Muundo wa muungano unaofaa huu hapa.

Muundo wa muungano unaofaa huu hapa.

Mpenda.Haki

Member
Joined
Jan 14, 2013
Posts
59
Reaction score
31
Kumekuwa na ghiriba nyingi toka kwa CCM kupinga serikali 3 na sasa wanatumia Vyombo vya Dora kuzuia mikutano ya vyama vya siasa wakati Kinana na Nape wakizunguka nchi nzima kunadi sera za CCM huku wakiwadharau, kuwakejeli na kuwabeza UKAWA. Ni hivi Bila serikali 3 hakitaeleweka. Na muundo ufuatao ndio unaofaa maana hakuna gharama yoyote itakayoongezeka kwa sababu hakuna hata mtu mmoja atakayeongezeka katika safu ya uongozi. Kitakachofanyika ni kutenga tu na kuweka mipaka kwa mambo ya Zanzibar, ya Muungano na ya Tanganyika. Wanaforum mnasemaje?



Muundo wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.jpg
 
Watakasirika wenye ndoto zao, ungeweka jusa , huku mbowe, kule juu hata lukuvi na wasira
 
Ndivyo ilivyo ila kwa sababu WM Mh Pinda ni wa Jamuhuri hilo box la Tanganyika lipo juu ya box la Zanzibar na hapo ndipo pana utata.
 
Binadamu mwenye akili timamu anajua kuwa Tanzania bara ni Tanganyika ila kwa kuwa masilahi ya muungano ni makubwa hivo inakuwa shida kwa wanaonufaika kuuweka wazi muundo huu kama unavotakiwa na wananchi.
 
Kumekuwa na ghiriba nyingi toka kwa CCM kupinga serikali 3 na sasa wanatumia Vyombo vya Dora kuzuia mikutano ya vyama vya siasa wakati Kinana na Nape wakizunguka nchi nzima kunadi sera za CCM huku wakiwadharau, kuwakejeli na kuwabeza UKAWA. Ni hivi Bila serikali 3 hakitaeleweka. Na muundo ufuatao ndio unaofaa maana hakuna gharama yoyote itakayoongezeka kwa sababu hakuna hata mtu mmoja atakayeongezeka katika safu ya uongozi. Kitakachofanyika ni kutenga tu na kuweka mipaka kwa mambo ya Zanzibar, ya Muungano na ya Tanganyika. Wanaforum mnasemaje?



View attachment 152409

Hizo Tanganyika na Zanzibar zitakuwa Majimbo au Nchi? Kama ni nchi basi hakuna tofauti na Serikali 3 za Warioba!
 
Hizo Tanganyika na Zanzibar zitakuwa Majimbo au Nchi? Kama ni nchi basi hakuna tofauti na Serikali 3 za Warioba!
Huo muundo unaeleza Muungano wa nchi mbili ambazo hazina muundo wa serikali moja kwa maana kwamba hazikuungana kwa kila kitu bali baadhi ya mambo ndo yako chini ya muungano kama ilivyo sasa. kwa hiyo kila nchi inabaki na mambo yake yale yasiyo ya muungano. Huo muundo ni sawa na ule uliopendekezwa na Watanzania kupitia kwa tume ya mabadiliko ya katiba kama inavyoelezwa na rasimu ya pili.
 
Huo muundo unaeleza Muungano wa nchi mbili ambazo hazina muundo wa serikali moja kwa maana kwamba hazikuungana kwa kila kitu bali baadhi ya mambo ndo yako chini ya muungano kama ilivyo sasa. kwa hiyo kila nchi inabaki na mambo yake yale yasiyo ya muungano. Huo muundo ni sawa na ule uliopendekezwa na Watanzania kupitia kwa tume ya mabadiliko ya katiba kama inavyoelezwa na rasimu ya pili.

Kama zikiungana bado zinabaki "Nchi" basi ndio kuvunja kwenyewe Muungano, huo muundo haufai!
 
Kama zikiungana bado zinabaki "Nchi" basi ndio kuvunja kwenyewe Muungano, huo muundo haufai![/QUOTE

Nadhani hujafanya home work yako vizuri ili kuelewa! Labda nikupe mfano, USA kila state ina serikali yake, UK kuna serikali za kingdom za Whales, Scotland na Northern Ireland na zinajulikana hivyo. Kinachovunja muungano sio wingi wa serikali bali ni utashi wa kisiasa. Kama uwepo wa serikali ya zanzibar hakuvunji muungano kwa nini kuwepo kwa serikali ya Tanganyika kuvunje muungano? Think Big!
 
Back
Top Bottom