Mtuhumiwa asomewa mashtaka 21

The dots are not connecting....... mtatuzuga sana ila tutajua tuuu.
 
ustaadh AMBROSE tehe tehe.....aibu tupu,,,kila tukio utaskia waislamu hao hao,,huyu atakuwa ni mfuasi wa kile chama cha KIGAIDI ambacho kiongozi wake yupo jela

Ustaadh Ambrose Bin Calist kutoka falme za kiarabu (UAE)..kwani FBI bado hawajachora picha ya Ustaadh Ambrose Bin Calist akiwa kwenye bodaboda amevaa bagharashea na kanzu??
 

kaka naona unamtetea mhusika ambae uchunguzi wake umepita chini ya FBI
Au coz jina lake AMBROSE(mkiristo) anyway angekua muislamu ungetetea ww NYINYI MUNAUWANA WENYEWE NA BADO MTAUWANA Xana tu
 
hapa ndio uone huyo victor alivyotolewa kafara kwa kweli mungu amsaidie sana
 
kaka sheikh ilunga hawez kukamatwa,si umeona ata ponda anapeta na anaendelea kutoa matamko misikitini....waarabu wameachiwa kijana wa watu muendesha bodaboda kageuzwa mbuzi wa kafara...wakat uamsho, sheikh ilunga na kna ponda wanapeta haya mambo yana mwsho 2015 tusrudie makosa tuliyoyafanya watanzania
 
Mtuhumiwa asomewa mashtaka 21

Mtuhumiwa mmoja kati ya tisa waliotiwa mbaroni kuhusiana mlipuko wa bomu katika Kanisa la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Arusha na kusomewa mashtaka 21 yakiwamo ya mauaji na kujaribu kuua.

Mbele ya Hakimu Mkazi, Devotha Kamuzora, mtuhumiwa huyo, Victor Ambrose (20), dereva wa Bodaboda na mkazi wa eneo la Kwa Mromboo, Arusha alisomewa mashtaka hayo yakiwamo matatu ya mauaji ya watu watatu waliofariki katika tukio hilo lililotokea Mei 5, mwaka huu.

Wakisoma kwa kupokezana hati ya mashtaka, Mawakili wa Serikali, Zachariah Elisaria na Haruna Matagane walidai Calist pia anatuhumiwa kwa makosa 18 ya kujaribu kuua.

Mshtakiwa huyo alifikishwa mahakamani hapo kimyakimya akiwa chini ya ulinzi wa maofisa wa polisi na hakutakiwa kujibu lolote kwa sababu mashtaka yanayomkabili yanapaswa kusikilizwa na Mahakama Kuu.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Mei 27, mwaka huu itakapotajwa tena na mtuhumiwa amerudishwa mahabusu.
Saa moja kabla ya Ambroce kupandishwa kizimbani saa nne asubuhi, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas aliitisha mkutano na waandishi wa habari kitendo ambacho kiliwafanya baadhi yao kushindwa kufuatilia vyema tukio hilo.

Waarabu waachiwa huru

Polisi imewaachia huru raia wanne wa kigeni waliokuwa wakishikiliwa kuhusiana na tukio hilo baada ya uchunguzi uliofanywa na Polisi wa Tanzania, Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) na Polisi wa Kimataifa (Interpol) na kubaini hawakuhusika.

Kamanda Sabas aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake jana kuwa raia hao walikamatwa baada ya kutiliwa shaka walipoonekana wakitoka kwenye hoteli moja karibu na Kituo Kikuu cha Mabasi Arusha, muda mfupi baada ya tukio hilo.

Raia watatu wa Falme za Kiarabu(UAE), walioshikiliwa na kuachiwa wamegundulika kuwa ni watumishi wa Serikali.
Kamanda Sabas aliwataja kuwa ni Abdul Azziz Mubarak (30), (Mamlaka ya Mapato), Fouad Saleem Ahmed Al Hareez Al Mahri (29), (Zimamoto) na Daeed Abdulla Saad (28), ambaye ni Askari wa Usalama Barabarani.

Raia hao pamoja na mwenzao, Al-Mahri Saeed Mohseen (29) kutoka Saudi Arabia, walikabidhiwa kwa Idara ya Uhamiaji kuchunguzwa iwapo waliingia nchini kihalali.
 

Unawashauri watanzania au wakristo? Maana juu umeongea vingine mwisho umeomba kura za wote.
 
jamani hebu tueleweshane kidogo labda nimepitwa hivi huyu muendesha boda boda ndio alierusha bomu au yeye ndie alempakia mtu ambae alienda kurusha bomu maana inaonekana kuna watu awili walioshiriki hapa sasa yupi ni muhusika hapa
 
ustaadh AMBROSE tehe tehe.....aibu tupu,,,kila tukio utaskia waislamu hao hao,,huyu atakuwa ni mfuasi wa kile chama cha KIGAIDI ambacho kiongozi wake yupo jela

Sasa ina Maana waliomuua Padre Zanzibar pia ni wa CHAMA cha KIGAIDI??? ambapo kiongozi wake yupo???
 

Mbona waliyoyachoma Makanisa ZNZ hawajatafuta SCAPGOAT? wanajua ZNZ watawaka MOTO na kuwapasukia hiyo SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano hadi leo hakuna aliyeshikwa na serikali kimya - lakini wanaiita CHADEMA GAIDI

Wanakwenda kwa Muarusha hawakushika Wamasai wanajua nini kingetokea
 
Mkuu umetuambia mashitaka ni 21halafu umetaja mawili mengine ni yapi.

kuua watu watatu ni mashitaka matatu na kukusudia kuua pengine watu 18 ni mashitaka mengine 18 jumla 21
 
Inaonekana kama vile kunawatu munamjua anaehusika na wala si huyu kijana na pia munaushahidi wa hili, nawaomba mukawasaidie polisi kwa upelelezi tunapenda kuona haki ikitendeka. Hapa kila mtu anaisema Serikali na kuilaumu mbona hamuzungumzii FBI na INTAPOL wakati wote wanashirikiana? Je na hao wanasifa kama mnazoipa serikali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…