Mtoto wa miezi minne aibiwa, mama yake adanganywa kwa kupewa 10,000

Donatila

JF-Expert Member
Oct 23, 2014
7,557
21,513
Mtoto mmoja mwenye umri wa miezi minne ameibiwa katika mtaa wa ustawi wa jamii kata ya Nyamanoro wilayani Ilemela Jijini Mwanza.

Imeelezwa kuwa watu waliomuiba mtoto huyo wamemchukua mama mzazi wa motto huyo kwa lengo la kwenda kufanya kazi za ndani lakini baada ya kufika Nyamanoro walimpa shilingi elfu kumi kwenda kununua mkate na baada ya kurudi amekuta tayari wameshaondoka na mtoto wake.

Wakizungumzia kuhusu tukio hilo baadhi ya wananchi wamesema kuwa ni jambo hilo limewashangaza kwani wameshindwa kuelewa lengo la watu hao kumuiba mtoto huyo ni nini na kuwaomba wazazi kuwa makini na watoto wao.

Akizungumzia tukio hilo kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Mwanza Ahmed Msangi amesema kuwa watu waliofanya tukio hilo mama mzazi wa mtoto anawafahamu hivyo Jeshi la Polisi linaendelea na msako wa kuwatafuta watu hao.

Hata hivyo Kamanda Msangi amesema jeshi la polisi koani humo linaendelea kuwasaka watu waliohusika na kumuiba motto huyo na kwamba watakapobainika watafikishwa katika vyombo vya dola.

Chanzo:
Mo Dewji Blog
 
Dar reporter nawe eti adanganywa na elfu kumi..apo watu anawajua wakamuagiza mkate ata kama wewe ungeacha kwenda KWA sababu ganii
 
ni huzuni kama mzazi kutokewa na tukio kama hili la kuibiwa mtoto,hili ndilo suala ambalo my home affairs minister angekuwa anayachukulia uzito unaositahili,human trafficking its very very seriously issue hasa ukanda huu wa SADC,wenzetu wameshaamka na sio rahisi kusafiri na mtoto bila ya kuwa na documents za mtoto,nchi yetu kila kitu tunakichukulia kisiasa ila kinapokukuta then unaona umuhimu wake,please my minister ni lazima nchi iwe na IDs kwa watanzania,na systems iwe inaongea nchi Zima ,tukio kama hili limetokea ID ya mtoto huyu ingekuwa flagged nchi nzima,border posts zetu zote zinge kuwa alert.nchi imekuwa kama public toilet mtu unaingia na kutoka utakavyo,this is not right,mtoto akizaliwa anasajiliwa pale hospitalini na anapewa cheti cha kuzaliwa palepale,na cheti hicho kimo ndani ya central systems ya nchi na informations zote kama majina ya wazazi wake na IDs number zao,address yao etc etc hatujachelewa bado.
 
Hizi dili za wizi wa watoto vichanga mnazipanga sana nyie wakina mama, na hii ni baada ya kuula usichana na sasa ukamdanganya mwenzi wako una ujauzito ilihali umefunga matambala miezi tisa ukitegemea hiyo miezi ikiisha ukaibe Mtoto.


Wakati matambara yanafungwa miezi 9 Mwenye mimba anakua wapi asiweze kuyaona?
 
ni huzuni kama mzazi kutokewa na tukio kama hili la kuibiwa mtoto,hili ndilo suala ambalo my home affairs minister angekuwa anayachukulia uzito unaositahili,human trafficking its very very seriously issue hasa ukanda huu wa SADC,wenzetu wameshaamka na sio rahisi kusafiri na mtoto bila ya kuwa na documents za mtoto,nchi yetu kila kitu tunakichukulia kisiasa ila kinapokukuta then unaona umuhimu wake,please my minister ni lazima nchi iwe na IDs kwa watanzania,na systems iwe inaongea nchi Zima ,tukio kama hili limetokea ID ya mtoto huyu ingekuwa flagged nchi nzima,border posts zetu zote zinge kuwa alert.nchi imekuwa kama public toilet mtu unaingia na kutoka utakavyo,this is not right,mtoto akizaliwa anasajiliwa pale hospitalini na anapewa cheti cha kuzaliwa palepale,na cheti hicho kimo ndani ya central systems ya nchi na informations zote kama majina ya wazazi wake na IDs number zao,address yao etc etc hatujachelewa bado.
Wazo zuri sana, lipange vizuri ili liweze someka vema na kueleweka kwa wengi.
 
Huyo mtuto ameibiwa nini? Mbona hujakitaja hicho kitu kilichoibwa toka kwa huyo mtoto? Au una maanisha huyo mtoto yeye ndio ameibwa?
 
Back
Top Bottom