Mwalimu hakuwa Maskini!!

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
21,443
40,537
Kuna dhana isiyo sahihi inajengwa miongoni mwa watanzania kwamba Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alikuwa Maskini kwa ivo ndiyo maana alikuwa muadilifu. Kwanza kwa wasiojua pamoja na Mwalimu kuwa Mtanganyika wa kwanza kusoma kwenye Chuo Kikuu Edinburgh cha nchini Uingereza, lakini pia alitoka kwenye koo ya kichifu.

Kwa viwango vyovyote vile vya watu wa Tanganyika wa zama hizo Mwalimu hakuwa ni miongoni mwa watu unaoweza kuwaita maskini. Mwalimu baadaye miaka ya sitini alijenga nyumba yake ya Msasani kwa Mkopo na alimjengea mama yake nyumba kutokana na fedha alizopata alipoacha kufundisha Pugu ili akafanye kazi za TANU. Mtu aliyeweza kulipa mkopo baada ya kuukopa huwezi kumwita maskini!

Mtu aliyekuwa analipwa shilingi mia tano (500) kwa mwezi zama hizo za miaka ya hamsini huwezi kusema kwamba alikuwa ni maskini na eti umaskini wake huo ndiyo uliomfanya awe muadilifu. Mwalimu hakupenda kutumia madaraka yake kujitajirisha lakini si kwa hoja kwamba kuwa alikuwa maskini bali uadilifu kwake ilikuwa ni sehemu ya imani yake!
 
mwaka 59 huyo mtu yuko fresh tu na ana londo new model mumuite maskini,eti michango ilichangwa sijui wapi ya tanu asafiri.hiki kichwa hela kilikua nazo kibao tu.mengine iliua maigizo fulani

Hawa wajamaa hawazeeki toka huo mwaka yupo fresh sn kama Mugabe
 
Prof. Ndalichako zidi kukaza Point za kujiunga na chuo kikuu.
Na hizi one na Two za O& A-level rekebisha gredi ziwe kazi kuzipata.

Ona sasa huyu kijana utumbo alio andika hapa.
 
mwaka 59 huyo mtu yuko fresh tu na ana londo new model mumuite maskini,eti michango ilichangwa sijui wapi ya tanu asafiri.hiki kichwa hela kilikua nazo kibao tu.mengine iliua maigizo fulani

Asante sana very interesting!
 
mwaka 59 huyo mtu yuko fresh tu na ana londo new model mumuite maskini,eti michango ilichangwa sijui wapi ya tanu asafiri.hiki kichwa hela kilikua nazo kibao tu.mengine iliua maigizo fulani

Huoni limeandikwa tanu?hata kama humpendi,uwe mkweli
 
mwaka 59 huyo mtu yuko fresh tu na ana londo new model mumuite maskini,eti michango ilichangwa sijui wapi ya tanu asafiri.hiki kichwa hela kilikua nazo kibao tu.mengine iliua maigizo fulani

Nimeipenda sana hii, miaka hiyo nagari machache na kuna lami
 
mwaka 59 huyo mtu yuko fresh tu na ana londo new model mumuite maskini,eti michango ilichangwa sijui wapi ya tanu asafiri.hiki kichwa hela kilikua nazo kibao tu.mengine iliua maigizo fulani

Noted
 
Back
Top Bottom