala ndeeefuu kujielezea?
Tulikubaliana ni mzee
Hakuna mchezaji wa simba anaeanza kikosi cha kwanza...
Ili mprove hyo kauli yenu mkamuweka Chama benchi
Mkude benchi
Na huyu mkomavu wa miaka 11 mtamuweka benchi mummalize...
Wenye akili ni 2 huko..
Usajili wa kukaa benchi mnamkomoa nani sasa....
 
Naona Zimbwe ameamua kuunga mkono juhudi.

Siasa za Tanzania = Mpira wa Tanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…