Jatropha
JF-Expert Member
- Apr 9, 2009
- 1,151
- 199
kwa jinsi ambavyo Muswada wa Katiba uliosomwa kwa mara ya kwanza bungeni jana tara 05 Aprili 2011 ulivyokuwa na mapungufu makubwa ikiashiria kuwa upo mzaha katika maandalizi yake. Hali hii inashiria jambo moja tu, nalo ni kuwa CCM inataka kudivert attention ya watu makini katika vyama vya upinzania hususana CHADEMA ili wajishughulishe na mchakato wa Katiba na kusahau kabisa ahadi zilizotolewa wakati wa kampeni za uchaguzi wa urais 2010.
Watu wasisahau kuw CCM ina uzoefu mkubwa wa kucheza na akili za binadamu, na inafahamu fika kuwa watanzania wengi ikiwemo idadi kubwa ya wanaojiita wasomi sasa hawajui tofauti kati ya Muswada wa kuandaa mchakato wa kupitia Katiba uliosomwa bungeni na mchakato wa kuandikwa kwa Katiba mpya, ambao imekuwa ikidaiwa kwa muda mrefu sana.
Hivyo wananchi walio wengi wanaona na kuridhika kuwa tayari Serikali inatekeleza matakwa na madai upinzani ya kutaka mabadiliko ya Katiba. Hivo jitihada zozote za kuweka shinikizo zaidi kwa njia ya mandamano n.k zinaweza kutafsiriwa kama fujo na machafuko. Tusisahau CCM walivyo wazuri kutumia misamiati hiyo hususan pale wananchi watakapoanza kushuhudia machungu ya hali hizo. Ikumbukwe kuwa watanzania hawajakomaa kiasi cha kuwa tayari kujitolea kama nchi tunazoona wakishiriki katika kudai haki kwa maandamano n.k
CHADEMA inatakiwa kuhakikisha kuwa haizami moja kwa moja katika malumbano ya Katiba pekee na kusahau mambo mengine ya kitaifa kama vile kufuatilia na kufanya tathmni za kina kuhusu utekelezwaji wa ahadi zilizotolewa wakati wa kampeni; kuwambusha wananchi mara ka mara kuhusu kiwango cha utekelezwaji wake na kujikita zaidi katika kukijenga chama kutoka ngazi ya taifa kilipo sasa kushuka chini hadi ngazi za mashina, kufungu matawi na kuiingiza idadi kubwa ya wananchama shughuli ambazo mpaka sasa hazionekani kuptiwa uzito wa kutosha.
Watu wasisahau kuw CCM ina uzoefu mkubwa wa kucheza na akili za binadamu, na inafahamu fika kuwa watanzania wengi ikiwemo idadi kubwa ya wanaojiita wasomi sasa hawajui tofauti kati ya Muswada wa kuandaa mchakato wa kupitia Katiba uliosomwa bungeni na mchakato wa kuandikwa kwa Katiba mpya, ambao imekuwa ikidaiwa kwa muda mrefu sana.
Hivyo wananchi walio wengi wanaona na kuridhika kuwa tayari Serikali inatekeleza matakwa na madai upinzani ya kutaka mabadiliko ya Katiba. Hivo jitihada zozote za kuweka shinikizo zaidi kwa njia ya mandamano n.k zinaweza kutafsiriwa kama fujo na machafuko. Tusisahau CCM walivyo wazuri kutumia misamiati hiyo hususan pale wananchi watakapoanza kushuhudia machungu ya hali hizo. Ikumbukwe kuwa watanzania hawajakomaa kiasi cha kuwa tayari kujitolea kama nchi tunazoona wakishiriki katika kudai haki kwa maandamano n.k
CHADEMA inatakiwa kuhakikisha kuwa haizami moja kwa moja katika malumbano ya Katiba pekee na kusahau mambo mengine ya kitaifa kama vile kufuatilia na kufanya tathmni za kina kuhusu utekelezwaji wa ahadi zilizotolewa wakati wa kampeni; kuwambusha wananchi mara ka mara kuhusu kiwango cha utekelezwaji wake na kujikita zaidi katika kukijenga chama kutoka ngazi ya taifa kilipo sasa kushuka chini hadi ngazi za mashina, kufungu matawi na kuiingiza idadi kubwa ya wananchama shughuli ambazo mpaka sasa hazionekani kuptiwa uzito wa kutosha.