Kwa heshima kubwa, napenda kuwaalika wana JF, kuja kusherehekea sikukuu ya mwaka mpya pamoja na mimi. Jinsi ya kufika kwangu rahisi sana, panda gari la Mbagala,shuka rangi 3,halafu panda magari ya Mbande mpaka Majimatitu,ukifika hapo sasa panda vigari vya kwenda Chasimba,shuka kwa Madobe,pale chukua tax mwambie akulete kwa Baba Chididi,Kisha chukua bodaboda mpaka uwanja wa Ganja,ukifika uwanjani,kodi baiskeli mpaka kwa mganga dk Kundambanda,angalia mbele Kuna msikiti pita kichochoro,mbele utakuta kibao cha shule ya Nzasa,hapo sasa nyuma ya shule tu, ndiyo kwangu,ulizia kwa Jelenga. Karibuni sana ndugu zangu tufurahie mwaka mpya kwa pamoja.