Pukudu
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 3,148
- 2,219
Leo katika uwanja wa CCM Kambarage kulikuwa na pambano LA Ligi kuu ya Vodacom, baina ya Stand Utd na Mtibwa Sugar. Mechi Hii ilisimamishwa katika dakika ya 34 baada ya mvua kubwa na kuzuia kuendelea kwa mechi. Ila hadi mpira unasimama Stand Utd Chama LA Wana!! Tulikuwa tunaongoza kwa goli moja. Lililofungwa na captain Haruna Chanongo baada ya kupokea pasi Safi toka kwa Abasarim Chidiabere
Hii ni Mara ya 3, kwa mvua kusababisha mechi ya Chama LA Wana!! Kuahirishwa! Katika mechi ya raundi ya kwanza Kati ya Mtibwa Sugar na Stand Utd, Manungu mpira ulihairishwa dakika ya Sita Stand akiwa anaongoza goli moja. Na mechi ya pill iliahirishwa dakika ya 84 Stand akiwa anaongoza goli moja.
Kwa hyo Kesho Kuna viporo 2 Kambarage asubuhi Stand na Mtibwa jion Simba na Kagera Sugar
Cc Makoye Matale, MASULE
Hii ni Mara ya 3, kwa mvua kusababisha mechi ya Chama LA Wana!! Kuahirishwa! Katika mechi ya raundi ya kwanza Kati ya Mtibwa Sugar na Stand Utd, Manungu mpira ulihairishwa dakika ya Sita Stand akiwa anaongoza goli moja. Na mechi ya pill iliahirishwa dakika ya 84 Stand akiwa anaongoza goli moja.
Kwa hyo Kesho Kuna viporo 2 Kambarage asubuhi Stand na Mtibwa jion Simba na Kagera Sugar
Cc Makoye Matale, MASULE
Last edited by a moderator: