Mwalimu Nyerere: Ukabila na madaraka mazito mazito

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,854
35,862
Mabibi na mabwana heshima kwenu na moja kwa moja kwenye mada.

Hayati baba wa taifa (rip) alikuwa ni miongoni mwa watu ambao walikuwa wamejitanabaisha vilivyo kuwa hawakuwa wakabila.

Japo hakuna sehemu yoyote au palipo na mifano yoyote yenye kutilia shaka hilo, pekenyu pekenyu zinatanabaisha kuwapo kwa tetesi kuwa kwa maslahi mapana ya taifa mwalimu alikuwa wazi kuwa makabila fulani fulani yasiaminiwe mno. Hasa hasa kwenye kushikilia nyadhifa nzito nzito na zenye madaraka makubwa.

Kwamba kutokea kanda pendwa palikuwa na makabila yasiyopungua mawili, kaskazini (angalau) moja, na kusini kusini huku palikuwa na jingine moja kwenye hiyo listi nyeusi ya mwalimu, ni tetesi zilizopo.

Je, pana ukweli katika tetesi hizi?

Je, yanayotusibu leo kuwa tumejikuta hatimaye tuko kwenye kuhitaji mgombea:

IMG_20200804_210728_515.jpg


ni matokeo ya kutozingatia wosia huo wa baba vilivyo?

Na je pana haja ya kuanza anza kujipanga kuzingatia wosia mbalimbali za baba yetu huyo ukiwamo huu kama nao upo?

Nawasilisha.
 
  • Thanks
Reactions: _ID
Mawazo ya kikabila kabila na udini yataliangamiza taifa.

Tanzania hii tukianza kujenga mawazo ya kijima kwamba kabila fulan ndiyo bora na kabila fulani halifai ama dhaifu, wadhani mjadala utakuwa na uhai huu?

Mjadala huu wenye viashiria vya ukabila ni wa hovyo kabisa ambao haustahili kuungwa mkono wala kujadiliwa.
 
Mawazo ya kikabila kabila na udini yataliangamiza taifa.

Tanzania hii tukianza kujenga mawazo ya kijima kwamba kabila fulan ndiyo bora na kabila fulani halifai ama dhaifu, wadhani mjadala utakuwa na uhai huu?

Mjadala huu wenye viashiria vya ukabila ni wa hovyo kabisa ambao haustahili kuungwa mkono wala kujadiliwa.

Huu siyo mjadala wa ukabila.

Hizo ni nukuu tokea katika wosia.

Inafahamika kuwa mwalimu alikuwa na sababu zake nzito zilizozaa mtazamo huo kwa mujibu wa tetesi.

Kujidanganya kuwa unaweza kutokuwa mkabila kuliko Nyerere (rip) itakuwa kichekesho kidogo.

Vipi mkuu, tetesi ulizisikia? Linakuhusu au kumgusa aliyetufikisha hapa tulipo?

Inafahamika kuwa kila anapoguswa guswa malaika wa Mungu mataga hutoka povu bora la OmO.
 
Huu siyo mjadala wa ukabila.

Hizo ni nukuu tokea katika wosia.

Inafahamika kuwa mwalimu alikuwa na sababu zake nzito zilizozaa mtazamo huo kwa mujibu wa tetesi.

Kujidanganya kuwa unaweza kutokuwa mkabila kuliko Nyerere (rip) itakuwa kichekesho kidogo.

Vipi mkuu, tetesi ulizisikia? Linakuhusu au kumgusa aliyetufikisha hapa tulipo?

Inafahamika kuwa kila anapoguswa guswa malaika wa Mungu mataga hutoka povu bora la OmO.
Jinsi ulivyoanzisha mjadala ni tofauti na maudhui.

Sababu kujadili kwamba kabila fulani halifai kuongoza wakati anayeongoza ni mtu mmoja na si kabila, basi mjadala mzima mrengo wake unakuwa ni ukabila.

Ukisema 'aliyetufikisha' siyo kabila ni mtu kama nilivyosema, sasa mjadala uwe kwa kiongozi ama uongozi.

Mjadala kama utakuwa wa hivyo basi, tuanze na kupembua mawazo yako kwanza.

'Aliyetufikisha' 'ndiyo yulee asiyetajwa' na anajulikana, sasa kwa mawazo yako ni nani unayetegemea 'atatuvusha'?

Mjadili tumthaminishe.
 
Jinsi ulivyoanzisha mjadala ni tofauti na maudhui.

Sababu kujadili kwamba kabila fulani halifai kuongoza wakati anayeongoza ni mtu mmoja na si kabila, basi mjadala mzima mrengo wake unakuwa ni ukabila.

Ukisema 'aliyetufikisha' siyo kabila ni mtu kama nilivyosema, sasa mjadala uwe kwa kiongozi ama uongozi.

Mjadala kama utakuwa wa hivyo basi, tuanze na kupembua mawazo yako kwanza.

'Aliyetufikisha' 'ndiyo yulee asiyetajwa' na anajulikana, sasa kwa mawazo yako ni nani unayetegemea 'atatuvusha'?

Mjadili tumthaminishe.

Sina hakika kama umenisoma vyema. Pia Sina hakika kama tetesi hizi umewahi kizisikia. Ni wazi kuwa tetesi hizo si ngeni kama kawaida yetu wengine tumeshanuna vilivyo.

Hata hivyo kama waungwana kupekenyua, kutafiti, kuwaza na kuwazua ndiko kunako tutofautisha na lb7. Koleo huitwa kwa jina lake - huko ndiko kustaarabika.

Ifahamike kuwa:

1. Maudhui ya mada yameshenishwa na tetesi tokea katika wosia baba.

2. Baba mwenyewe (rip) anatukukuka haswa kwenye kutoamini katika ukabila.

3. Hata hivyo katika wosia wa baba anafahamu umuhimu wa demokrasia na hasa kwenye kutambua uwepo wachache na hata ambao ni disadvantaged dhidi ya walio wengi na hata wenye neema tayari. Mambo ya afya tu.

4. Makabila aliyoya-black list kistaarabu Mwalimu (rip) as per tetesi yalikuwa ni makabila yaliyokuwa makubwa zaidi au yenye fursa zaidi kuliko mengine.

Nadhani mwalimu alikuwa na hoja ndiyo maana kudumu kwa fikra zake kuliitishwa kila leo na waungwana wakaitikia: "zidumu!"
 
Mwalimu, amua umpende au umchukie kwa hakika alikuwa baba lao.

Bongo yake aliitendea haki vilivyo. Kipi alikipuuzia? Huyu angalikuwapo (rip), wengi uchwara uchwara hawa wala wasingetufikisha huku tuliko leo.

Mwalimu alikuwa na jeuri ya kumshitaki mtu kwa wenye nchi. Aulizwe yule mzee wa maruhusa ruhusa, "kwa Mungu au kwa wananchi, Mwalimu aliwananga wapi warugaruga?"

Sina uhakika ule mchakato wa wenye kheri uliishia wapi.
 
Back
Top Bottom