Mwalimu Nyerere aliisuka 'System' ikasukika,tunaishi kwenye kivuli hicho

Sesten Zakazaka

JF-Expert Member
Sep 10, 2017
10,561
19,056
'It has been confirmed that, One of Africa's greatest sons, champion of Africa liberation, dear friend of Uganda, former President of United Republic of Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere has died' Baada ya tangazo hilo lililotolewa bungeni na aliekua Makamu wa Rais wa Uganda wakati huo Eliya Kategeya bunge zima lilipiga kimya kwa sekunde kadhaa kama limemwagiwa maji na ikaanza minong'ono na zogo la fadhaa kwa taarifa hizo za kifo cha Mwalimu. shughuli za bunge la Uganda kwa siku hiyo zika ahirishwa!

Mtakumbuka hivi karibuni Rais Museveni alipokua kwenye ufunguzi wa jengo la forodha kama sikosei, Mtukula Mkoani Kagera alifichua kwamba alikua akipita sana hapo border miaka ya nyuma kwa 'kuvunja sheria'. Alikua anapitisha silaha! Halikadhalika kwenye mazishi ya Nelson Mandela Rais Kikwete alieleza mlolongo wa viongozi na matukio ya kimkakati ambayo wapigania uhuru wa Afrika ya Kusini walipitia wakiwa Tanzania, japo watu wengine walikosoa hotuba ile kama ya kuwasimanga watu baada ya kuwasaidia, kwamba angekua Nyerere asingeweza kutoa siri hizo kama ambavyo amekufa na siri nyingi za namna hiyo.

Huyo ndio Mwalimu Nyerere anaekumbukwa kwa kutengeneza 'mifumo' ndani na nje ya nchi yake. Kwa nje ya nchi ni mtu aliyekua na weledi wa hali ya juu kabisa wa diplomasia,siasa na sheria za kimataifa. Alitengeneza viongozi wengi wa kanda yetu ya Afrika mashariki kama hao kina Museveni, Kagame na hata Raila alishawahi kufichua hadharani kwamba wakati serikali ya Moi ilipomnyima Passport ya kusafiria kwenda Ujerumani kusoma miaka hiyo Nyerere alimpatia kama raia wa Tanzania!

Aliwajua watu kwa historia, hulka na tabia zao na akizitumia kama advantage ya kumsaidia kufikia malengo yake. Ukizungumza na Waganda watakwambia hata majina ya baadhi ya wapiganaji wa jeshi la 'kuikomboa' Uganda toka utawala Idd Amin Dadaa aliyatoa yeye. Hayo ni kama ya kina Salim Salehe ambae ni ndugu wa mama mmoja na Museveni na wengine wengi ambao Mwalimu alishauri watumie majina ya kiislamu ili kuchota fikra za baadhi ya Waganda ambao walikua wanadhani Amini anaungwa mkono na waislam!

Kambi na Oparations za wapigania Uhuru wa Msumbiji, Zimbabwe na Afrika ya Kusini zilikua na ukubwa ambao usingeweza kudhania kama ulikua unaendelea Tanzania. Mambo mengi yaliratibiwa kwa siri na ustadi mkubwa na kwa uongozi na maelekezo ya moja kwa moja ya Mwalimu Nyerere.
Kwa siasa za ndani bado hajatokea bingwa wa kuweza kuzicheza kama Mwalimu. Nyerere alilijua vyema taifa lake, aliwajua watu wake na aliwajua aliokua akifanya nao kazi nguvu na udhaifu wao. Aliiunda taasisi ya intelijensia yenye weledi wa hali ya juu kwa majukumu ya ndani na nje ya nchi.
Sehemu zote kuanzia mitaani, viwandani, mashuleni na kwenye taasisi za elimu pamoja na taasisi za dini(Hasa zile kubwa kama TEC,CCT na BAKWATA) waliwekwa watu wa system ambao kazi yao ni tofauti na polisi. Taarifa kuhusu hali ya nchi na hasa usalama zilikua zinaratibiwa very systematically na usiri mkubwa ulikuwepo, tofauti na siku hizi ambapo hata Mkurugenzi na naibu Mkurugenzi wa TISS sio tu wanajulikana kwa majina bali kwa kuonekana kwenye runinga mara kwa mara. Ilikua inawezekana kwa taasisi za kidini kuwa na kiongozi asiekua wa dhehebu hilo na hakuna aliyejua!
Nyerere alipowashauri CCM waingie katika mfumo wa vyama vingi alisema inabidi CCM iratibu hiyo transition vinginevyoi mabadiliko yakitoka nje itakua tabu. Matokeo yake vikaundwa vyama ambavyo wengi ya viongozi wake na wanachama waandamizi ni watumishi wa System. Nikiwaona baadhi ya wanaodhaniwa ni viongozi imara na wafia mabadiliko wa vyama vya upinzani wanavyochota na kuchochea watu hua nachekea tumboni tu. Mwalimu Nyerere mwenyewe akitamani sana CCM imeguke vipatikane vyama viwili ambavyo hakika vingekuana na mfumo kama wa chama dola hivi, lakini vinavyodhibitiwa na dola yenyewe.
Hata mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 fundi mkuu ambaye mkono wake wa chuma haukuonekana alikua Mwalimu Nyerere(pitia kitabu cha kwaheri ukoloni kwaheri uhuru), na viongozi wengine wanaodhaniawa ni wapigania demokrasia kiuhalisia ni watu wanaochukua maagizo kutoka katika 'Mfumo" ambao Mwalimu aliuasisi
Hali hivi sasa inaanza kugeuka kwa system kufanya kazi kama ya kipolisi kitu ambacho nadhani mwasisi wake kama angekua hai leo asingelishauri hivo. Najiuliza ni weledi umepungua au uoga umezidi au mchasnganyiko wa vyote viwili? Vyovyote itakavyokua kitendo chochote cha kuimarisha nchi na tunu zake ni kitendo cha kuungwa mkono na kinyume chake kilaaniwe
 
Njerere iz ze champion of true revolution
Alikuwa zaidi ya hatali
Alikwamishwa sana na watu wake Wa karibu wenye uroho wa madaraka.
# vita ya Uganda & Tanzania 1987 aliingia front mwenyewe hadi uwanja Wa kivita.
Alikuwa na itikadi Kali aliwakatalia serikali ya kigiriki kumwachia mgiriki alieikashi serikali ya mwl
Ata ugiriki ilipomtumia rafiki take jomo Kenyatta bado alikataa
Hadi walipomtuma askofu osei tutu from s.africa ndo akamwachia kwa masharti mazito
SIJAONA RAIS KAMA NJERERE JAMANI
 
Mkoloni alisuka systems za ubaguzi za elimu yahani waroma, waagrikana, kkkt, waislamu walitofautishwa kwa shule zao lakini uyu baba kaja kan'goa mfumo huo shule zote alinyanganya
hakika anakumbukwa kwa ushujaa mwingi sana
 
Njerere iz ze champion of true revolution
Alikuwa zaidi ya hatali
Alikwamishwa sana na watu wake Wa karibu wenye uroho wa madaraka.
# vita ya Uganda & Tanzania 1987 aliingia front mwenyewe hadi uwanja Wa kivita.
Alikuwa na itikadi Kali aliwakatalia serikali ya kigiriki kumwachia mgiriki alieikashi serikali ya mwl
Ata ugiriki ilipomtumia rafiki take jomo Kenyatta bado alikataa
Hadi walipomtuma askofu osei tutu from s.africa ndo akamwachia kwa masharti mazito
SIJAONA RAIS KAMA NJERERE JAMANI
Vita ya Uganda ilipiganwa 1978-79, umahiri wa Mwalimu kama Amiri Jeshi Mkuu ulionekana pale, maana yeye ndie alikua master planner wa vita ile kimkakati, japo sio katika medani moja kwa moja. Baada ya kugundua kua Idd Amini alikua na silaha far more superior kuliko za jeshi lake alihakikisha anapiganisha vita ile ki intelijesia zaidi na ndio siri ya ushindi kwa tanzania
 
Ila Nchi Ilimshinda?Alishindwa Kuhangaika Na Matatizo Ya Nchi Yake Akadandia Ya Majirani Kwa Njia Ya Ukombozi Leo Hii Haohao Wanatusimanga Tena
Nchi haikumshinda njerere dadisi facts achana na propaganda
Njerere alipenda ujamaa zaidi ya ubepali akabuni/wakabuni N.A.M.
Ku sort out wababe Wa dunia lakini aliishi ulama a hadi mavazi yake yalisharabu UJAMAA na sera
Alipoona ulamaa umezidiwa nguvu toka juu USSR
Akamuweka mwingi ili asisaliti UJAMAA
 
Ila Nchi Ilimshinda?Alishindwa Kuhangaika Na Matatizo Ya Nchi Yake Akadandia Ya Majirani Kwa Njia Ya Ukombozi Leo Hii Haohao Wanatusimanga Tena
Hahahaaa, hakutaka kugeuka jiwe kwa akukubaliana na masharti ya kina World Bank na IMF kutokana na msimamo wake, ndio maana akaona kuliko kukubaliana nao bora aachie huo Urais aje mtu mwingine. Lakini naamini nyuma ya pazia alikua anamshauri Rais Mwinyi akubaliane na masharti flani flan ya mabeberu hawa. Nadhani kuna mahali utekelezaji ukawa tatizo kwa watu kuanza kujilimbikizia mali
 
Hahahaaa, hakutaka kugeuka jiwe kwa akukubaliana na masharti ya kina World Bank na IMF kutokana na msimamo wake, ndio maana akaona kuliko kukubaliana nao bora aachie huo Urais aje mtu mwingine. Lakini naamini nyuma ya pazia alikua anamshauri Rais Mwinyi akubaliane na masharti flani flan ya mabeberu hawa. Nadhani kuna mahali utekelezaji ukawa tatizo kwa watu kuanza kujilimbikizia mali
Angefuata Tu Ubepari Toka Awali Watanzania Wangekuwa Wamepanuka Kifikra Kwa Mbali Sana Wewe Angalia Ujamaa Ulidumaza Watanzania Mpaka Leo Hii Wanajitahidi Kujinasua
 
Nchi haikumshinda njerere dadisi facts achana na propaganda
Njerere alipenda ujamaa zaidi ya ubepali akabuni/wakabuni N.A.M.
Ku sort out wababe Wa dunia lakini aliishi ulama a hadi mavazi yake yalisharabu UJAMAA na sera
Alipoona ulamaa umezidiwa nguvu toka juu USSR
Akamuweka mwingi ili asisaliti UJAMAA
Nyerere aliipenda kidhati kabisa nchi yake. Hajawahi hata kwa kusingiziwa kuiibia nchi au kujilimbikizia mali, hata maadui zake wanakubaliana na hili. Pia aliona kua ubepari ni unyama.
Unajua mwanamuziki wa Tanzania Mbaraka Mwinshehe alifia Kenya kwenye nchi ya kibepari baada ya kupata ajali na alipopelekwa hospitali hapakua na mtu wa kudhamini malipo ya matibabu yake hadi mauti yakamkuta. Kuna watu hapa Tanzania miaka ya hivi karibuni walikutwa wanapewa matibabu kwa kutumia kadi za bima za matibabu za watu wengine wakachukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kushtakiwa mahakamani kwa kosa la jinai, Mwalimu angekua hai na yupo madarakani asingehesabu kua hilo ni kosa na labda angeweka utaratibu usio wa kibaguzi kuhakikisha kila mtu hata kama hana pesa anatibiwa maana anapigania uhai wake, ndio msingi wa ujamaa
 
Nchi haikumshinda njerere dadisi facts achana na propaganda
Njerere alipenda ujamaa zaidi ya ubepali akabuni/wakabuni N.A.M.
Ku sort out wababe Wa dunia lakini aliishi ulama a hadi mavazi yake yalisharabu UJAMAA na sera
Alipoona ulamaa umezidiwa nguvu toka juu USSR
Akamuweka mwingi ili asisaliti UJAMAA
unaongea nini wewe..nchi kukosa mahitaji muhimu sio kumshinda!?..kiwango kidogo cha literacy sio kushindwa?..huduma mbovu za afya sio kushindwa?
 
Nyerere aliipenda kidhati kabisa nchi yake. Hajawahi hata kwa kusingiziwa kuiibia nchi au kujilimbikizia mali, hata maadui zake wanakubaliana na hili. Pia aliona kua ubepari ni unyama.
Unajua mwanamuziki wa Tanzania Mbaraka Mwinshehe alifia Kenya kwenye nchi ya kibepari baada ya kupata ajali na alipopelekwa hospitali hapakua na mtu wa kudhamini malipo ya matibabu yake hadi mauti yakamkuta. Kuna watu hapa Tanzania miaka ya hivi karibuni walikutwa wanapewa matibabu kwa kutumia kadi za bima za matibabu za watu wengine wakachukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kushtakiwa mahakamani kwa kosa la jinai, Mwalimu angekua hai na yupo madarakani asingehesabu kua hilo ni kosa na labda angeweka utaratibu usio wa kibaguzi kuhakikisha kila mtu hata kama hana pesa anatibiwa maana anapigania uhai wake, ndio msingi wa ujamaa
bila hela utatoaje vitu bure..aliweza kwa kuwa alipata pesa toka kwa wajamaa,mabeberu na scandinavia..
 
Nyerere aliipenda kidhati kabisa nchi yake. Hajawahi hata kwa kusingiziwa kuiibia nchi au kujilimbikizia mali, hata maadui zake wanakubaliana na hili. Pia aliona kua ubepari ni unyama.
Unajua mwanamuziki wa Tanzania Mbaraka Mwinshehe alifia Kenya kwenye nchi ya kibepari baada ya kupata ajali na alipopelekwa hospitali hapakua na mtu wa kudhamini malipo ya matibabu yake hadi mauti yakamkuta. Kuna watu hapa Tanzania miaka ya hivi karibuni walikutwa wanapewa matibabu kwa kutumia kadi za bima za matibabu za watu wengine wakachukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kushtakiwa mahakamani kwa kosa la jinai, Mwalimu angekua hai na yupo madarakani asingehesabu kua hilo ni kosa na labda angeweka utaratibu usio wa kibaguzi kuhakikisha kila mtu hata kama hana pesa anatibiwa maana anapigania uhai wake, ndio msingi wa ujamaa
nchi yako shule na hospitali hazitoshi unajenga makambi ya wapigania Uhuru na kugharamia kuwafuga
 
bila hela utatoaje vitu bure..aliweza kwa kuwa alipata pesa toka kwa wajamaa,mabeberu na scandinavia..
Ni kweli alikua anapata misaada kutoka kwa washirika wake wa maendeleo ambao hawakua na masharti magumu na serikali pia ilikua na biashara kupitia viwanda, makampuni na mashirika ya umma. Hata hivo wakati wa mabadiliko alimuachia Rais Mwinyi aiingize nchi katika mfumo wa soko huria kwa nidhamu ile ile aliyoijenga ya kuweka maslahi ya nchi kwanza kitu ambacho hata wachina ambao tulikua tuna muelekeo mmoja wa kiitikadi wamekifanya bila kuathiri misingi ya utaifa
 
Njerere iz ze champion of true revolution
Alikuwa zaidi ya hatali
Alikwamishwa sana na watu wake Wa karibu wenye uroho wa madaraka.
# vita ya Uganda & Tanzania 1987 aliingia front mwenyewe hadi uwanja Wa kivita.
Alikuwa na itikadi Kali aliwakatalia serikali ya kigiriki kumwachia mgiriki alieikashi serikali ya mwl
Ata ugiriki ilipomtumia rafiki take jomo Kenyatta bado alikataa
Hadi walipomtuma askofu osei tutu from s.africa ndo akamwachia kwa masharti mazito
SIJAONA RAIS KAMA NJERERE JAMANI
Unamaanisha njerere au njegere au me ndo celewi....
 
nchi yako shule na hospitali hazitoshi unajenga makambi ya wapigania Uhuru na kugharamia kuwafuga
Asilimia kubwa ya ya budget ya harakati hizo haikutoka katika mapato ya nchini kwetu, nchi nyingi sana duniani zilikua zinachangia fedha, silaha na mafunzo kwa wapigania uhuru. Kikubwa alichofanya ni kukubali ardhi ya Tanzania kutumika kwa harakati hizo
 
Ni kweli alikua anapata misaada kutoka kwa washirika wake wa maendeleo ambao hawakua na masharti magumu na serikali pia ilikua na biashara kupitia viwanda, makampuni na mashirika ya umma. Hata hivo wakati wa mabadiliko alimuachia Rais Mwinyi aiingize nchi katika mfumo wa soko huria kwa nidhamu ile ile aliyoijenga ya kuweka maslahi ya nchi kwanza kitu ambacho hata wachina ambao tulikua tuna muelekeo mmoja wa kiitikadi wamekifanya bila kuathiri misingi ya utaifa
Ni kweli alikua anapata misaada kutoka kwa washirika wake wa maendeleo ambao hawakua na masharti magumu na serikali pia ilikua na biashara kupitia viwanda, makampuni na mashirika ya umma. Hata hivo wakati wa mabadiliko alimuachia Rais Mwinyi aiingize nchi katika mfumo wa soko huria kwa nidhamu ile ile aliyoijenga ya kuweka maslahi ya nchi kwanza kitu ambacho hata wachina ambao tulikua tuna muelekeo mmoja wa kiitikadi wamekifanya bila kuathiri misingi ya utaifa
1985 viwanda vilikua vinakata roho baada ya kuzalisha kwa ajili ya vita
 
Back
Top Bottom