Mustafa Mkulo atoka mbio kukwepa ghadhabu ya wananchi Dumila

Nimependa sana ujasiri wa wananchi..iwe wembe huo huo utumike kwa wabunge wote wasio timiza ahadi zao.

Kweli mkuu, Ubunge usiwe uchochoro wa kujitajirisha, lazima MP awajibike ikiwa atashindwa kukidhi matarajio ya wapiga kura wake.
 
Ndiyo maana kwenye katiba mpya nilipendekeza kuwa na wagombea huru katibu wake wa chama alimtukana pumbafu .
 
[/B]

Sijakuelewa unamaanisha nini.Yaani Mtu akiwa Waziri ndio Jimbo lake liendelee kuliko Mengine?Funguka Tafadhali naona network imeshindwa kukunasa vizuri.

Tumia akili japo kidogo mkuu wapi nimesema mtu akiwa waziri jimbo lake liendelee kuliko mengine? Kinachoshamgaza ni mtu kupewa kuongoza wizara kubwa na nyeti ya taifa, wakati management ya maendeleo ya jimbo lake ni majanga.
 
Huu ni uzembe tu ... naamini hashindwi kutoa au kuchangisha hiyo hela.

Sio pesa zake, ni mfuko wa maendeleo ya jimbo ambapo kwa robo ya mwaka 2011 ilikuwa Tsh 46,865,000. (mgao upo wa awamu 3 -4) sasa jumlisha mpaka 2013. Ndo maana katoka nduki
 
Mbunge umepewa mfuko wa jimbo..wewe unageuza wa kujipatia utukufu "utapigwa tu" wananchi wanasema hivi wewe unajibu vile "watakupiga tu" Na mimi nasema "upigwe tu" Ni lazima ujue kuwa cheo ni dhamana na ukikaidi "watakupiga tu" na mimi nasema "upigwe tu" maana tumechoka!
 
Yaani huo mradi wa maji wanataka kuufisadi kama ule wa Karatu alivyoufisadi Dr. Slaa.

Maji ni UHAI...
Unauchungu wa kuporwa mke nini? Uzembe wako ndio ulisababisha mkeo akukimbie na hata hako kamalaya kanakokuhifadhi sasa hivi kana mpango wa kusepa si muda mrefu!
 
Sasa huyo mtoto wa waziri mkuu wa zaman wa chama zamani anaijua hii mada, kweli watoto wa viongozi wa MAFISADI ni majanga tu.
 
Wana bodi,

Naamini wengi mnapajua Dumila. Mji huu upo katka wilaya ya Kilosa, jimbo linaloongozwa na Mustapha Mkulo.
Leo hii takriban saa moja lililopita Mhe. Mkulo amelazimika kukimbia kabisaaa (Namaanisha kukimbia) pale wananchi wa mji huu walipoanza kupaza sauti za kumzomea baada ya kutoa majibu mabaya juu ya mradi wa maji ambao yeye aliahiti kutoa Tsh 5,000,000 toka katika Mfuko wa Jimbo tangu mwaka 2011 lakin hadi leo hajatoa na aliwahi kunukuliwa akisema hatatoa kwa madai kwamba alitukanwa na katibu wa CCM wa wilaya.

Majibu yake kwamba "... sitoi hela mpaka katibu aniombe msamaha kwa maandishi..." ndo yakaibua hasira za wananchi ambao mwaka huo wa 2011 walilazimishwa kwa vipigo kutoa kila mtu Sh 3500 tofauti na makubaliano ya kuchangia sh 2000 kwa kaya... pesa ambazo nazo zimeliwa.

Mkulo kadandia gari yake aina ya Range Rover Vogue na kutimka.

Nikiweza ntaleta picha
Nimuda muafaka kwa wananchi kuamka.
 
Huyu mzee hafai kabisa hata kidogo, hata makao ya wilaya kilosa kwa sbb ya mbunge mbovu. Hapakuwa na mawe hata mmtupie...
 
Wana bodi,

Naamini wengi mnapajua Dumila. Mji huu upo katka wilaya ya Kilosa, jimbo linaloongozwa na Mustapha Mkulo.
Leo hii takriban saa moja lililopita Mhe. Mkulo amelazimika kukimbia kabisaaa (Namaanisha kukimbia) pale wananchi wa mji huu walipoanza kupaza sauti za kumzomea baada ya kutoa majibu mabaya juu ya mradi wa maji ambao yeye aliahiti kutoa Tsh 5,000,000 toka katika Mfuko wa Jimbo tangu mwaka 2011 lakin hadi leo hajatoa na aliwahi kunukuliwa akisema hatatoa kwa madai kwamba alitukanwa na katibu wa CCM wa wilaya.

Majibu yake kwamba "... sitoi hela mpaka katibu aniombe msamaha kwa maandishi..." ndo yakaibua hasira za wananchi ambao mwaka huo wa 2011 walilazimishwa kwa vipigo kutoa kila mtu Sh 3500 tofauti na makubaliano ya kuchangia sh 2000 kwa kaya... pesa ambazo nazo zimeliwa.

Mkulo kadandia gari yake aina ya Range Rover Vogue na kutimka.

Nikiweza ntaleta picha

CHADEMA jimbo hilo 2015 mwageni sumu huko
 
Kama imefikia.wakati wananchi wanaanza zomea viongozi basi ujue woga ushawatoka. Huku tunapokwenda kutamu sana! Watu washachoshwa na ahadi hewa
 
Wana bodi,

Naamini wengi mnapajua Dumila. Mji huu upo katka wilaya ya Kilosa, jimbo linaloongozwa na Mustapha Mkulo.
Leo hii takriban saa moja lililopita Mhe. Mkulo amelazimika kukimbia kabisaaa (Namaanisha kukimbia) pale wananchi wa mji huu walipoanza kupaza sauti za kumzomea baada ya kutoa majibu mabaya juu ya mradi wa maji ambao yeye aliahidi kutoa Tsh 5,000,000 toka katika Mfuko wa Jimbo tangu mwaka 2011 lakin hadi leo hajatoa na aliwahi kunukuliwa akisema hatatoa kwa madai kwamba alitukanwa na katibu wa CCM wa wilaya.

Majibu yake kwamba "... sitoi hela mpaka katibu aniombe msamaha kwa maandishi..." ndo yakaibua hasira za wananchi ambao mwaka huo wa 2011 walilazimishwa kwa vipigo kutoa kila mtu Sh 3500 tofauti na makubaliano ya kuchangia sh 2000 kwa kaya... pesa ambazo nazo zimeliwa.

Mkulo kadandia gari yake aina ya Range Rover Vogue na kutimka.

Nikiweza ntaleta picha
Huo ni uongo kabisa. Hata ukimdanganya Mtoto aliyetumboni mwa mama yake ataukataa na ataanza kucheza tumboni mwa mama yake kupinga uongo kama huo. Sijui kama unasema uongo kiasi hicho watoto wako wanajifunza nini kutoka kwako. Kwanza haiingii akilini uongo wako huo kugeuka ukweli.
 
Huo ni uongo kabisa. Hata ukimdanganya Mtoto aliyetumboni mwa mama yake ataukataa na ataanza kucheza tumboni mwa mama yake kupinga uongo kama huo. Sijui kama unasema uongo kiasi hicho watoto wako wanajifunza nini kutoka kwako. Kwanza haiingii akilini uongo wako huo kugeuka ukweli.

haya wewe mkweli tuambie ilikuwaje,sio unaleta poroja hapa.
 
Back
Top Bottom