Mabibi na mabwana heshima kwenu na moja kwa moja kwenye mada.
Hayati baba wa taifa (rip) alikuwa ni miongoni mwa watu ambao walikuwa wamejitanabaisha vilivyo kuwa hawakuwa wakabila.
Japo hakuna sehemu yoyote au palipo na mifano yoyote yenye kutilia shaka hilo, pekenyu pekenyu zinatanabaisha kuwapo kwa tetesi kuwa kwa maslahi mapana ya taifa mwalimu alikuwa wazi kuwa makabila fulani fulani yasiaminiwe mno. Hasa hasa kwenye kushikilia nyadhifa nzito nzito na zenye madaraka makubwa.
Kwamba kutokea kanda pendwa palikuwa na makabila yasiyopungua mawili, kaskazini (angalau) moja, na kusini kusini huku palikuwa na jingine moja kwenye hiyo listi nyeusi ya mwalimu, ni tetesi zilizopo.
Je, pana ukweli katika tetesi hizi?
Je, yanayotusibu leo kuwa tumejikuta hatimaye tuko kwenye kuhitaji mgombea:
ni matokeo ya kutozingatia wosia huo wa baba vilivyo?
Na je pana haja ya kuanza anza kujipanga kuzingatia wosia mbalimbali za baba yetu huyo ukiwamo huu kama nao upo?
Nawasilisha.
Hayati baba wa taifa (rip) alikuwa ni miongoni mwa watu ambao walikuwa wamejitanabaisha vilivyo kuwa hawakuwa wakabila.
Japo hakuna sehemu yoyote au palipo na mifano yoyote yenye kutilia shaka hilo, pekenyu pekenyu zinatanabaisha kuwapo kwa tetesi kuwa kwa maslahi mapana ya taifa mwalimu alikuwa wazi kuwa makabila fulani fulani yasiaminiwe mno. Hasa hasa kwenye kushikilia nyadhifa nzito nzito na zenye madaraka makubwa.
Kwamba kutokea kanda pendwa palikuwa na makabila yasiyopungua mawili, kaskazini (angalau) moja, na kusini kusini huku palikuwa na jingine moja kwenye hiyo listi nyeusi ya mwalimu, ni tetesi zilizopo.
Je, pana ukweli katika tetesi hizi?
Je, yanayotusibu leo kuwa tumejikuta hatimaye tuko kwenye kuhitaji mgombea:
ni matokeo ya kutozingatia wosia huo wa baba vilivyo?
Na je pana haja ya kuanza anza kujipanga kuzingatia wosia mbalimbali za baba yetu huyo ukiwamo huu kama nao upo?
Nawasilisha.