sinapindu
Member
- Nov 27, 2010
- 45
- 43
Habari za jioni!
Naomba msamaha iwapo nitakuwa mkosefu katika ufikishaji wa fikra zangu hapa, nimekuwa kimya kwa muda nikisoma mengi hapa na kufanya tafakuri kuangalia mashiko ya hoja katika mijadala mbalimbali lakini hatmae nimegundua katika ung'amuzi wangu kuwa kuna tatizo la kutoichanganua CHANYA.
Pengine nitakuwa sielewi vema uhali chanya ni upi?au ukoje?katika uhalisia wake, hivyo nitatarajia kuelimishwa na kufahamishwa kwa kina, lakini pengine nanyi mnaelewa vema UCHANYA au mnaelewa vema ndivyo sivyo uchanya ulivyo, hapo hati hii itakuwa somo mintarafu kwenu, Kwa vyovyote viwavyo hali hii inatuhamasisha kukubali kukubaliana kuwa tumekuwa na tofauti za msingi katika kile kinachoweza kutunasibisha wote hapa kuwa tuna uelewa wa mambo na tena tunaelewa kwa ufikiri chanya watanzania wenzangu.
Naamin pia kuwa tunaifaham kwa hakika hata kama si kichanya kuwa tunayo safari tena iliyo ndefu katika usahihishaji,uboreshaji,uelimishaji,uteteaji na uundaji chanya wa jamii yetu kuanzia ngazi ya chini hadi kileleni, na pia nakosa shaka ya kuwa eti hatutambui ila naamini tunatambua kuwa katika safari hii kuna changamoto kadhaa zinazoikabili jamii yetu kwa sasa.
Ukweli ni kuwa MAPENZI NI SHINIKIZO LA UPOFU WA MOYO KWA AKILI YA MWANADAMU na TAFAKURI KATIKA AKILI YA MWANADAMU NI UFUNGUO WA MUONGOZO WA FIKRA KATIKA USTAWI WA KILA JAMBO LA MWANADAMU
Hivyo basi ni vema kwa Wafikiriaji wawe watulivu tena wawe watu wa mijadala mipevu inayotegemea uwezo wa tafakuri katika akili kwa kina na si mianguko ya upofu wa mioyo, hapa akili zinapaswa kuchimba, kuibua, kufukua, kufufua, kuchakatua {ku~process} na kupanga mikakati thabiti ya utatuzi wa matatizo tatizi katika kinachotatiza watatizwaji iwe tumo miongoni mwao au si katika wao.
Ndugu zangu ukweli utabaki kuwa ukweli kwa muda wote wa maisha ya dunia hii, ukweli wafikiriaji na wajadiliaji mijadala mingi wana tatizo la kuacha kujadili kwa fikra zao na matokeo yake hutumia sehemu ya bongo zao za nyuma kutema kumbukumbu ya nukuu za wenzao waliojituma kufikiri na wakanena kuendana na changamoto za maisha ya mwanadam. Si kosa na sisemi kamwe kuwa ni kosa kunukuu semi za wasemao vema duniani, ila nasema ni vema nasi tunene maneno ya hekima {kama tumejaaliwa hekima na kama hatunayo pole yetu} yatakayonukuliwa na vizazi vingine.
Tujipe fursa ya kuishi katika ukweli kwa kuwa duniani tunapita,isije ukaja wakati binadamu wajao wakadhani ulipata kutokea muda hapa duniani waliishi wanatheolojia, ambao hawakufikiri na kunena maneno yao ila walikuwa wananukuu BETI, STANZA na AYA katika BIBLIA, MISALE YA BWANA, NYIMBO, KHADITHI ZA MTUME na QUR'AN, pia hapa sisemi kufanya hivyo ni kosa, bali nasema itakuwa tumeviongopea vijukuu vyetu, kwani wangapi ni makasisi, wachungaji, maaskofu na masheikh miongoni mwetu? Hao mbona ni idadi ndogo katika sisi? Tena akheri tungekuwa wafuasi makini wa dini zetu katika matendo, lakini wala maneno tunayoyanukuu hatuyaishi kabisa, sisi tutakanwa mkano wa tofauti ya ule alokanwa mkweli yule YESU wa Mariamu. Yeye ilikuwa mara tatu tena alfajir, pengine kwa kuwa alikuwa mkweli na aliyaishi aliyoyanena huku akinukuu mkweli mwenzake ISAYA, lakini sisi twaweza kukanwa mara mia kenda na kenda tena wakati wa adhuhuri jua linapongeuka kati. Hakika OLE WETU WASOMI WAPOFU!
Hakika tatizo la wengi ni kutohitaji kujifunza ujenzi wa hoja zenye nguvu au uteteaji wa hoja zao dhaifu lakini zenye ukweli lukuki ,...tatizo hili limekuwa ni kubwa sana kwa wachangiaji au wajadiliaji mijadala katika hashuo hili au matando-pepe karibu yote kuanzia Facebook TZ, JAMII FORUM, Jukwaa huru nk.
Nimenena haya leo, sikunena jana, haingalipo jana sasa ndio sababu nikanena leo kwa ajili ya kesho, nimethubutu kunena, nimethubutu kujitanabaisha. Hakika nimesema kwa kuwa nimeona niseme ambacho hakijasemwa hapa katika msemo huu. "if something positive has not yet done, we have to be the first to do or act" Kumradhi kwa kutumia lugha ya wageni kwa kuwa ndio jadi ya hao wasiofikiri kufikirisha akili zao, miongoni mwetu, wasije wakadhani siwajali.
Nimenena wanaofikiri na kupenda kufikiri watafikiri na kuungana nami kufikiri zaidi na kufanya jitihada katika ujenzi wa jamii bora.
Sina neno jema ila tuuache UKASUKU kwa kuwa tofauti ya kasuku na sisi ni kufikiri na kuamua kwa utashi. Ahsanteni sana karibuni katika tafakuri chanya mkiwa na kumbukumbu kuwa HATA SAA INAYOONGOPEA WAKATI, UPO MUDA HUTAJA WAKATI SAHIHI!
Naomba msamaha iwapo nitakuwa mkosefu katika ufikishaji wa fikra zangu hapa, nimekuwa kimya kwa muda nikisoma mengi hapa na kufanya tafakuri kuangalia mashiko ya hoja katika mijadala mbalimbali lakini hatmae nimegundua katika ung'amuzi wangu kuwa kuna tatizo la kutoichanganua CHANYA.
Pengine nitakuwa sielewi vema uhali chanya ni upi?au ukoje?katika uhalisia wake, hivyo nitatarajia kuelimishwa na kufahamishwa kwa kina, lakini pengine nanyi mnaelewa vema UCHANYA au mnaelewa vema ndivyo sivyo uchanya ulivyo, hapo hati hii itakuwa somo mintarafu kwenu, Kwa vyovyote viwavyo hali hii inatuhamasisha kukubali kukubaliana kuwa tumekuwa na tofauti za msingi katika kile kinachoweza kutunasibisha wote hapa kuwa tuna uelewa wa mambo na tena tunaelewa kwa ufikiri chanya watanzania wenzangu.
Naamin pia kuwa tunaifaham kwa hakika hata kama si kichanya kuwa tunayo safari tena iliyo ndefu katika usahihishaji,uboreshaji,uelimishaji,uteteaji na uundaji chanya wa jamii yetu kuanzia ngazi ya chini hadi kileleni, na pia nakosa shaka ya kuwa eti hatutambui ila naamini tunatambua kuwa katika safari hii kuna changamoto kadhaa zinazoikabili jamii yetu kwa sasa.
Ukweli ni kuwa MAPENZI NI SHINIKIZO LA UPOFU WA MOYO KWA AKILI YA MWANADAMU na TAFAKURI KATIKA AKILI YA MWANADAMU NI UFUNGUO WA MUONGOZO WA FIKRA KATIKA USTAWI WA KILA JAMBO LA MWANADAMU
Hivyo basi ni vema kwa Wafikiriaji wawe watulivu tena wawe watu wa mijadala mipevu inayotegemea uwezo wa tafakuri katika akili kwa kina na si mianguko ya upofu wa mioyo, hapa akili zinapaswa kuchimba, kuibua, kufukua, kufufua, kuchakatua {ku~process} na kupanga mikakati thabiti ya utatuzi wa matatizo tatizi katika kinachotatiza watatizwaji iwe tumo miongoni mwao au si katika wao.
Ndugu zangu ukweli utabaki kuwa ukweli kwa muda wote wa maisha ya dunia hii, ukweli wafikiriaji na wajadiliaji mijadala mingi wana tatizo la kuacha kujadili kwa fikra zao na matokeo yake hutumia sehemu ya bongo zao za nyuma kutema kumbukumbu ya nukuu za wenzao waliojituma kufikiri na wakanena kuendana na changamoto za maisha ya mwanadam. Si kosa na sisemi kamwe kuwa ni kosa kunukuu semi za wasemao vema duniani, ila nasema ni vema nasi tunene maneno ya hekima {kama tumejaaliwa hekima na kama hatunayo pole yetu} yatakayonukuliwa na vizazi vingine.
Tujipe fursa ya kuishi katika ukweli kwa kuwa duniani tunapita,isije ukaja wakati binadamu wajao wakadhani ulipata kutokea muda hapa duniani waliishi wanatheolojia, ambao hawakufikiri na kunena maneno yao ila walikuwa wananukuu BETI, STANZA na AYA katika BIBLIA, MISALE YA BWANA, NYIMBO, KHADITHI ZA MTUME na QUR'AN, pia hapa sisemi kufanya hivyo ni kosa, bali nasema itakuwa tumeviongopea vijukuu vyetu, kwani wangapi ni makasisi, wachungaji, maaskofu na masheikh miongoni mwetu? Hao mbona ni idadi ndogo katika sisi? Tena akheri tungekuwa wafuasi makini wa dini zetu katika matendo, lakini wala maneno tunayoyanukuu hatuyaishi kabisa, sisi tutakanwa mkano wa tofauti ya ule alokanwa mkweli yule YESU wa Mariamu. Yeye ilikuwa mara tatu tena alfajir, pengine kwa kuwa alikuwa mkweli na aliyaishi aliyoyanena huku akinukuu mkweli mwenzake ISAYA, lakini sisi twaweza kukanwa mara mia kenda na kenda tena wakati wa adhuhuri jua linapongeuka kati. Hakika OLE WETU WASOMI WAPOFU!
Hakika tatizo la wengi ni kutohitaji kujifunza ujenzi wa hoja zenye nguvu au uteteaji wa hoja zao dhaifu lakini zenye ukweli lukuki ,...tatizo hili limekuwa ni kubwa sana kwa wachangiaji au wajadiliaji mijadala katika hashuo hili au matando-pepe karibu yote kuanzia Facebook TZ, JAMII FORUM, Jukwaa huru nk.
Nimenena haya leo, sikunena jana, haingalipo jana sasa ndio sababu nikanena leo kwa ajili ya kesho, nimethubutu kunena, nimethubutu kujitanabaisha. Hakika nimesema kwa kuwa nimeona niseme ambacho hakijasemwa hapa katika msemo huu. "if something positive has not yet done, we have to be the first to do or act" Kumradhi kwa kutumia lugha ya wageni kwa kuwa ndio jadi ya hao wasiofikiri kufikirisha akili zao, miongoni mwetu, wasije wakadhani siwajali.
Nimenena wanaofikiri na kupenda kufikiri watafikiri na kuungana nami kufikiri zaidi na kufanya jitihada katika ujenzi wa jamii bora.
Sina neno jema ila tuuache UKASUKU kwa kuwa tofauti ya kasuku na sisi ni kufikiri na kuamua kwa utashi. Ahsanteni sana karibuni katika tafakuri chanya mkiwa na kumbukumbu kuwa HATA SAA INAYOONGOPEA WAKATI, UPO MUDA HUTAJA WAKATI SAHIHI!