Zamaulid
JF-Expert Member
- May 25, 2009
- 18,653
- 13,472
ni last week tu nimetoka home kuja huku ninako hangaikia maisha ya famila!jana nimeongea na wife kwa skype hadi saa 4 usiku!!asubuhi napigiwa simu na namba ya jirani 'nipigie mimi mkeo usiku tumevamiwa na majambazi'!tulipomaliza kuskype anajilaza kidogo kama saa 6 majambazi yakafika yakaanza kuvunja mlango kwa zaidi ya nusu saa yakafanikiwa kuingia ndani!!yana taka dola!!!jamani dola kweli majohe zitoke wapi!!wakachukua laptop na hela kidogo waliyoikuta ndani!!wakabeba simu za majirani pia wanaokuja kucharge hapo home wakachukua ufunguo wa gari na fujo nyingi!!zoezi zima limechukua zaidi ya saa nzima,walipotaka kutoka wakadondosha ufunguo,nasikia wameutafuta bila mafanikio!!cha kumshukuru Mungu ni kwamba wamechua walichoweza ila wameacha uhai wa familia!kweli MUNGU ANAIPENDA FAMILIA YANGU!