Museven hata wewe?


"Mwalimu Nyerere akaona ni vema ikawa jioni ikawa asubuhi Mwalimu akamwambia Museveni chukua vijana wako wa uzao wako walete hapa kambini Bukoka nao wawe pamoja nawe wakipata mafunzo pamoja nawe kumkabili hasimu wako Idd Amini."
Na katika vijana wake aliowachukua na kuwaleta walikuwamo akina Kagame. Sasa anakabiliwa na tatizo awakane vijana wake au baba yake!
 
Huu upuuzi wote wa hivi vinchi vidogo vidogo umeletwa na CCM kushindwa kusimamia Uchumi imara bila utegemezi kushinndwa kuikemea RUSHWA Mungu ametupa nchi Yenye kila kitu utajiri mkubwa wa Rasilimali CCM imeshindwa Kuendeleza Bandari ya Dar Es salaam imeshindwa kujenga Reli ya kati hivyo vyote ni Muhimili wa uchumi imekalia longolongo tu Waachezi watutenge Udhaifu wa CCM ndio matunda yake haya
 
Watu wanasema Mda ni jaji mzuri, acheni kupiga kelele, waacheni wafanye watakalo. Tujikiteni ktk tamaduni zenye kuheshemu kazi na miiko ya kazi.

shirikisho halina faida yoyote mara nyingi ni hasara tu. Nchi zilizo ktk EU wana matatizo makubwa kuliko nchi ambazo hazimo EU kama vile Switzerland, Norway nk. Hata UK wanampango wa kupiga kura kujitoa EU. Na angalia hizi nchi zinapata msukomsuko wakati viongozi wake wanafuata miiko ya kazi.

Tupigeni makofi kwa kushangilia kwamba ni wao wenyewe wameamua kututoa, sioni cha kusikitika hapo zaidi ya furahaa. Furahieni na mpige vigelegele
 
Kumtetea JK inabidi uwe na roho ya chuma. Hasa nikikumbuka vijana wa JK walipofanya mambo ya ovyo kwa Mwangosi,Arusha,Morogoro,Mtwara na Ulimboka na mpaka leo hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kwa wahusika zaidi ya Usanii.Sipendi kuwa mzalendo wa kinafiki.
 


Kumbuka Julius Caesar pigo la mwisho kisu na lililommaliza lilitoka kwa rafiki yake Brutus. There is no way we should be trusting Mseven!!
 
Mkuu mbona majeshi ya M7 na Kagame waliwahi kupigana vikali huko Congo, mahusiano yao si rahisi kuyaelewa - nasikia kuna wakati M7 na Kagame walikuwa hawa pikiki chungu kimoja, walikaa zaidi ya nusu mwaka bila ya kujuliana hali!! Watanzania tutegemee nini kutoka kwa such an odd PAIR ambao wako highly unpredictable.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…