Mullen: China now a world power

Serikali ya marekani na raia wa marekani ni vitu viwili tofauti, inapokuja kwenye maswala ya nchi hakuna mambo ya utu bali ni maslahi tuu

Pamoja na marekani kuwa na maslahi binafsi, lakini hata ile democratic stability waliyonayo ukilinganisha na China, ni bora Marekani maamuzi yako decentralized kidogo walau kuna usalama. Lakini China siyo nchi ya kupewa nafasi kabisa maana kitakachotokea duniani Mungu peke yake ndo anajua.

Kwanza tutarajie tu kuwa china itasambaratika siku yoyote ile maana inakwenda against nature haiamini katika uhuru wa kutoa maoni, haiamini katika haki za binadamu, pamoja na mafanikio makubwa ya kiuchumi lakini wachina wengi hawajui kinachoendelea duniani. Serikali imedhibiti habari za nje, ni CCTV 9 tu inayotoa habari ambazo pamoja na kuchujwa sana lakini walau zina sura ya kimataifa hata hivyo wachina hawatumii CCTV 9 kwa sababu karibu 95% ya wachina hawajui kiingereza. Chanel zingine zaidi ya 30 ambazo nazo ziko chini ya CCTV zinatangaza kwa kichina lakini hizo ukiziangalia hata kama hujui kichina utagundua kuwa zimekaa kipropaganda kama ilivyokuwa kwa vyombo vya habari enzi za Nyerere. Ni kuwasifu viongozi wa kisiasa, na kuonesha jinsi china ilivyoonewa na mataifa makubwa, hata mgogoro wa tibet watu nje ya china wana habari nyingi sahihi kuliko wachina wenyewe.
Kwahiyo kinachotokea Arabuni sasa kitatokea china pia japo sio siku za karibuni. Itachukua mda mrefu wachina kutambua haki zao lakini siku wakitambua basi yanayotokea Arabuni yatatokea. Na yakitokea basi Marekani ikae sawa kwasababu kama Marekani itaanza kurusha mpira kama inavyorusha huko Syria, Yemen na Bahrain kwasababu za kimaslahi basi mauaji yatakayotokea hayajapata kutokea maana ile sio serikali.

Sasa nchi kama hiyo haiwezi kuvaa viatu vya Marekani duniani labda kama tunataniana. Tunaweza kuwa tunachukizwa na jinsi ambavyo Marekani inashughulikia baadhi ya matatizo kwa kuzingatia maslahi zaidi. Lakini dunia kuongozwa na Marekani ya sasa ni salama zaidi kuliko kuongozwa na china ya sasa, labda china ifanye mabadiliko makubwa ya kiuongozi.
 
Pamoja na marekani kuwa na maslahi binafsi, lakini hata ile democratic stability waliyonayo ukilinganisha na China, ni bora Marekani maamuzi yako decentralized kidogo walau kuna usalama. Lakini China siyo nchi ya kupewa nafasi kabisa maana kitakachotokea duniani Mungu peke yake ndo anajua.
Tatizo hapo tunalinganisha machungwa na ndizi, huwezi linganisha Marekani na China hata kidogo, historia na utamaduni wao ni tofauti. Mambo yaliyowezekana Marekani sirahisi kuyafanyika China.

Kwanza tutarajie tu kuwa china itasambaratika siku yoyote ile maana inakwenda against nature haiamini katika uhuru wa kutoa maoni, haiamini katika haki za binadamu, pamoja na mafanikio makubwa ya kiuchumi lakini wachina wengi hawajui kinachoendelea duniani.

Sirahisi kusambaratika na haya mambo ya kujua wanagharibi wanasema nini sio dili kwasababu hata wachina wakawaida wakijua Sen. Tom Coburn kasema nini haina tija kwa maisha yao kilasiku ni sisi wabongo tuu ndo huwa tunapapalikia mambo ya nje.

Hata Marekani kwenyewe vyombo vyote vya habari havisemi ukweli (vipo kipropaganda zaidi). Huwa hawatoi habari za uhalisia zaidi ya zile za kipropaganda juu ya mambo ya nje, Chaneli kama za aljazira, DW, Sky News, CNN international na BBC huwa hazipatikani kwenye chaneli za kawaida (abc, cbs, fox, news, mnsnbc n.k) ambazo zinatumiwa na wamarekani wa kawaida.

Taifa lolote kubwa haliwezi huwa hivyo bila ya kujenga utamaduni wa kuwapumbaza wananchi wake.Marekani inafanya hivyo pia, we angalia mfumo wa elimu ya msingi ya marekani utaona jinsi watoto wanavyokuwa brainwashed. Hawafundishi jiografia ya dunia kama sisi tulivyosoma bongo, hii yote ni kupumbaza jamii isijue chochote kuhusu nje ya Marekani ili iweze kutawaliwa. Mfano mzuri ni huduma za afya ya jamii, wamarekani wengi wameaminishwa kuwa gharama kubwa za matibabu nchini kwao ni kutokana na ubora wa huduma za afya binafsi lakini hii si kweli, Cuba jirani zao ambao matibabu yao ya serikali ni bure wanawazidi kwa ubora.

Sasa wamarekani wengi hayajui haya kwasababu hawapati habari hizi kwenye vyombo vya habari. Sasa unaweza kuniambia mbona Wamarekani wanaweza kupata haya kwenye mtandao? Tatizo ni kwamba kama hujui hata ukweli upi wa kuutafuta kwenye mtandao huwezi jua neno gani la ku-google.

Sasa nchi kama hiyo haiwezi kuvaa viatu vya Marekani duniani labda kama tunataniana. Tunaweza kuwa tunachukizwa na jinsi ambavyo Marekani inashughulikia baadhi ya matatizo kwa kuzingatia maslahi zaidi. Lakini dunia kuongozwa na Marekani ya sasa ni salama zaidi kuliko kuongozwa na china ya sasa, labda china ifanye mabadiliko makubwa ya kiuongozi.

Tunahitaji China na hata Afrika kama ikiwezekana ili kuwa na uwiano wa uongozi duniani, hata hiyo Marekani yenyewe wana sheria ya uwiano wa umiliki (sherman Antitrust Act) ambayo inazuia mtu/chombo kimoja kutawala kila kitu bila ya kuchunguzwa na serikali waliweka hii sheria kuzuia ukiritimba wa watu kama wakina Bill gates (software) na John D. Rockafellar(mafuta na chuma). Kwasasa wamarekani ni wakiritimba katika kila kitu, tunahitaji uwiyano katika dunia hii ya sasa.
 
Tatizo hapo tunalinganisha machungwa na ndizi, huwezi linganisha Marekani na China hata kidogo, historia na utamaduni wao ni tofauti. Mambo yaliyowezekana Marekani sirahisi kuyafanyika China.



Sirahisi kusambaratika na haya mambo ya kujua wanagharibi wanasema nini sio dili kwasababu hata wachina wakawaida wakijua Sen. Tom Coburn kasema nini haina tija kwa maisha yao kilasiku ni sisi wabongo tuu ndo huwa tunapapalikia mambo ya nje.

Hata Marekani kwenyewe vyombo vyote vya habari havisemi ukweli (vipo kipropaganda zaidi). Huwa hawatoi habari za uhalisia zaidi ya zile za kipropaganda juu ya mambo ya nje, Chaneli kama za aljazira, DW, Sky News, CNN international na BBC huwa hazipatikani kwenye chaneli za kawaida (abc, cbs, fox, news, mnsnbc n.k) ambazo zinatumiwa na wamarekani wa kawaida.

Taifa lolote kubwa haliwezi huwa hivyo bila ya kujenga utamaduni wa kuwapumbaza wananchi wake.Marekani inafanya hivyo pia, we angalia mfumo wa elimu ya msingi ya marekani utaona jinsi watoto wanavyokuwa brainwashed. Hawafundishi jiografia ya dunia kama sisi tulivyosoma bongo, hii yote ni kupumbaza jamii isijue chochote kuhusu nje ya Marekani ili iweze kutawaliwa. Mfano mzuri ni huduma za afya ya jamii, wamarekani wengi wameaminishwa kuwa gharama kubwa za matibabu nchini kwao ni kutokana na ubora wa huduma za afya binafsi lakini hii si kweli, Cuba jirani zao ambao matibabu yao ya serikali ni bure wanawazidi kwa ubora.

Sasa wamarekani wengi hayajui haya kwasababu hawapati habari hizi kwenye vyombo vya habari. Sasa unaweza kuniambia mbona Wamarekani wanaweza kupata haya kwenye mtandao? Tatizo ni kwamba kama hujui hata ukweli upi wa kuutafuta kwenye mtandao huwezi jua neno gani la ku-google.



Tunahitaji China na hata Afrika kama ikiwezekana ili kuwa na uwiano wa uongozi duniani, hata hiyo Marekani yenyewe wana sheria ya uwiano wa umiliki (sherman Antitrust Act) ambayo inazuia mtu/chombo kimoja kutawala kila kitu bila ya kuchunguzwa na serikali waliweka hii sheria kuzuia ukiritimba wa watu kama wakina Bill gates (software) na John D. Rockafellar(mafuta na chuma). Kwasasa wamarekani ni wakiritimba katika kila kitu, tunahitaji uwiyano katika dunia hii ya sasa.

Kuhusu suala la uwiano nakubaliana na wewe lakini pamoja na hayo binadamu kwa asili wanapenda haki na uhuru, kwahiyo hata kama panahitajika uwiano lakini China haiwezi kuwa nchi ya kuleta uwiano katika ulimwengu wa kidemokrasia ila ni nchi inayotaka kuleta mfumo mbadala wa demokrasia.

Kuhusu kinachoendelea ndani ya china juu ya TVs ni tofauti na unachosema, TVs kama Aljazeera, BBC, CNN etc hazipatikani kabisa labda kama zimeanza kuanzia 2009. Ni tofauti na US na TZ kwamba mtu haangalii Aljazeera kwa sababu ya sababu zake mwenyewe lkn akitaka anaweza ku-access.

Kuhusu huduma bora za afya Cuba kuliko Marekani, labda ilikuwa zamani. Sasa hivi pamoja na Cuba kuwa na uwiano mzuri wa daktari kwa wagonjwa lkn commitment yao iko chini na facilities ni poor kwa kiasi ambacho sio rahisi kulinganisha na Marekani.

Hata hivyo si kwamba mie ni muumini wa USA la hasha ila nataka tuwekane sawa kwamba hata kama tutakuwa na mataifa makubwa mengi zaidi lkn lazima mataifa yawe na mtazamo wa kisera na kimtazamo wa kulinda na kuendeleza uhuru, haki na ustawi wa binadamu.
 
Kuhusu suala la uwiano nakubaliana na wewe lakini pamoja na hayo binadamu kwa asili wanapenda haki na uhuru, kwahiyo hata kama panahitajika uwiano lakini China haiwezi kuwa nchi ya kuleta uwiano katika ulimwengu wa kidemokrasia ila ni nchi inayotaka kuleta mfumo mbadala wa demokrasia.

Unajua hii ulimwengu wa demokrasia inanikumbusha wakati wa utawala wa Bush walipokuwa wakimsema Putin eti nchi yake haina demokrasia, jamaa akasema hii ndiyo demokrasia yetu (Russian democracy), ni tofauti na ile ya kimagharibi. Ndiyo maana nikasema hapo mwanzo kuwa haya mambo yanategemeana na utamaduni wa watu. Marekani yenyewe kwa watu waiso wamarekani wanaweza kusema Raisi wao hachaguliwi kidemokrasia kwasababu huchaguliwa kwa kura za majimbo (electoral vote) badala ya wingi wa kura (popular votes).

Kwahiyo utambulizi wako wa demokrasia ya dunia kuwa sawa kila sehemu haiwezekani kwasababu kila nchi iko tofauti. Ukiangalia ukubwa wa China (1.3bil) si rahisi kuruhusu watu wajifanyie wanavyotaka hii italeta vurugu na serikali haita weza kudhibitu ghasia.

kuhusu mfumo mbadala bado sijakupata vizuri naomba maelezo zaidi na pia kama China isiwe moja ya super power je nchi iwe mbadala?
 
Back
Top Bottom