Musoma: CHADEMA yamponza mwenyekiti CCM, polisi watumika!

• Polisi wamsaidia kwa kupiga mabomu, risasi

na Sitta Tumma,


HALI bado ni tete kwa safu mpya ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) waliochaguliwa hivi karibuni kwa tambo kuwa watakabiliana na vuguvugu la upinzani linalokikabili chama hicho.

Zikiwa ni wiki chache tangu sekretarieti mpya ya chama hicho na baadhi ya mawaziri wazomewe katika mikoa ya Mtwara na Rukwa, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa, Abdallah Bulembo, naye ameonja kadhia hiyo mkoani Mara juzi.

Bulembo alizomewa kwenye mkutano wa hadhara kiasi cha Jeshi la Polisi kulazimika kutumia nguvu kwa kufyatua mabomu ya machozi hewani ili kutuliza munkari wa wananchi mkutanoni hapo.

Mwenyekiti huyo ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu (CC), alikumbana na zomea zomea hiyo wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika viwanja vya Shule ya Msingi Mukendo mjini hapa na kudai kuwa madiwani wa Manispaa ya Musoma wanatumia vibaya fedha za halmashauri hiyo.

Alisema serikali ya CCM imepeleka fedha kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa ofisi ya manispaa hiyo na kwamba madiwani wa CHADEMA inayoongoza manispaa hiyo wamehamisha na kuzipeleka kwenye ujenzi wa barabara bila kufuata taratibu.

"Serikali yetu ya CCM imeleta fedha nyingi hapa Musoma kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa ofisi ya manispaa, lakini madiwani wa CHADEMA wamezipeleka fedha hizo kwenye ujenzi wa barabara bila kufuata utaratibu.

"Kwa maana hiyo, uamuzi wa madiwani wa CHADEMA wa kupeleka fedha hizi kwenye ujenzi wa barabara utawatokea puani si siku nyingi, na mtakuja kuona," alisema Bulembo kisha akazomewa na wananchi.

Wakati zomeazomea hiyo ikiendelea, makundi ya vijana, kina mama na wazee waliokuwepo mkutanoni hapo, walisikika wakiimba…Nyerere, Nyerere, Nyerere jembe huku wakihoji ni kipi bora kati ya mpango wa serikali ya CCM kujenga ofisi au mpango wa CHADEMA kujenga barabara kwa ajili ya wananchi?

Hata hivyo, zomeazomea hiyo ilionekana kumkera Bulembo, ambapo alisema kuwa hata wakizidi kushangilia vitendo hivyo kwa kipindi kifupi kijacho hawatapata maendeleo kwani serikali ya CCM haiwezi kupeleka fedha kwa kulenga mradi fulani halafu madiwani wakahamisha matumizi yaliyokusudiwa.

"Baada ya miaka miwili mtalia na kusaga meno. Hakuna fedha mtakazozipata hapa kwa maendeleo na watu watafikishwa mahakamani. Mfano mzuri huyu Meya wenu Kisurura (Alex), ameletewa milioni 96 za barabara yeye akapeleka milioni 70 na kujenga barabara chini ya kiwango na mitaro hivyo hivyo," alidai na kuzomewa tena.

Baada ya kuona hali imekuwa tete, Bulembo alijaribu kutaka kubadilisha upepo kwa kumshambulia mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Godbless Lema, akisema aheshimu uamuzi wa mahakama.

Bulembo alidai kuwa Lema aliandika kwenye kitabu cha wageni nyumbani kwa Mwalimu Julius Nyerere kuwa ni mbunge wa Arusha Mjini wakati akijua si kweli, lakini kauli hiyo ilizidisha jazba kwa wananchi na kumtaka aondoke.

"Ondoka zako nyie wezi wakubwa, mmetuletea umaskini mkubwa leo mnatuambia nini hata kwa Mwalimu Nyerere hamuoni haya kwenda wakati mmefilisi nchi?

"Hivi leo mnakwenda nyumbani kwa Mwalimu mnajieleza vipi...iko siku Nyerere atakuja kufufuka, na akiwakuta mko katika kaburi lake mtajuta!" alisikika mmoja wao huku akiungwa mkono na wenzake, jambo lililomfanya Bulembo kuchukua kama dakika tatu hivi akisema CCM oyeee."

Aidha, alitoa onyo kwa wanasiasa kuacha kusimama majukwaani kumshambulia kwa maneno Rais Jakaya Kikwete, akidai kuwa kuanzia sasa uvumilivu umewashinda.

Bulembo katika hali ya kubabaika alijipachika wadhifa wa serikali kwa kuwaagiza wakuu wa wilaya na mikoa pamoja na jeshi la polisi kuwachukulia hatua wanasiasa watakaotumia majukwaa kumshambulia Rais Kikwete.

Alipokaribisha maswali, aliulizwa kuhusu baadhi ya vigogo wa CCM wanaodaiwa kuficha mamilioni ya fedha nchini Uswisi, ambapo alisema madai hayo ni uzushi wa Zitto Kabwe kwani alishindwa kuwataja wahusika.

Hata hivyo katika hatua ya kushangaza, Mkuu wa wilaya ya Musoma Mjini, Jackson Msome, alikataa kupanda jukwaani baada ya kuitwa na mwenyekiti huyo.

Baada ya mkutano huo kufikia hatua za mwisho majira ya saa 12:30 jioni, polisi walianza kuwakamata vijana waliokuwa wakiimba na kumsifu mbunge wa Musoma mjini, Vincent Nyerere (CHADEMA).

Baada ya askari polisi hao kuanzisha kamatakamata hiyo, baadhi ya wananchi walianza kuwarushia mawe polisi hao, jambo lililowalazimu kufyatua hovyo mabomu na risasi hewani na hivyo kuondoa utulivu eneo hilo
 
Hivi magamba mmekatika breki ya masaburi nini?mbona ni pumba tu kila mahali?eti nyinyiemu haitatoa fedha kwa musoma...ni zenu?Na bado tunazitaka pesa zetu za uswiss,meno ya tembo mtutajie anayewaua,msafirishaji ni katibu wenu ki-nana-si,wauza unga mwenyekiti anawajua,epa ,richmond,kiwira,kule kwenye mgodi mliosema ni wa tiss,wallah haya majinamizi hayatawaacha mpaka mtakapowajibika....nyambaffffffffffff.
 
Na Mwandishi wetu

14th December 2012

Jeshi la polisi mkoani Mara limelazimika kurusha risasi za moto ili kuwadhibiti watu waliodaiwa kuwa ni wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jimbo la Musoma mjini ambao walionekana kupinga kauli ya Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdallah Bulembo, za kudai kuwa madiwani wa halmashauri hiyo wanatumia vibaya fedha za halmashauri hiyo.

Bulembo ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM Taifa, alikumbana na hali hiyo juzi jioni wakati akihutubia wanachama wachache wa Ccm katika uwanja wa Shule ya Msingi ya Mkendo huku mkutano huo ukikumbwa na zomea zomea na kufanya kiongozi huyo kukatisha hotuba yake kila mara.

"Serikali imeleta fedha kwaajili ya kumalizia ujenzi wa ofisi ya Manispaa, madiwani wa Chadema wamehamisha fedha hizo na kuzielekeza kujenga barabara…utaratibu wa kubadili matumizi utawatokea puani siku si nyingi mtakuja kuona," alisema Bulembo na kuchafua hali ya hewa.

Kutokana na kauli hiyo, vijana,wakina mama na wazee ambao walikuwa enao la karibu na mkutano huo, walianza kuzomea.

Zomea zomea hiyo ilionekana kumkera Bulembo ambaye alisema kuwa hata wakizidi kushangilia vitendo hivyo kwa kipindi kifupi kijacho hawatapata maendeleo kwani serikali hawezi kuleta fedha kwa kulenga mradi wowote kisha madiwani wakahamisha matumizi yaliyokusudiwa.

"Baada ya miaka miwili utasaga meno hakuna fedha mtakazozipata hapa kwa maendeleo na watu watafikishwa mahakamani…mfano mzuri huyu Meya wenu Kisurura ameletewa milioni 96 za barabara, yeye kapeleka milioni 70 na kujenga barabara chini ya kiwango na mitaro hivyo hivyo," alisema Bulembo huku akiendelea kuzomewa.

Baada ya kuona hali hiyo imekuwa ngumu alijaribu kuhamia kwa Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema, Godbless Lema, akidai ameshangaa kuona kwa jinsi Lema asivyoheshimu maamzi ya mahakama kwa kitendo chake cha kuandika kwenye kitabu cha wageni nyumbani kwa Mwalimu Nyerere kuwa ni Mbune wa Arusha Mjini wakati akijua siyo mbunge wa Arusha Mjini.

Kauli hiyo ilionekana kuwachukiza zaidi watu hao ambao walikuwa wengi kuliko wale walikuwa wakimsikiliza Bulembo ma kuwatolea maneno ya kuwadukuza eneo hilo. Baada ya maneno hayo Bulembo aliwaambia waliokuwa wakimsikiliza kuwa akisema CCM oyeee, CCM oyeee, Ccm oyeee'.

Baadaye alisema kuanzia sasa CCM haitawavumilia tena watu watakapanda katika majukwaa na kuanza kumtukana na kutoa rugha za kashfa kwa Rais Jakaya Kiwete ambaye ni Mwenyekiti wa chama hicho.

Wakati mkutano ukikaribia kumalizika, polisi walianza kuwakamata ovyo vijana waliokuwa wakiimba jina la Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere, jambo lilosababisha baadhi ya vijana kurusha mawe na kuwafanya polisi kurusha risasi na kuwalazimisha waliokuwapo kukimbia.

Baadaye polisi waliondoka na baadhi ya vijana waliowakamata.


CHANZO: NIPASHE
 
Makamanda tusijali sana kukamatwa kuwekwa ndani na kuteswa hizo ndizo gharama za ukombozi! Mandela anafahamu sana! Jomo kenyatta anafahamu! Mkwawa alijiua akipinga udhalilishwaji wa aina hii! shime makamanda tusirudi nyuma watatuua watatujeruhi lakini wapo watakaobaki kunufaika na haya mapambano M4C forever!!
 
........hivyo kwa miaka miwili au mitatu iliyobaki kabla ya uchaguzi mkuu serikali ya chama hicho haitatoa fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa watu wa Musoma kwa sababu walichangua mbunge wa CHADEMA.

Fedha ni mali ya ccm au ni ya umma, mbona huyu kichefuchefu? na kwa hiyo maendeleo yanaelekezwa kwa kuhongwa?
 
mie napita tu! .....ila kuna nyeti nimepata toka hapa tff , Bulembo hana hata cheti cha form 4! Ajabu!
 
Kama ni chuki kwa wanachi ndo sasa inapamba moto

Na kama mpaka sasa hajaonywa na wakuu wake basi sikio la kufa halisikii dawaw
 
Na hao polisi wana matatizo! Sijui kama wanafahamu Polisi ni jeshi? Wanapewaje amri na mtu asiye tambulika jeshini na wao wanakubali tu?

Hivi polisi wana force number? They are more citizens than soldiers!
 
Magamba wanazidi kulowa. Maji yanazidi unga.

Wakati Mahakama ya Rufaa Kanda ya Dar es Salaam ikitoa hukumu ya kumrudishia udiwani na kumthibitisha Kamanda Ulole Ulole kuwa Diwani halali wa Kata ya Kijitonyama dhidi ya Abdalla Bulembo wa CCM leo, jana huko kwenye manispaa ya Musoma, Mwenyekiti huyo wa Wazazi Bulembo alikutana na nguvu ya umma akalazimika kuomba Jeshinla Polisi kuinusuru CCM mbele ya wananchi wa mji huo.

Ilikuwaje! Alikuwa akihutubia mkutano wa hadhara mjini Musoma siku moja baada ya mkutano wa CHADEMA chini ya Kamanda Vincent Nyerere na Godbless Lema.

Hoja akawa hana au zikamwishia au hakujiandaa kama ilivyo kawaida ya magamba. Akaanza kutukana mbunge Vincent na wananchi wa Musoma waliomchagua. Akisema CCM ndiyo wenye serikali, ndiyo wanaotoa fedha, na yeye anazungumza kama Mjumbe wa Kamati Kuu na M-NEC, hivyo kwa miaka miwili au mitatu iliyobaki kabla ya uchaguzi mkuu serikali ya chama hicho haitatoa fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa watu wa Musoma kwa sababu walichangua mbunge wa CHADEMA.

Wananchi wakavumilia. Wakaendelea kusikiliza. Unajua hata mjinga mpe muda uujue ujinga wake unapoanzia na unapoishia. Akaanza kujilinda na kujishtukia. Anasema yeyote atakayeharibu mkutano wake ataamurisha polisi wamkamate. Akatoa amri kwa polisi kuwa yeyote atakayekaidi agizo lake la kukamata raia, atafukuzwa kazi na yeye anazungumza kama Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na M-NEC. Na kwamba kuanzia sasa CCM wataagiza watumishi wote wa umma ambao wanakaidi maagizo ya viongozi wa CCM, wafukuzwe kazi mara moja.

Watu wakaendelea kuvumilia. Na ukisikia watu wa Musoma wanavumilia, basi ujue wamevumilia kweli kweli.

Akaendelea kufyatuka. Akasema, DC wa Musoma kama walivyo ma-DC wengine nchi nzima ni makada wa CCM na wajumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM ya Wilaya, hivyo watawajibika kutoa taarifa zozote zile kwenye mikutano ya CCM wala hawataweza kufanya hivyo kwenye mikutano ya Mbunge (hata kama ni mkutano wa kiserikali), kwa sababu ni mbunge wa CHADEMA.

Sasa ukawadia wakati wa maswali na majibu. Shughuli ikaanzia hapo.

Swali la kwanza; mwananchi akauliza, sasa kama CCM inasema inaweza kutoa amri kwa vyombo vya dola kuwakamata na kuwashughulikia wananchi kwa kutoa amri tu, kwa nini wasitumie amri hiyo na uwezo huo huo kuagiza mafisadi wakamatwe na fedha za Uswisi zirejeshwe. Oooh! Kosa kubwa. Bulembo akatoa amri pale pale 'kamata huyo'. Yule muuliza swali akadakwa pale pale na mmoja wa maaskari waliokuwa pale. Kitu cha kushangaza sana askari aliyekuwa akikamata ni dereva wa gari la polisi anayepaswa kuwa kwenye usukani muda wooote.

Swali la pili; mwananchi akahoji kwamba wao wanavyofahamu ni kwamba DC ni kiongozi wa kiserikali, sasa kwa nini kwenye mikutano ya CHADEMA ambayo inakuwa na watu WENGI viongozi kama yeye hawaji au hawafiki kutoa taarifa kwa wananchi badala yake wanakuja kwenye mikutano ya CCM ambayo inakuwa na watu wachache. Oooooh, kosa! Bulembo, Mwenyekiti wa Wazazi wa Magamba, akatoa amri tena mwananchi yule akamatwe. Akakamatwa palepale.

Kitumbua kikaingia mchanga. Watu uvumilivu sasa ukawashinda. Uonevu una mwisho wake wa kuvumiliwa. Mawe yakaanza kurushwa. Ikawa mawe Vs risasi za moto kutoka kwa PolisiCCM. Taarifa zinasema askari mmoja amejeruhiwa.

Mpaka mwisho jumla ya watu watano walikuwa wamekamatwa. Labda wameongeza wengine baadae.

1. Emmanuel Charles, mwalimu wa Shule ya Sekondari Mwembeni
2. Wabunda Biseko
3. Said Ally
4. Mwinyi Ramadhan
5. Bakari Ramadhan

Sasa kazi kutwa ya leo alikuwa nayo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, ambaye aligeuzwa au alijigeuza kuwa PRO wa CCM, akiwakusanya waandishi wa habari, akiwatongoza sana wasitoe hiyo habari. Haijajulikana kafanikiwa kiasi gani. Tusubiri tuone kuanzia jioni hii kwenye vyombo vya habari;

Nawasilisha wana bodi...

Gazetini:

Huyu Bulembo ni wa kuhurumiwa tu jamani, shule inamkwaza. Kiongozi kuwa na elimu ya msingi dunia ya leo ndiyo madhara yake hayo. huyu jamaa aligombea uenyekiti wa Villa Squad ya Magomeni TFF ilimuengue sababu ya kutokidhi kigezo cha elimu ambapo kiwango cha chini cha elimu kwa mgombea uenyekiti ni elimu ya kidato cha nne ambayo kenge Bulembo hana. Tusubiri tutaona mengi mwaka huu.
 
Polisi anamkataje raia bila kujiridhisha kuwa huyo raia ametenda kosa? Kuambiwa na DC au mjumbe wa NEC kuwa amkate raia haiotoshi, lazima polisi aridhike na sababu zilizotolewa. Sasa kuuliz swali ni kosa?
Hili swali linafaa aulizwe IGP
 
Magamba wanazidi kulowa. Maji yanazidi unga.

Wakati Mahakama ya Rufaa Kanda ya Dar es Salaam ikitoa hukumu ya kumrudishia udiwani na kumthibitisha Kamanda Ulole Ulole kuwa Diwani halali wa Kata ya Kijitonyama dhidi ya Abdalla Bulembo wa CCM leo, jana huko kwenye manispaa ya Musoma, Mwenyekiti huyo wa Wazazi Bulembo alikutana na nguvu ya umma akalazimika kuomba Jeshinla Polisi kuinusuru CCM mbele ya wananchi wa mji huo.

Ilikuwaje! Alikuwa akihutubia mkutano wa hadhara mjini Musoma siku moja baada ya mkutano wa CHADEMA chini ya Kamanda Vincent Nyerere na Godbless Lema.

Hoja akawa hana au zikamwishia au hakujiandaa kama ilivyo kawaida ya magamba. Akaanza kutukana mbunge Vincent na wananchi wa Musoma waliomchagua. Akisema CCM ndiyo wenye serikali, ndiyo wanaotoa fedha, na yeye anazungumza kama Mjumbe wa Kamati Kuu na M-NEC, hivyo kwa miaka miwili au mitatu iliyobaki kabla ya uchaguzi mkuu serikali ya chama hicho haitatoa fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa watu wa Musoma kwa sababu walichangua mbunge wa CHADEMA.

Wananchi wakavumilia. Wakaendelea kusikiliza. Unajua hata mjinga mpe muda uujue ujinga wake unapoanzia na unapoishia. Akaanza kujilinda na kujishtukia. Anasema yeyote atakayeharibu mkutano wake ataamurisha polisi wamkamate. Akatoa amri kwa polisi kuwa yeyote atakayekaidi agizo lake la kukamata raia, atafukuzwa kazi na yeye anazungumza kama Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na M-NEC. Na kwamba kuanzia sasa CCM wataagiza watumishi wote wa umma ambao wanakaidi maagizo ya viongozi wa CCM, wafukuzwe kazi mara moja.

Watu wakaendelea kuvumilia. Na ukisikia watu wa Musoma wanavumilia, basi ujue wamevumilia kweli kweli.

Akaendelea kufyatuka. Akasema, DC wa Musoma kama walivyo ma-DC wengine nchi nzima ni makada wa CCM na wajumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM ya Wilaya, hivyo watawajibika kutoa taarifa zozote zile kwenye mikutano ya CCM wala hawataweza kufanya hivyo kwenye mikutano ya Mbunge (hata kama ni mkutano wa kiserikali), kwa sababu ni mbunge wa CHADEMA.

Sasa ukawadia wakati wa maswali na majibu. Shughuli ikaanzia hapo.

Swali la kwanza; mwananchi akauliza, sasa kama CCM inasema inaweza kutoa amri kwa vyombo vya dola kuwakamata na kuwashughulikia wananchi kwa kutoa amri tu, kwa nini wasitumie amri hiyo na uwezo huo huo kuagiza mafisadi wakamatwe na fedha za Uswisi zirejeshwe. Oooh! Kosa kubwa. Bulembo akatoa amri pale pale 'kamata huyo'. Yule muuliza swali akadakwa pale pale na mmoja wa maaskari waliokuwa pale. Kitu cha kushangaza sana askari aliyekuwa akikamata ni dereva wa gari la polisi anayepaswa kuwa kwenye usukani muda wooote.

Swali la pili; mwananchi akahoji kwamba wao wanavyofahamu ni kwamba DC ni kiongozi wa kiserikali, sasa kwa nini kwenye mikutano ya CHADEMA ambayo inakuwa na watu WENGI viongozi kama yeye hawaji au hawafiki kutoa taarifa kwa wananchi badala yake wanakuja kwenye mikutano ya CCM ambayo inakuwa na watu wachache. Oooooh, kosa! Bulembo, Mwenyekiti wa Wazazi wa Magamba, akatoa amri tena mwananchi yule akamatwe. Akakamatwa palepale.

Kitumbua kikaingia mchanga. Watu uvumilivu sasa ukawashinda. Uonevu una mwisho wake wa kuvumiliwa. Mawe yakaanza kurushwa. Ikawa mawe Vs risasi za moto kutoka kwa PolisiCCM. Taarifa zinasema askari mmoja amejeruhiwa.

Mpaka mwisho jumla ya watu watano walikuwa wamekamatwa. Labda wameongeza wengine baadae.

1. Emmanuel Charles, mwalimu wa Shule ya Sekondari Mwembeni
2. Wabunda Biseko
3. Said Ally
4. Mwinyi Ramadhan
5. Bakari Ramadhan

Sasa kazi kutwa ya leo alikuwa nayo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, ambaye aligeuzwa au alijigeuza kuwa PRO wa CCM, akiwakusanya waandishi wa habari, akiwatongoza sana wasitoe hiyo habari. Haijajulikana kafanikiwa kiasi gani. Tusubiri tuone kuanzia jioni hii kwenye vyombo vya habari;

Nawasilisha wana bodi




Gazetini:

Huyu mheshimiwa ni kati ya mafisadi kupindukia!

1.Fisadi namba 1


2.Ni taqpeli wa kutupwa



3.Ni mzazi mzuri (Mwigulu mchemba cha mtoto)


Tusitegemee chochote kwake tusubiri tuone niliyoyata hapo juu yanaongezeka,anamikataba ya kihuni kupindukia katika halmashauri ,manispaa na majiji.moja kati ya kampuni zake inaitwa New Metro.ametusumbua sana hapa Arusha na vijana wake.Pesa yote alikuwa anachukua yeye na manispaa ilikuwa inachukua kiduchu.Huyu ndie bulembo.
 
Back
Top Bottom