Mabibi na mabwana,
Mtanzania mwenzetu aliyeondoka akiwa "mfu", hatimaye amerejea leo salama salimini nyumbani Tanzania.
Jambo la heshima kubwa sana kwetu sisi sote ambao ni wana halisi wa nchi hii na wazalendo.
Tumeshinda!
Tumeshinda sote tuliofanikisha kurejea kwa mwana huyu wa nchi hii salama na kwa amani. Tafsiri halisi ya kuwa sote tu wajenzi wa nyumba moja. Yaani Tanzania.
Kesho inshallah kwa umoja wetu tena, kama Watanzania na tukamuage kwa pamoja Mzee wetu Rais mstaafu Mkapa (RIP) pale Uhuru, ambaye hakubahatika hata kumwona mwana huyu akirejea nyumbani.
Yaliyopita si ndwele, baada ya mazishi tujipange kuganga yajayo.
Kwako mheshimiwa rais wetu: kwa hakika haupo muda mzuri wa maridhiano na kuponya nchi hii kuliko huu.
Sentensi yako moja tu mkuu, itaifanya Tanzania yote akiwamo Mh. Lissu kuripuka kwa vifijo na vigeregere vya:
"Magufuli tosha!"
Kuyatambua madhila aliyoyapitia mja wake mola huyu, kumkaribisha nyumbani na neno moja la "pole" tu, litabeba uchawi wote unaohitajika.
Eeh mola wetu, hebu ukatujalie kuweza kuyaona yasiyoonekana na hasa kuudhihirisha ushindi wetu huu kwa wote wale wasioitakia mema nchi yetu.
Mungu ibariki Tanzania.
Mtanzania mwenzetu aliyeondoka akiwa "mfu", hatimaye amerejea leo salama salimini nyumbani Tanzania.
Jambo la heshima kubwa sana kwetu sisi sote ambao ni wana halisi wa nchi hii na wazalendo.
Tumeshinda!
Tumeshinda sote tuliofanikisha kurejea kwa mwana huyu wa nchi hii salama na kwa amani. Tafsiri halisi ya kuwa sote tu wajenzi wa nyumba moja. Yaani Tanzania.
Kesho inshallah kwa umoja wetu tena, kama Watanzania na tukamuage kwa pamoja Mzee wetu Rais mstaafu Mkapa (RIP) pale Uhuru, ambaye hakubahatika hata kumwona mwana huyu akirejea nyumbani.
Yaliyopita si ndwele, baada ya mazishi tujipange kuganga yajayo.
Kwako mheshimiwa rais wetu: kwa hakika haupo muda mzuri wa maridhiano na kuponya nchi hii kuliko huu.
Sentensi yako moja tu mkuu, itaifanya Tanzania yote akiwamo Mh. Lissu kuripuka kwa vifijo na vigeregere vya:
"Magufuli tosha!"
Kuyatambua madhila aliyoyapitia mja wake mola huyu, kumkaribisha nyumbani na neno moja la "pole" tu, litabeba uchawi wote unaohitajika.
Eeh mola wetu, hebu ukatujalie kuweza kuyaona yasiyoonekana na hasa kuudhihirisha ushindi wetu huu kwa wote wale wasioitakia mema nchi yetu.
Mungu ibariki Tanzania.