101 East
JF-Expert Member
- Feb 25, 2015
- 1,040
- 2,121
Mkuu wa Shule ya Sekondari Sale wilayani Ngorongoro, Ngunai Gidore ameingia katika uchunguzi kutokana na tuhuma zilizoelekezwa kwake akidaiwa kuwadhalilisha wanafunzi wake wa kike.
Taarifa kutoka katika shule hiyo ambazo hata hivyo zimekanushwa na Mwalimu Gidore akisema wanaozitoa wanamuonea wivu, zinadai kuwa kwa nyakati tofauti amekuwa akiwaita baadhi ya wanafunzi nyakati za usiku na kuwafanyia vitendo vya udhalilishaji.
Hata hivyo, Kamishna wa Elimu nchini, Dk Lyabwene Mtahabwa alipotafutwa jana alisema ofisi yake haina taarifa ya suala hilo lakini itafuatilia kuanzia kwa Mdhibiti Ubora wa Elimu Kanda ya Kaskazini ili kama lipo, hatua ziweze kuchukuliwa.
Vitendo anavyodaiwa kufanywa na mwalimu hiyo ni pamoja na na kuwashurutisha kufanya nao ngono, kuwaingizia vidole sehemu za siri, kuchezea matiti, kuwatongoza na kutaka kuwakagua kama ni bikira.
Chanzo: Mwananchi
Taarifa kutoka katika shule hiyo ambazo hata hivyo zimekanushwa na Mwalimu Gidore akisema wanaozitoa wanamuonea wivu, zinadai kuwa kwa nyakati tofauti amekuwa akiwaita baadhi ya wanafunzi nyakati za usiku na kuwafanyia vitendo vya udhalilishaji.
Hata hivyo, Kamishna wa Elimu nchini, Dk Lyabwene Mtahabwa alipotafutwa jana alisema ofisi yake haina taarifa ya suala hilo lakini itafuatilia kuanzia kwa Mdhibiti Ubora wa Elimu Kanda ya Kaskazini ili kama lipo, hatua ziweze kuchukuliwa.
Vitendo anavyodaiwa kufanywa na mwalimu hiyo ni pamoja na na kuwashurutisha kufanya nao ngono, kuwaingizia vidole sehemu za siri, kuchezea matiti, kuwatongoza na kutaka kuwakagua kama ni bikira.
Chanzo: Mwananchi