Mtu ana mtaji lakini anakosea location ya biashara mwisho inakufa Kwa kukosa wateja

Mtu ana mtaji lakini anakosea location ya biashara mwisho inakufa Kwa kukosa wateja

OgaBoy

JF-Expert Member
Joined
Aug 22, 2022
Posts
3,173
Reaction score
4,488
Kwanini unakosea, kufanya maamuzi ya location ya biashara wakati una mtaji.


1. Hutaki Kutofanya utafiti wa soko​

Watu wengi wanafungua biashara mahali fulani kwa kutegemea mawazo kichwani bila kuangalia watu wa eneo husika wanahitaji bidhaa hiyo, wana uwezo wa kununua na ushindani WA hapo au eneo hilo ni center ya biashara mfano WATU wakija eneo hilo Kwa ajili ya huduma au kununua wanaweza kuona bidhaa/huduma YAKO.

2. Tabia ya kufata bei nafuu ya pango​

Wengine huchagua sehemu kwa sababu pango ni rahisi.
Lakini mara nyingi sehemu yenye pango rahisi huwa mbali na watu wengi, pili haina mzunguko mkubwa wa wateja. Usisahahu Biashara inahitaji wateja wengi zaidi kuliko pango rahisi.

3. Kufata mkumbo​

Mtu anaona biashara fulani imefanikiwa sehemu fulani, naye anaenda kuiga bila kuchunguza sababu za mafanikio. Hayo.

4. Kushindwa kuelewa mazingira​

Kila eneo lina tabia yake.
Mfano, Eneo la wanafunzi linafaa kwa chakula cha bei nafuu na mahitaji madogo madogo ya msimu, Eneo la watu wenye kipato kikubwa linafaa kwa bidhaa au huduma zenye ubora. Ukikosea kuelewa tabia ya eneo, biashara inakuwa ngumu.

5. Maamuzi ya haraka​

Wengine wana mtaji na wanataka kuanza fasta fasta bila kufanya uchunguzi wa muda.
Biashara nzuri mara nyingi huanza kwa kuangalia eneo, watu, na mahitaji yao kwa muda flani.


Nimeandika uzi BAADA ya kuona MTU kaanzisha biashara Eneo lile nililotoka biashara Ile Ile iliyofeli pale na muda wote anashika tama.

Eneo liko vile vile
 
Kwanini unakosea, kufanya maamuzi ya location ya biashara wakati una mtaji.


1. Hutaki Kutofanya utafiti wa soko​

Watu wengi wanafungua biashara mahali fulani kwa kutegemea mawazo kichwani bila kuangalia watu wa eneo husika wanahitaji bidhaa hiyo, wana uwezo wa kununua na ushindani WA hapo au eneo hilo ni center ya biashara mfano WATU wakija eneo hilo Kwa ajili ya huduma au kununua wanaweza kuona bidhaa/huduma YAKO.

2. Tabia ya kufata bei nafuu ya pango​

Wengine huchagua sehemu kwa sababu pango ni rahisi.
Lakini mara nyingi sehemu yenye pango rahisi huwa mbali na watu wengi, pili haina mzunguko mkubwa wa wateja. Usisahahu Biashara inahitaji wateja wengi zaidi kuliko pango rahisi.

3. Kufata mkumbo​

Mtu anaona biashara fulani imefanikiwa sehemu fulani, naye anaenda kuiga bila kuchunguza sababu za mafanikio. Hayo.

4. Kushindwa kuelewa mazingira​

Kila eneo lina tabia yake.
Mfano, Eneo la wanafunzi linafaa kwa chakula cha bei nafuu na mahitaji madogo madogo ya msimu, Eneo la watu wenye kipato kikubwa linafaa kwa bidhaa au huduma zenye ubora. Ukikosea kuelewa tabia ya eneo, biashara inakuwa ngumu.

5. Maamuzi ya haraka​

Wengine wana mtaji na wanataka kuanza fasta fasta bila kufanya uchunguzi wa muda.
Biashara nzuri mara nyingi huanza kwa kuangalia eneo, watu, na mahitaji yao kwa muda flani.


Nimeandika uzi BAADA ya kuona MTU kaanzisha biashara Eneo lile nililotoka biashara Ile Ile iliyofeli pale na muda wote anashika tama.

Eneo liko vile vile
Ahsante kwa andiko fikirishi! Nimetembelea kituo cha biashara pale ilipokuwa stand ya mkoa pale Ubungo Dar karibu na TBC. Yaani hili andiko lako limesadifu uwekezaji uliofanyika pale. Bora pangejengwa hospitali watu wakatibiwa. I stand to be corrected.
 
Kwanini unakosea, kufanya maamuzi ya location ya biashara wakati una mtaji.


1. Hutaki Kutofanya utafiti wa soko​

Watu wengi wanafungua biashara mahali fulani kwa kutegemea mawazo kichwani bila kuangalia watu wa eneo husika wanahitaji bidhaa hiyo, wana uwezo wa kununua na ushindani WA hapo au eneo hilo ni center ya biashara mfano WATU wakija eneo hilo Kwa ajili ya huduma au kununua wanaweza kuona bidhaa/huduma YAKO.

2. Tabia ya kufata bei nafuu ya pango​

Wengine huchagua sehemu kwa sababu pango ni rahisi.
Lakini mara nyingi sehemu yenye pango rahisi huwa mbali na watu wengi, pili haina mzunguko mkubwa wa wateja. Usisahahu Biashara inahitaji wateja wengi zaidi kuliko pango rahisi.

3. Kufata mkumbo​

Mtu anaona biashara fulani imefanikiwa sehemu fulani, naye anaenda kuiga bila kuchunguza sababu za mafanikio. Hayo.

4. Kushindwa kuelewa mazingira​

Kila eneo lina tabia yake.
Mfano, Eneo la wanafunzi linafaa kwa chakula cha bei nafuu na mahitaji madogo madogo ya msimu, Eneo la watu wenye kipato kikubwa linafaa kwa bidhaa au huduma zenye ubora. Ukikosea kuelewa tabia ya eneo, biashara inakuwa ngumu.

5. Maamuzi ya haraka​

Wengine wana mtaji na wanataka kuanza fasta fasta bila kufanya uchunguzi wa muda.
Biashara nzuri mara nyingi huanza kwa kuangalia eneo, watu, na mahitaji yao kwa muda flani.


Nimeandika uzi BAADA ya kuona MTU kaanzisha biashara Eneo lile nililotoka biashara Ile Ile iliyofeli pale na muda wote anashika tama.

Eneo liko vile vile
Kuna bidada hapa kaunguza US $ 350,000 kafungua gym sehemu haina wateja (northeast USA), miezi michache hata mwaka haujafika kafunga biashara.

Kachukua sehemu kubwa sana kuliko uwezo wa biashara yake ku support. Alikuwa analipa rent tu $30,000 kwa mwezi, hapo bado nishahara ya wafanyakazi wake na vifaa vya gym alivyonunua.

Alivyoanzisha aliniomba niungane naye tuchanganye mtaji, nikaona hii biashara sijaelewa itaingiza pesa vipi sehemu haina wateja. Yeye akawa anataka kuanzisha kibishi.

Nikaona hii biashara ni passion zaidi ya profit.

Na kweli, ikawa hivyo hivyo.
 
Nini maana ya mtaji mdogo?

Nijibu hapa kwanza twende mbele
Kuna aina ya biashara unatamani kufungua maeneo yaliyo na wateja wengi lakini kutokana na kiasi ulichonacho unaamua kutafuta sehemu ya kawaida yenye pangonla bei mdogo na bidhaa zako mbili tatu,

Umeelewa?
 
Huu ndo ugonjwa wa biashara nyingi.

Kuna mtu alijenga vyumba vingi takribani 400 maajabu wafanya biashara mwanzoni walivikimbilia..kilichofuta wateja wakakosekana. Wakaamua kufunga leo hii vyumba vipi havina wateja..

Biashara ya kuiga na bila kufanya utafiti
 
Kama mtu ana mtaji mdogo afanye nini ili asikumbane na haya?
Kuna aina ya biashara unatamani kufungua maeneo yaliyo na wateja wengi lakini kutokana na kiasi ulichonacho unaamua kutafuta sehemu ya kawaida yenye pangonla bei mdogo na bidhaa zako mbili tatu,

Umeelewa?
Kama mtaji ni mdogo kulingana na maelezo ya hapo juu, maana yake ni kwamba biashara unayotaka kufanya inahitaji uwekezaji zaidi YAANI location ambayo kwa wakati huo huwezi kui-afford.

Hapo kuna factor kadhaa zinaonyesha upungufu wa mtaji kulingana na mahitaji ya hiyo biashara.

Sasa badala ya kulazimisha kufanya ile biashara unayoipenda kwenye location mbovu au ya kawaida isiyo na wateja, unaweza kubadili idea kwa muda.

Unaweza kufanya biashara nyingine yenye cashflow nzuri kulingana na mtaji uliopo, ambao unaweza kukuwezesha kupata location nzuri. Hii biashara utaitumia kama daraja la kuongeza mtaji, ili baadaye uweze kufungua ile biashara uliyoipenda sehemu sahihi.

Kwa sababu utakapoifungua ile biashara unayoipenda, itakuwa katika location nzuri yenye wateja wa kutosha, na inaweza kukupa matunda makubwa zaidi kuliko kuifungua Kwa pupa kwenye eneo lisilo na uhitaji mkubwa wa bidhaa au huduma hiyo.
Kinyume chake, ukilazimisha kuanza nayo katika location mbovu, inaweza kukuletea maumivu makali ya kifedha na ukuaji wa Kobe kobe.

Ndiyo maana mara nyingi utaona watu wengi waliofanikiwa wanawekeza kwanza kwenye biashara zenye cashflow nzuri kulingana na mtaji waliokuwa nao, hivyo inakuwa rahisi kupata location nzuri na wateja wengi.


Mfano

Tuseme unapenda sana biashara ya nguo za gharama kubwa.
Labda unataka kuuza nguo ambazo zinavaliwa na watu maarufu, wasanii, au watu wenye kipato kikubwa.
Aina hii ya biashara mara nyingi inahitaji location ya kifahari
Yenye maduka mazuri YAANI
sehemu zinazotembelewa na watu wenye pesa
Lakini kama mtaji wako ni mdogo, huwezi kumudu pango la sehemu hizo. Ukilazimisha kufungua duka hilo kwenye eneo la kawaida lisilo na wateja wa aina hiyo, biashara inaweza isiende vizuri.

Anza biashara nyingine yenye cashflow nzuri, mfano:
nguo za kawaida zinazouzwa kwa wingi
viatu vya bei nafuu
au bidhaa nyingine zinazouza haraka
Biashara hiyo itakusaidia kukusanya mtaji na uzoefu.
Baada ya muda utaweza kufungua ile biashara ya nguo za gharama kubwa katika location sahihi, ambapo wateja wake wapo.


Usifanye Biashara Kwa passion kama UNATAKA PESA bishara haitaki hisia sana Bali uhalisia.
 
Kuna bidada hapa kaunguza US $ 350,000 kafungua gym sehemu haina wateja (northeast USA), miezi michache hata mwaka haujafika kafunga biashara.

Kachujua sehemu kubwa sana kuliko uwezo wa biashara yake ku support. Alikuwa analipa rent tu $30,000 kwa mwezi, hapo bado nishahara ya wafanyakazi wake na vifaa vya gym alivyonunua.

Alivyoanzisha aliniomba niungane naye tuchanganye mtaji, nikaona hii biashara sijaelewa itaingiza pesa vipi sehemu haina wateja. Yeye akawa anataka kuanzisha kibishi.

Nikaona hii biashara ni passion zaidi ya profit.

Na kweli, ikawa hivyo hivyo.
Ni hatari sana mkuu WENGINE hufanya biashara Kwa hisia na passion, kimsingi wawekezaji WANATAKA kuona matunda si longolongo
 
Ni hatari sana mkuu WENGINE hufanya biashara Kwa hisia na passion, kimsingi wawekezaji WANATAKA kuona matunda si longolongo
Biashara inataka passion, lakini passion ikae backseat data za viability na Cost Benefit Analysis ziongoze kuendesha biashara.

Huyo dada alikuwa anaendeshwa na passion kuliko data.

Unafungua biashara kwa gharama kubwa kwa matumaini tu kwamba ukijenga watakuja.

Mara nyingine unaweza kujenga sehemu ambayo hawapo, ukatumia pesa nyingi na wasije.
 
Biashara inataka passion, lakini passion ikae backseat data za viability na Cost Benefit Analysis ziongoze kuendesha biashara.

Huyo dada alikuwa anaendeshwa na passion kuliko data.

Unafungua biashara kwa gharama kubwa kwa matumaini tu kwamba ukijenga watakuja.

Mara nyingine unaweza kujenga sehemu ambayo hawapo, ukatumia pesa nyingi na wasije.
Ni kweli mkuu
 
Kuna bidada hapa kaunguza US $ 350,000 kafungua gym sehemu haina wateja (northeast USA), miezi michache hata mwaka haujafika kafunga biashara.

Kachukua sehemu kubwa sana kuliko uwezo wa biashara yake ku support. Alikuwa analipa rent tu $30,000 kwa mwezi, hapo bado nishahara ya wafanyakazi wake na vifaa vya gym alivyonunua.

Alivyoanzisha aliniomba niungane naye tuchanganye mtaji, nikaona hii biashara sijaelewa itaingiza pesa vipi sehemu haina wateja. Yeye akawa anataka kuanzisha kibishi.

Nikaona hii biashara ni passion zaidi ya profit.

Na kweli, ikawa hivyo hivyo.
hii kitu inawakuta vijana wengi hata apa chini lakni unashanga anakuja mlugaluga moja(wengi kutoka upinzani) ambae hata biashasha hajui ana tupa lawama kwa mlaka ya TRA
 
Back
Top Bottom