Miziki ya sasa hivi ni kama aibu !
Kama una umri fulani itakubidi kuchagua aina za miziki .
Kwa wale mnaofahamu lugha kutokana na miziki mtakuwa mnaelewa.
Tuje kwenye miziki yetu ya ndani hapa tanzania tena kizazi hiki.
unajua tena ofisi binafsi kama unamiliki kuwa na tv ni jambo la kawaida.
Sasa chaneli iliyowekwa ikawa inapiga nyimbo hizi za vijana.
Kuna nyimbo moja ya kadada kamoja kana jiita vitu vilivyomo kwenye bustani ,mtajua kwenye bustani kunatakiwa kuwekwa nini ila sio za bustani ya vyakula.
Ile nyimbo kwa kweli ni aibu kama inavosema "mwagia ndani ,mwagia ndani chakula ya watoto"
Suala jingine kwenye miziki ya sasa kuna maneno ya ajabu ajabu na si kiburudisho.