Mwalimu Julius Nyerere alikuwa nabii

Mwalimu Julius Nyerere alikuwa nabii

Ili uwe nabii kwanza lazima uwe mcha Mungu.Nyerere hakuwa mcha Mungu,he belonged to this world.Kwa hiyo hakuwa Nabii kwa kigezo chochote kile.
Neno nabii linatoka na neno la Kiebrania nābî au prophētēs (kwa Kiingereza prophet) mtu mwenye maono (visionary, seer) na mwenye ujumbe wenye mantiki (rational speech) na unaogusa jamii kwa ujumla wake hasa kwa kutoa ujumbe wenye usasa (God’s now message) kwa watu husika.Mwalimu Julius Nyerere ni mmoja wa viongozi wachache duniani, ambaye anakidhi vigezo vya kuwa nabii kwa taifa letu na Afrika nzima kutokana na mchango wa maisha yake binafsi (uadilifu wake) na uongozi wake uliotukuka (kuonesha njia).

Alitumia elimu yake kwa manufaa ya wote – alikuwa akiwafundisha wakulima namna ya kutayarisha mashamba
yao kutokana na majira ya mwaka maana alijua jiografia ya nchi na majira yake vizuri.
Mwalimu alisisitiza maadali kwa viongozi wa umma na alitaka maendeleo yatokane na ushiriki wa wananchi katika kufanya kazi halali kwa juhudi na maarifa ili waweze kujitegemea. Alisisitiza ili tuendelee tunahitaji ardhi, watu, siasa safi na uongozi bora. Alikemea rushwa (adui wa haki) na uporaji wa raslimali za nchi kwa manufaa ya watu wachache. Aliona ni bora utajiri unaotokana na mali asili usubiri Watanzania waweze kuutumia wao wenyewe kuliko kuuweka rehani kama ilivyo sasa hivi.Ni wazi msisitizo wake kuhusu maadui watatu wa maendeleo – ujinga, umaskini na magonjwa – bado ni hai kwa maana hakuna maendeleo ya kweli kama maadui hao watatu bado wana nguvu.

Mchango wake katika kupiga vita adui ujinga kwa kupanua wigo wa elimu hadi ya watu wazima ni kitu cha kujivunia.
Raslimali za nchi yetu zinaporwa mchana na usiku na viongozi wanaopaswa kukemea hali hii wamekaa kimya. Baadhi yao walisubiri Mwalimu atutoke ndipo waoneshe makucha yao vizuri maana walijua hakuna atayeweza kuwanyooshea kidole na hawakuthubutu kufanya hivyo wakati akiwepo maana angewakosoa na kama walifanya walifanya kwa kujificha sana tofauti na ilivyo leo hii.Tunavyoadhimisha miaka 50 ya Uhuru na 12 tangu atutoke, hotuba zote za Mwalimu zina ujumbe wa usasa (kila hotuba aliyoitoa inaigusa jamii kwa sasa) – ni hotuba za kinabii tu zina ujumbe wa aina hii.

Sikiliza hotuba zake alizozitoa miaka ya 1950s, 1960s, 1980s na 1990s zote zina ujumbe wa sasa na hazikinzani na ndiyo maana kila hotuba yake wananchi wanapenda kuisikiliza kwa vile inawagusa kutokana na yale yanayotendeka leo hii katika nchi yetu: haki imekuwa ya kununua, raslimali za nchi zinaporwa na viongozi walioko madarakani wanahalalisha uporaji huo, matajiri wanazidi kuwa matajiri na maskini kuwa maskini, ukabila, udini na utengano vimeanza kutunyemelea.
 
Jamani inatosha Nyerere alikuwa mtu makini rais wetu wa kwanza.

Amekua tena Nabii hii kwangu ni ujinga

Nakubaliana na wewe. hii ya kumuita Kambarage alikuwa nabii ni kichekesho manake kesho na keshokutwa mtamwita Kikwete nae nabii.
 
Msibishane sana Mwl. Nyerere alikuwa na maono ndo maana hotuba zake zinakuwa ni very current na hali ya sasa nchini. . Nyerere was the Prophet!

Ngoja nikusamehe bure tu...

...Kama Mwl Nyerere ni Nabii basi akina Isaac Newton, Michael Faraday, Albert Einsten, Galileo Galilei, Aristotle na Plato itabidi tuwaite miungu kabisa??shame...
 
IMO Nyerere hakuwa nabii wala mtakatifu. Tunapotosha maana ya unabii na utakatifu.
 
Hapa ndipo ulipopotoka, kwa definition hii almost wote wenye busara, wote wanaowaongoza watu, na Wanataaluma woote utawaita Manabii...

Nikwambie tu, Nabii ni zaidi ya "Mtu anayeona mbali" (who can sees the future), Nabii ni Mtu Aliyechaguliwa na Mungu kuufikisha Ujumbe wake kwa Watu kwa niaba ya Mungu Mwenyewe, kwa kifupi ni Nabii ni Msemaji wa Mungu (God's Spokesman).

...Sasa kama Nyerere alikuwa ni God's Spokesman, wewe wasema...

Unaelewa maana ya kuwa Professor? Kabla ya kubisha jaribu kujifunza kusikiliza ili upate kujua zaidi...Kuwa na kiburi ni pamoja na kutokupenda kujulishwa upate kujua zaidi!
 
IMO Nyerere hakuwa nabii wala mtakatifu. Tunapotosha maana ya unabii na utakatifu.

Hivi unajua unaweza kuwa nabii wa shetani? Na je unajua hata nabii aweza kuwa mchawi? Soma maandiko vizuri Balamu alikuwa nani!
 
Tafakari vizuri! Soma vizuri historia ya unabii kuanzia Musa. Nani aliyewafikisha waana wa Israeli nchi ya ahadi, Musa? Manabii wote walifaulu missions zao (as you know them)? Chukulia Yesu mwenyewe: did he succeed in his mission and did even his close disciples understand and implement what he taught them? Ukisha jibu hayo maswali sasa uje kwa Nyerere na uone kama failure disqualifies one from being a prophet. Niulize: je hata Mungu amefaulu jinsi alivyotaka wanadamu wawe (wamjue yeye kama Mungu wa kweli na wamtumikie yeye tu)?


hivi unafikiri unabii unapewa tu kama cheo cha mkuu wa wilaya eeh?
 
Hapa ndipo ulipopotoka, kwa definition hii almost wote wenye busara, wote wanaowaongoza watu, na Wanataaluma woote utawaita Manabii...

Nikwambie tu, Nabii ni zaidi ya "Mtu anayeona mbali" (who can sees the future), Nabii ni Mtu Aliyechaguliwa na Mungu kuufikisha Ujumbe wake kwa Watu kwa niaba ya Mungu Mwenyewe, kwa kifupi ni Nabii ni Msemaji wa Mungu (God's Spokesman).

...Sasa kama Nyerere alikuwa ni God's Spokesman, wewe wasema...

Neno "nabii" linatumika katika maana kuu mbili: maana ya kwanza ni "general na secular" na maana ya pili ni "specific na religious". Kwa maana ya kwanza nabii ni mtu 'inspirational or charismatic' - mtu ambaye maneno na matendo yake yanagusa mioyo ya watu kwa namna wanavyoguswa naye. Maana hii inaweza pia kuwa ndani ya maana ya pili ambayo ni more spicific na katika religious - 'interpreter of God's word' au God's spokesperson' kama ulivyosema.

Maneno na matendo ya Mwalimu yanawagusa watu kwa maana ya kwanza (ingawa pia yanaweza kuwagusa kwa maana ya pili kulingana na kuguswa kwao). Kwa yale ambayo Mwalimu aliyasema na kuyatenda hapakuwa na tofauti na ndiyo maana hadi leo hii hotuba zake zina ujumbe unaowagusa watu "kwa sasa". Tunaweza kusema pia kupitia Mwalimu, Mungu anatuonesha wapi anatupa changamoto kwa mambo muhimu ambayo kama hatutayatafutia ufumbuzi tutanedelea kuongeza matatizo badala ya kuyapunguza.

Mfano, alipokuwa anazungumzia rushwa utafikiri ni jana au leo hata kama hotuba yake ilikuwa ya zamani. Hii ina maana maneno anayoyaongelea yanagusa maisha ya Watanzania maana ndiyo matatizo yao yanayowakabili leo hii. Kuwa na ujumbe unaowagusa wananchi ni tofauti na kuwafanya wauelewe na kuufanyia kazi. Na hii haiwezi kupimwa kwa mara moja. Baada ya miaka kadhaa sasa ndio baadhi ya Watanzania wanaanza kuelewa kitu alichomaanisha aliposema "tutunze raslimali zetu." Nikirejea mafundisho ya Yesu, baada ya kuwa wauaji wake wameshamwua baadhi ya watu walioshuhudia jinsi gani alivyostahimili mateso yote waliweza kusema: "Truly, this man was the son of God". Kwa nini hawakuweza kusema hivyo Yesu alipoanza kufundisha? Kwa hiyo, licha ya hoja kuwa Mwalimu alishindwa kuleta maendeleo kiuchumi (na sijaona rais ambaye ameshaleta hayo maendeleo anyway) lakini kwa ujumla Mwalimu amejitahidi kuongoza kwa maneno na matendo na sisi inabidi tuenzi yale mazuri ambayo ametuasa kuhusu miiko ya uongozi (uadilifu), rushwa (adui wa haki) na hali ya kujirundikia mali kwa kuwanyonya wengine.
 
Mtume Muhammadi SWA.. Amefanikiwa sana maana kila mja mzungu, mhindi, miafrika wote wanawaogopa muslimu maana hawaachi kujilipua so ukae nao kwa akili...
Tafakari vizuri! Soma vizuri historia ya unabii kuanzia Musa. Nani aliyewafikisha waana wa Israeli nchi ya ahadi, Musa? Manabii wote walifaulu missions zao (as you know them)? Chukulia Yesu mwenyewe: did he succeed in his mission and did even his close disciples understand and implement what he taught them? Ukisha jibu hayo maswali sasa uje kwa Nyerere na uone kama failure disqualifies one from being a prophet. Niulize: je hata Mungu amefaulu jinsi alivyotaka wanadamu wawe (wamjue yeye kama Mungu wa kweli na wamtumikie yeye tu)?
 
Kama Nyerere alikuwa Nabii alitumwa kwa kina nani? Na alikuja na kitabu gani?

Kama ni hiyo basi Nyerere ana tofauti na Yesu, au Muhamad, hawa ni Manabii
 
Tatizo wakristo mna manabii na mitume wengi sana waliojitokeza baada ya yesu kupaa mbinguni!sijui ni vigezo gani mnatumia na jee mungu anaridhia?
 
Neno "nabii" linatumika katika maana kuu mbili: maana ya kwanza ni "general na secular" na maana ya pili ni "specific na religious". Kwa maana ya kwanza nabii ni mtu 'inspirational or charismatic' - mtu ambaye maneno na matendo yake yanagusa mioyo ya watu kwa namna wanavyoguswa naye. Maana hii inaweza pia kuwa ndani ya maana ya pili ambayo ni more spicific na katika religious - 'interpreter of God's word' au God's spokesperson' kama ulivyosema.

Maneno na matendo ya Mwalimu yanawagusa watu kwa maana ya kwanza (ingawa pia yanaweza kuwagusa kwa maana ya pili kulingana na kuguswa kwao). Kwa yale ambayo Mwalimu aliyasema na kuyatenda hapakuwa na tofauti na ndiyo maana hadi leo hii hotuba zake zina ujumbe unaowagusa watu "kwa sasa". Tunaweza kusema pia kupitia Mwalimu, Mungu anatuonesha wapi anatupa changamoto kwa mambo muhimu ambayo kama hatutayatafutia ufumbuzi tutanedelea kuongeza matatizo badala ya kuyapunguza.

Mfano, alipokuwa anazungumzia rushwa utafikiri ni jana au leo hata kama hotuba yake ilikuwa ya zamani. Hii ina maana maneno anayoyaongelea yanagusa maisha ya Watanzania maana ndiyo matatizo yao yanayowakabili leo hii. Kuwa na ujumbe unaowagusa wananchi ni tofauti na kuwafanya wauelewe na kuufanyia kazi. Na hii haiwezi kupimwa kwa mara moja. Baada ya miaka kadhaa sasa ndio baadhi ya Watanzania wanaanza kuelewa kitu alichomaanisha aliposema "tutunze raslimali zetu." Nikirejea mafundisho ya Yesu, baada ya kuwa wauaji wake wameshamwua baadhi ya watu walioshuhudia jinsi gani alivyostahimili mateso yote waliweza kusema: "Truly, this man was the son of God". Kwa nini hawakuweza kusema hivyo Yesu alipoanza kufundisha? Kwa hiyo, licha ya hoja kuwa Mwalimu alishindwa kuleta maendeleo kiuchumi (na sijaona rais ambaye ameshaleta hayo maendeleo anyway) lakini kwa ujumla Mwalimu amejitahidi kuongoza kwa maneno na matendo na sisi inabidi tuenzi yale mazuri ambayo ametuasa kuhusu miiko ya uongozi (uadilifu), rushwa (adui wa haki) na hali ya kujirundikia mali kwa kuwanyonya wengine.

Kwame Nkrumah akipingana na mawazo ya Nyerere juu ya Muungano wa Afrika, na muda umeonyesha kuwa maono ya Kwame Nkrumah, miaka takribani 40 iliyopita yalikuwa sahihi na ya Nyerere yalikuwa wrong,makosa ya mawazo potofu ya Nyerere kuhusu hili,yataliandama bara la Afrika milele kama Kwame Nkrumah alivyobashiri....

" The functional conception: that African unity should be purely a matter of economic co-operation. Those who hold this view overlook the vital fact that African regional economic organizations will remain weak and subject to the same neo-colonialist pressures and domination, as long as they lack overall political cohesion. Without political unity, African states can never commit themselves to full economic integration, which is the only productive form of integration able to develop our great resources fully for the well-being of the African people as a whole. Furthermore, the lack of political unity places inter-African economic institutions at the mercy of powerful, foreign commercial interests, and sooner or later these will use such institutions as funnels through which to pour money for the continued exploitation of Africa." Kwame Nkrumah

...Kama Mwl Nyerere ni Nabii basi akina Isaac Newton, Michael Faraday, Albert Einsten, Galileo Galilei, Aristotle na Plato ingebidi tuwaite miungu kabisa??shame...
 
Jamani inatosha Nyerere alikuwa mtu makini rais wetu wa kwanza.

Amekua tena Nabii hii kwangu ni ujinga
Nakubaliana na wewe mkuu. Mwalimu alikua kiongozi aliyefanya mambo mazuri na mabaya Kama walivyobinadamu.Hili la kuwa "nabii" au "mtakatifu" kwa maana ya hadhi ya kimbingu linatia "kichefuchefu" kwa sababu kwa mtazamo wangu hastahili.
 
Kwame Nkrumah akipingana na mawazo ya Nyerere juu ya Muungano wa Afrika, na muda umeonyesha kuwa maono ya Kwame Nkrumah, miaka takribani 40 iliyopita yalikuwa sahihi na ya Nyerere yalikuwa wrong,makosa ya mawazo potofu ya Nyerere kuhusu hili,yataliandama bara la Afrika milele kama Kwame Nkrumah alivyobashiri....

" The functional conception: that African unity should be purely a matter of economic co-operation. Those who hold this view overlook the vital fact that African regional economic organizations will remain weak and subject to the same neo-colonialist pressures and domination, as long as they lack overall political cohesion. Without political unity, African states can never commit themselves to full economic integration, which is the only productive form of integration able to develop our great resources fully for the well-being of the African people as a whole. Furthermore, the lack of political unity places inter-African economic institutions at the mercy of powerful, foreign commercial interests, and sooner or later these will use such institutions as funnels through which to pour money for the continued exploitation of Africa." Kwame Nkrumah

My God! Mimi sioni kama watu wawili wakitofautiana kuhusu kitu basi mmojawapo ni lazima awe wrong. Kila mmoja alizungumzia from a certain perspective. Siamini kwamba mawazo ya Nkrumah tu ndiyo yanayofaa kuhusu muungano wa Afrika kuliko ya Nyerere and, therefore, Nyerere alikuwa wrong! Hii conclusion imetokana na premises zipi?
 
Tafakari vizuri! Soma vizuri historia ya unabii kuanzia Musa. Nani aliyewafikisha waana wa Israeli nchi ya ahadi, Musa? Manabii wote walifaulu missions zao (as you know them)? Chukulia Yesu mwenyewe: did he succeed in his mission and did even his close disciples understand and implement what he taught them? Ukisha jibu hayo maswali sasa uje kwa Nyerere na uone kama failure disqualifies one from being a prophet. Niulize: je hata Mungu amefaulu jinsi alivyotaka wanadamu wawe (wamjue yeye kama Mungu wa kweli na wamtumikie yeye tu)?

Magobe umejibu swali hili kwa hoja yenye mashiko.
 
Neno "nabii" linatumika katika maana kuu mbili: maana ya kwanza ni "general na secular" na maana ya pili ni "specific na religious". Kwa maana ya kwanza nabii ni mtu 'inspirational or charismatic' - mtu ambaye maneno na matendo yake yanagusa mioyo ya watu kwa namna wanavyoguswa naye. Maana hii inaweza pia kuwa ndani ya maana ya pili ambayo ni more spicific na katika religious - 'interpreter of God's word' au God's spokesperson' kama ulivyosema.

Maneno na matendo ya Mwalimu yanawagusa watu kwa maana ya kwanza (ingawa pia yanaweza kuwagusa kwa maana ya pili kulingana na kuguswa kwao). Kwa yale ambayo Mwalimu aliyasema na kuyatenda hapakuwa na tofauti na ndiyo maana hadi leo hii hotuba zake zina ujumbe unaowagusa watu "kwa sasa". Tunaweza kusema pia kupitia Mwalimu, Mungu anatuonesha wapi anatupa changamoto kwa mambo muhimu ambayo kama hatutayatafutia ufumbuzi tutanedelea kuongeza matatizo badala ya kuyapunguza.

Mfano, alipokuwa anazungumzia rushwa utafikiri ni jana au leo hata kama hotuba yake ilikuwa ya zamani. Hii ina maana maneno anayoyaongelea yanagusa maisha ya Watanzania maana ndiyo matatizo yao yanayowakabili leo hii. Kuwa na ujumbe unaowagusa wananchi ni tofauti na kuwafanya wauelewe na kuufanyia kazi. Na hii haiwezi kupimwa kwa mara moja. Baada ya miaka kadhaa sasa ndio baadhi ya Watanzania wanaanza kuelewa kitu alichomaanisha aliposema "tutunze raslimali zetu." Nikirejea mafundisho ya Yesu, baada ya kuwa wauaji wake wameshamwua baadhi ya watu walioshuhudia jinsi gani alivyostahimili mateso yote waliweza kusema: "Truly, this man was the son of God". Kwa nini hawakuweza kusema hivyo Yesu alipoanza kufundisha? Kwa hiyo, licha ya hoja kuwa Mwalimu alishindwa kuleta maendeleo kiuchumi (na sijaona rais ambaye ameshaleta hayo maendeleo anyway) lakini kwa ujumla Mwalimu amejitahidi kuongoza kwa maneno na matendo na sisi inabidi tuenzi yale mazuri ambayo ametuasa kuhusu miiko ya uongozi (uadilifu), rushwa (adui wa haki) na hali ya kujirundikia mali kwa kuwanyonya wengine.

Well said mkuu!

Wanaotaka kutulisha maneno yakuwa mwl alikuwa failure watuambie kwa facts alishindwa nini na wapi kisiasa kiuchumi na hata kijamii? Nami nitawaambia alifanikiwa vipi katika nyanja zote hizo....Mwl angekuwa katika dunia ya wenzetu sifa zote za Brutland waziri mkuu wa Norway zingeenda kwake...Aliyeweza kui alert dunia development principles wanazotumia siyo sustainable na wasipoangalia maisha yatakoma....

Ukisoma kitabu cha Hanna et al cha 1996 kuhusu institutions na ukasoma kazi za Ostrom Elinor; Williamson O; North Dowglass scholars wa Institutions na New Intitution Economics, wote hawa wanaelezea concept sahihi za Azimio la Arusha na scholarly articles za Mwl za Ujamaa tofauti ni kuwa hawa wengine ni wanataaluma na yeye akiwa mwanasiasa mweusi anayetakiwa kutawaliwa kiakili ili aendelee kuwa tegemezi! Hata recent work za Lans Bovernberg na Rud de Mooij wa Harvard utaona concept za Mwl zikiwa valid...Hii ni kwa upande wa theory za uchumi na maendeleo.

Ukija kijamii mwl alifanikiwa kuiunganisha jamii yetu hata tukawa na sauti mmoja inapokuja kwenye maswala ya kitaifa kuanzia watoto, vijana hadi wazee; social capital was very high kiasi kwamba imani hiyo aliyoijenga ndiyo ambayo mpaka sasa hawa mafisadi wanaringa nayo kuaptia kura kwani wengi wa watu wazima na wazee bado wanayo inside their heart.

Kiuchumi jaribu kuangalia by the time anang'atuka gap between the poor na the rich ilikuwa kiasi gani; primary school enrolment ilikuwa % ngapi na drop outs pia ni kiasi gani; Idadi ya wataalamu kulingana na ratio yake kwa population iliyokuwapo wakati huo (msije na absolute numbers no bali relative number) in terms of no. of Drs; school teachers; number of schools; hospitals na hata child mortality pia ambao walipata chanjo muhimu. Angalia GDP na GDP per capita ilikuwa kiasi gani anaglia employment ni % ngapi ilikuwa employed kuanzia viwanda; mashamba ya ushirika; mashamba makubwa; etc. Angalia export ilikuwa kiasi gani na mwisho angalia deni la nje lilikua sh. ngapi pamoja na mambo mengi ya siasa za nje kama majeshi yetu nje ya nchi; tume train viongozi wa ngapi wa bara hili na mengine mengi.

Haya ni yale yaliyomo kichwani mwangu sasa fikiria nikianza kuvitafuta si nitajaza pages za mafanikio yake Kisiasa, kiuchumi na kijamii? Leta hapa ya Rais mwingine yeyote wa Tanzania ulinganishe na yake one by one uone kulivyo na gap kubwa!
 
Concept ya mwl ilikuwa kujenga siasa ya ujamaa na kujitegemea, That was excellent despite 1+1 sio lazima kuwa 2 inaweza kuwa great or less than 3. Ona the Arusha azimio ilikuwa kujenga misingi imara ya uongozi, hatukulazimishi ukubali bali mind you mwl was in kiongozi na alikua na maamuzi hata ya kuuza kila kitu kwa hao jamaa unaopigania i mean wakoloni, but these days tunao kibao wakoloni unaopigania refered richmond, epa, deep green na wengine wengi, hakika kwa mtazamo wako hayo ni maendeleo. defenetely matumizi mabaya ya rasilimali za nchi ikiwepo rasilimali watu: unaaminiwa kusaidia wanyonge na unatumia usomi wako kuwanyonya wanyonge. Development ni Mchakato na lazima tungeweza kufika kule mwl alipokusudia, kindly bare in mind and tazana China na inchi nyingine wako juu we should have been doing the same.Mtu yeyote mwenye manufaa ndani ya utawala uliopo hawezi kusimama na kupinga jambo lolote, these days hakuna uzalendo, mtu akikabidhiwa shirika or any department akaiba fastafasta ataonekana mjanja akifanya kwa uzalendo jamii inamcheka eti kashezea chance, lazima tuwe wazalendo na tututimize wajibu wetu
 
Tafakari vizuri! Soma vizuri historia ya unabii kuanzia Musa. Nani aliyewafikisha waana wa Israeli nchi ya ahadi, Musa? Manabii wote walifaulu missions zao (as you know them)? Chukulia Yesu mwenyewe: did he succeed in his mission and did even his close disciples understand and implement what he taught them? Ukisha jibu hayo maswali sasa uje kwa Nyerere na uone kama failure disqualifies one from being a prophet. Niulize: je hata Mungu amefaulu jinsi alivyotaka wanadamu wawe (wamjue yeye kama Mungu wa kweli na wamtumikie yeye tu)?






SIJAWAHI KUSOMA COMMENT MAKINI KAMA HII HUMU JF...BIG UP MAKOBE T KWA MAJIBU MAZURI NA MAKNI KABISA YANAYOJITOSHELEZA[]
 
Tatizo wakristo mna manabii na mitume wengi sana waliojitokeza baada ya yesu kupaa mbinguni!sijui ni vigezo gani mnatumia na jee mungu anaridhia?

Ni kweli kabisa na imani yetu inakubali hilo kwa usahihi zaidi soma Waraka wa Paulo kwa kanisa la Epheso: Eph: 4:7: 11-14. akiwaambia; But unto every one of us is given grace according to the measure of the gift of christ......And gave some apostles; and some prophets; and some pastors and teachers; For perfecting of the saints, for the work of ministry, for edifying the body of christ (church): Till we all come in the unity of the faith and of the knowledge of the Son of God unto a perfect man unto the measure of the stature of the fullness of christ: That we henceforth be no tossed to and fro and carried about with every wind of doctrine by the sleight of men and cunning craftiness, whereby they lie in wait to deceive.

Kwasababu tunao hao wote ndiyo maana hatuyumbishwi yumbishwi na mambo ya udini maana tukitaka kujua future manabii wanatuambia ama wana sema neno nalo linatekelezwa na mbingu kama lilivyotamkwa; tukitaka kuelewa kuna waalimu wanatufundisha inside out kwa habari ya Mungu na haki yake; tukitaka kuteka miji tunapeleka mitume watangulie kuweka sawa mambo na hatimaye ili tusipotee tunaowachungaji wanaotulisha mema yote huku Mungu akiwa ndani mwetu sote kutuunganisha kwa pendo lake la AGAPE.
 
Back
Top Bottom