Mwakyembe: Mwanasheria anayebaka sheria kusudi

Mwakyembe: Mwanasheria anayebaka sheria kusudi

tina pole sana. maana naona nyie mmeamua kula sahan moja na mwakyembe ..ha ha ha ...sasa huku jamiiforums ndo pccb? peleka ushahid huko.siyo kuja kila siku hapa kumsema mwakyembe kisa amewabana au mmeshndana.peleken hizo data kunakohusika then mpendekeze nan anafaa ..
 
kuwa na id unknown si hoja Tina utaishia pabaya na genge lenu lote la wala rushwa hapo bandarini kwa sababu mmoja ukitiwa ndani utaeleza na washirika wako(all conspirators)
 
tina pole sana. maana naona nyie mmeamua kula sahan moja na mwakyembe ..ha ha ha ...sasa huku jamiiforums ndo pccb? peleka ushahid huko.siyo kuja kila siku hapa kumsema mwakyembe kisa amewabana au mmeshndana.peleken hizo data kunakohusika then mpendekeze nan anafaa ..

Na wewe pole sana. Kama jina lako linavyojielekeza huwezi kuwa chizi ukawa na maarifa!!!! Soma kwa makini uelewe hoja!
 
Tina,
Hii si mara yako ya kwanza kushusha tuhuma mzito mzito dhidi ya Mwakyembe na Mapande! Nakumbuka kwenye tuhuma zako za awali zili-include tabia mbaya ya Mapande kuwadhalilisha wanawake pale TPA, pamoja na mambo mengine ikiwa na kuwashika makalio bila ridhaa yao! Leo, umekuja na tuhuma zingine lakini kwa bahati mbaya zako zinakuwa juu juu wakati kati ya yale uliyotaja yangekuwa na uzito endapo yangekuwa yamewekewa nyama. Mathalani, ikiwa una uhakika kwamba Mwakyembe alishinikiza ajira kwa mtoto wa dadake basi bila shaka jina la huyo mtoto utakuwa unalifahamu unless kama na wewe umesikia tu kwa mtu kwamba yule ni mpwa wa Mwakyembe! Tuwekee hilo jina ili wasioona taabu kufuatilia wafanye hivo kwavile hili ni rahisi sana kulipatia ukweli!!!

Halikadhalika, hapa naona unajikanganya ama hueleweki. Unasema: "- Kuvunja sheria mama ya TPA (Port Act of 2004) kwa kumteua mfanyakazi wa ngazi ya chini bandari ya Mtwara kuwa mjumbe wa bodi ya Wakurugenzi wa TPA. Sheria mama hii inatamka wazi kuwa mtu yeyote mwenye maslahi yanayokinzana katika Mamlaka ya TPA asiwe mjumbe wa bodi.- Uteuzi huu umefanyika kwa makusudi, ili mjumbe huyo alinde maslahi ya Mwakyembe kwa nguvu zote, ili na yeye ajihakikishie maslahi yake binafsi kutokana na marupurupu na posho nono za bodi hiyo, hasa ikizingatiwa kuwa mteule huyo alikimbia umande na hajawahi kukanyaga darasani." Hebu tueleze hoja yako hapo ipo wapi hasa? NI kwamba aliyeteuliwa ni Junior Staff au aliyeteuliwa ana maslahi kinzani na TPA? Which is which?

Aidha unasema: "------ Uteuzi wa wajumbe wa bodi ya Wakurugenzi TPA kwa urafiki badala ya utaalamu, weledi na uzoefu katika nyanja mbalimbali, hususan sekta ya bandari ili kusimamia kwa umadhubuti taasisi hii muhimu ambayo kwayo nchi hii inaweza kuvuka kutoka kwenye dimbwi la umaskini." Hii nayo ni easily provable subject ikiwa ungitoa ikiwa imejitosheleza! Ni akina nani hao? Kwanini usiweke majina na sifa/qualification zao hapa ili tujiridhishe kwamba kweli wamechomekwa kishikaji? Mathalani, ikiwa mmoja wapo ni NasDaz mwenye Certificate ya Agriculture kutoka Naliendele, hapo kweli watu itabidi wajiulize! Ikiwa umeamua, kwanini unakuja na habari nusu nusu? Kwa staili yako ya uletaji habari haitashangaza hata kidogo watu waki-conclude kwamba ni majungu.

Anyway, mifano ipo mingi lakini thread yako inatoa somo moja tu kubwa kwamba Harrison Mwakyembe yupo on top of the most corrupt people in the country. So, kwanini tuhuma mzito kama hizo usiwe unazipa nyama ya kutosha especially kwa yale maeneo ambayo ni rahisi watu ufuatilia? Unataja kwamba Mwakyembe amekula deal kununua ardhi kwa sh.16 billion ambayo ni ya kigogo mwenzake lakini hutaki kumtaja huyo kigogo na kuishia tu kusema (jina lako tunalo). Sasa wewe kweli lengo lako ni kufichua uovu au ku-deal na Mwakyembe? Sehemu kibao unaishia tu kusema kwa maslahi yake na ....na...na....; hao wengine hutaji; what does it mean? Angalia pia ulivyohitimisha hoja yako kwa kutoa wito kwa serikali: Wito kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali naMheshimiwa Jaji Kiongozi : Chonde chonde Mheshimiwa Mwanasheria Mkuu waSerikali na Mheshimiwa Jaji Kiongozi, kwa heshima na taadhima, mnaombwa kwapamoja mfungue macho yenu muone, na masikio msikie ili mfahamu kinagaubaga,migongano na migogoro ya mwanasheria Mwakyembe, aliyebobea katika sheria nakuzivunja kwa hila, ili mchukue hatua za kinidhamu dhidi yake, kwa kuwakadhalilisha taaluma ya sheria.- Haya sio makosa ya kisiasa, bali ni uvunjwajiwa sheria, uliukwaji wa haki za binadamu na udhalilishaji wa taaluma ya sheriaambayo nyie mnaisimia vizuri." Tuhuma ulizotoa ni za ufisadi wa kutisha kiasi cha kuogofya lakini hitimisho lako ni kama unakerwa na Mwakyembe vile anavyobananga sheria na kanuni za uendeshaji; si tena ule ufisadi wa kutisha kwa maana mtu unaposema ardhi ya sh.16 billion kwa mahali kama Kisarawe; mwenye akili timamu anaweza kujiuliza ni ardhi ya namna gani hiyo; au wanataka kununua wilaya mzima? Lakini pamoja na hofu hiyo ya kutsha, unahitimisha kirahisi rahisi tu kwamba AG na Chief Judge wafahamu kinagaubaga, migongano na migogoro ya mwanasheria Mwakyembe, aliyebobea katika sheria na kuzivunja kwa hila, ili mchukue hatua za kinidhamu dhidi yake, kwa kuwa kadhalilisha taaluma ya sheria.- Haya sio makosa ya kisiasa, bali ni uvunjwaji wa sheria, uliukwaji wa haki za binadamu na udhalilishaji wa taaluma ya sheria ambayo nyie mnaisimia vizuri." where's your point really lay?


Mkuu angalao umetoa changamoto kwa mada husika sio wanaokwepa hoja kwa majibu mepesi na kejeli za kitoto. Tuzame kwenye hoja.


Hapa hoja yangu sio kutaja majina ya watu bali kuibua uvunjaji wa sheria unaofanywa na- Mwakyembe ili umma wa Watanzania wafahamu huyu jembe lao la zamani limekuwa butu.- Hivyo vyombo husika kama vile CAG, Usalama wa Taifa na TAKUKURU ni wajibu wao sasa kuchunguza ukweli na kuchukua hatua muafaka. Majina yote ya wahusika yanajulikana, lakini hoja hapa sio hao wahusika kuwepo au kutokuwepo bali huu ufisadi unaofanywa na Mwakyembe na Kipande bila kuzuiliwa na wenye mamlaka ya juu.- Sakata la ardhi ya Kisarawe linamhusisha Mh. Turky ambaye ni mbunge kutoka Zanzibar. Shinikizo la kununua ardhi hiyo alilitoa Mwakyembe kwa bodi ya TPA huko Mtwara mwezi wa Desemba. Suala kama hili kama kweli kuna- dhati ya utawala bora kwa vyombo husika, ni dhahiri kuwa uchunguzi utabaini hali halisi. Mimi dodosa hizi ninazipata kutokana na nia yangu ya kulinda rasilimali za nchi hii, na kuwaibua mafisadi kama Mwakyembe ambao wamevaa ngozi ya kondoo lakini kumbe ni mbwa mwitu.

Wajumbe wa bodi na sifa zao ni suala tu la kuzitafuta na zinapatikana bila taabu.- Hapa hoja ni kuwa uteuzi wa Mwakyembe umezingatia urafiki na uswahiba na sio sifa na uzoefu wao.- Uchambuzi wa kina kuhusu wajumbe hawa nilishaufanya kwenye angalizo langu la awali.- Kioja kikubwa ni kwamba Mwakyembe kavunja sheria mama ya TPA kwa kumteua mfanyakazi wa TPA ambaye ni kiongozi wa wafanyakazi bandarini kuwa mjumbe wa bodi hiyo, ili kumfunga mdomo, na pia kulinda maslahi ya Mwakyembe na Kipande.- Sheria mama ya TPA inakataza mtu mwenye maslahi yanayokinzana (conflict of interest) kuwa mjumbe wa bodi ya TPA. Hii sio siri wala majungu bali ni sheria ambayo Mwkyembe alipashwa kuizingatia. Ukiachilia mbali kuvunja sheria kwa ajili ya conflict of interest, mjumbe huyu wa bodi Edmund Njowoka kazi yake ni mfagizi, na alipokuwa Dar port alifanya kazi kama mfagizi wa maeneo ya nje na wakati mwingine kwenye vyoo. Sasa kweli mtu wa aina hii ambaye hakwenda shule kabisa, atatoa mchango gani katika masuala mazito ya TPA ili kuisaidia iende mbele? Hili nalo likifanyiwa uchunguzi wa kina, kila kitu kitajulikana, na wala sio majungu.

Kuhusu unyanyasaji wa kinjisia unaofanywa na Kipande kwa wanawake wa TPA, huo umejikita sio tu kwenye ngono bali pia anawanyanyapaa wanawake wote kutoka ngazi ya chini hadi juu ndani ya- TPA.- Hata wakifanya nae ngono, mwishowe anakuwaanika na kuwaumbua maungo yao yalivyo kwa washikaji wake akiwa kwenye mabaa. Ripoti ya Bodi ya TPA- iliyotolewa na John Ulanga kabla kuvunjwa mwezi Septemba 2013,- kwa kuwa walitaka kumdhibiti Kipande- ambayo pia nilishaitoa ili Watanzania mjionee jinsi Mwakyembe alivyowasaliti, hasa kuona ni jinsi gani- Mwakyembe kaigeuza TPA kuwa shamba la bibi kwa kumtumia KIpande ambaye mtaji wake mkubwa ni matusi ya nguoni kwa kila mtu, yaani wateja, wadau, wafanyakazi, wanawake, wakubwa zake, n.k. ilishatoa list ya wanawake waliodhulumiwa haki yao na Kipande.- Pia taarifa za magazeti mbali mbali zimeonyesha jinsi gani Kipande anawahamisha mabinti ambao wanakataa kuridhia haja zake za ngono kwa kuwapeleka bandari za maziwa ambako ajira zao (posts) wala hazipo kwenye ikama.- Hili suala la unyanyasaji wa wanawake TPA ni zito na tunatoa wito kwa Bi Sofia Simba, Waziri wa Jinsia, Wanawake na Watoto kufanya uchunguzi wa kina ili ikithibitika basi hatua dhidi ya Kipande zichukuliwe haraka.- Karne hii ya 21 sio ya kutumia mfumo dume kuwakandamiza kina mama, dada na mabinti zetu, bali ni haki sawa kwa wote.

Hitimisho langu sio jepesi kama unavyodhani, bali hii ni njia ya kufuata sheria ili haki itendeke.- Kwa bahati mbaya, sina uwezo wa kuhakiki uozo unaofanywa na Mwakyembe kwa kumtumia Kipande na bodi ya Wakurugenzi TPA kwa asilimia mia moja, lakini Mwanasheria Mkuu na Jaji kiongozi kwa kutumia vyomba kama vile TAKUKURU, CAG, na Usalama wa Taifa, Tume ya Haki za Binadamu, n.k wanao uwezo wa kupata ukweli kuhusu kashfa lukuki zilizoibuliwa dhidi ya Mwakyembe na KIpande ili wachukue hatua zitakazoinusuru taasisi hii muhimu sana kwa TZ na majirani zetu.
 
Last edited by a moderator:
Hii ndio Tanzania, ukifanya kazi kwa bidii/ uadilifu katika ofisi za umma watu watakutafutia zengwe tu, nahisi jamaa amewabana sana mpaka mmemuwekea mitego na bahatimbaya labda yeye amenasa.
Tuhuma ni tuhuma, pelekeni malalamiko kwenye vyombo husika.
 
Watanzania wana tabia moja ambayo mie huwa inanikera sana na wengi wao wenye tabia hii tuko humu JF. Kitu kikisemwa na somebody ambaye hajulikaniki kama hiki basi tutapinga kwa namna tunazozijua sisi ila kwa kitu hiki hiki kije kisemwe Bungeni na Mbunge let's say mtu kama Mnyika au Kange Lugola basi watu hapa JF tutakuwa kama vile bendera fuata upepo na kuwa support wabunge na kumkalia kooni mwakyembe

Inshu kama Operation Tokomeza, Epa, Richmond iwapo ile ripoti ningeiandika mie C.T.U na kuja kuiripoti hapa watu wangenisakama kama mnavyomsakama Tina hapa lakini iwapo ingefichuliwa bungeni basi ingekuwa ni kama Bomu lililolipuka

Watu wengi hawaelewi kinachoendelea TPA now

Mwakyembe kajitahidi sana kucheza na media na akili za watanzania huku yeye kaficha maovu nyingi nyuma yake

Ila watu wataelewa tu kinachoendelea
 
Watanzania wana tabia moja ambayo mie huwa inanikera sana na wengi wao wenye tabia hii tuko humu JF. Kitu kikisemwa na somebody ambaye hajulikaniki kama hiki basi tutapinga kwa namna tunazozijua sisi ila kwa kitu hiki hiki kije kisemwe Bungeni na Mbunge let's say mtu kama Mnyika au Kange Lugola basi watu hapa JF tutakuwa kama vile bendera fuata upepo na kuwa support wabunge na kumkalia kooni mwakyembe

Inshu kama Operation Tokomeza, Epa, Richmond iwapo ile ripoti ningeiandika mie C.T.U na kuja kuiripoti hapa watu wangenisakama kama mnavyomsakama Tina hapa lakini iwapo ingefichuliwa bungeni basi ingekuwa ni kama Bomu lililolipuka

Watu wengi hawaelewi kinachoendelea TPA now

Mwakyembe kajitahidi sana kucheza na media na akili za watanzania huku yeye kaficha maovu nyingi nyuma yake

Ila watu wataelewa tu kinachoendelea

Mkuu umeongea kama GT. Keep it up!
 
Back
Top Bottom