AZUSA STREET
JF-Expert Member
- Oct 31, 2013
- 2,007
- 1,893
Eee Mungu, Muumba wa mbingu na nchi, wewe ndiwe Mungu wa kweli, wewaza kutuokoa hata sasa. wewe ni Mungu wa haki, haki hutawala mbele zako milele na uovu na dhuluma hazitakushida wewe. Tunakuomba iponye Tanzania, tunakuomba ikomboe Tanzania, tuokoe toka kwenye mikono ya watesaji, wauawaji, wale wanaoleta huzuni katika mioyo ya watu, wale wanaotesa raia wasio na hatia, wao wanategemea nguvu za mwili, wanategemea waganga wa kienyeji, wanategemea bunduki na silaha za mwili, sisi tunakutegemea wewe Mungu ambaye haujawahi kushindwa, na hautakuja kushinda milele, uweza wako ni wa milele, nguvu zako ni za milele, haki yako hutawala milele na hautamwacha mtu atuonee milele.
usifurahi eeh adui yangu, niangukapo nitasimama tena. Eeh Mungu tunayaleta haya kwalo leo, yale yanayotuumiza mioyo yetu:
usifurahi eeh adui yangu, niangukapo nitasimama tena. Eeh Mungu tunayaleta haya kwalo leo, yale yanayotuumiza mioyo yetu:
- Angalia Tundu Lisu alipigwa risasi mchana na watu wasiojulikana
- Angalia binti wa watu jana anatoka shule amepigwa risasi Kinondoni
- Angalia watu wanavyookotwa kwenye fukwe za bahari
- Angalia watu wanavyoishi kwa hofu na mashaka, hawana amani
- Angalia uchumi ulivyodorora, hakuna pesa mtaani, shida zimezidi
- Angalia watoto wetu wanavyokosa mikopo vyuo vikuu, ni wengi mno
- Angalia mishahara ya watumishi haipandishwi wala vyeo vyao
- Angalia watu wanavyofukuzwa kazi kwa upendeleo
- Angalia watu wanavyokamatwa bila makosa ya msingi na ya haki
- Angalia wanaosemekana na vyeti feki wamefukuzwa lakini wapo wengine hawafukuzwi
- Angalia watu walivyokosa furaha na amani,