Mtoto nje ya ndoa aleta changamoto

Mtoto nje ya ndoa aleta changamoto

KALYANKOZILE

Member
Joined
Apr 24, 2013
Posts
19
Reaction score
1
Baada ya baba kuwa na familia alijaliwa watoto wa kike wawili na wa wakiume mmoja wakati huo huo baba huyu alijipenyeza na kwenda nyumba ndogo ambapo alijipatia pia mtoto wa kiume na baada ya kufikisha umri wa miaka 14 baba yake ameamua kuweka mambo wazi kwa mke wake na mke wake kumuelewa na hivyo kijana huyo kuanza maisha mapya kwenye familia yao lakini Kijana huyu amekuwa mtata pale anashindwa kuwaelewa ndugu aliowakuta kwenye familia hiyo hasa wa kike na kuanza kuwauliza maswali; nyie mnasema mimi ni ndugu yenu mbona mna mama yenu na mimi nina mama wa kwangu? na baba huyu ni baba yenu wa kwangu mama aliniambia alifariki nikiwa mdogo je inakuwaje awe huyu au amefufuka!!!matokeo yake ameanzisha mahusiano ya kimapenzi na watoto wote wa kike na kubahatika kumpatia mimba msichana mmoja na penzi lao kujifunua kwa wanafamilia wote kwani wameshindwa kuficha mahusiano yao.Swali je na wa kurahumiwa ni nani? na nini kifanyike kwani hadi sasa mto umeanza kuwaka kwenye familia hiyo.
 
baba awakalishe chini nakuwaambia ukweli na mama wa huyo kijana akiri mbele yake kuwa huyo ni bb yake aache upuuzi wake 14yrs hajui kinachoendelea mpuuzi kabisa anauliza uliza maswali yakijinga ashukuu mungu angeshatupwa huko kwenye mapipa!!
 
Kwani alivopelekwa kwa hiyo familia mpya hakuambiwa anaenda kwa nani? kama familia nzima inamfahamu iweje huyu kijana anakifanya mbumbumbu? Na mahusiano gani ameanzisha na dada Zake akiwa na miaka 14? wakae kifamilia waongee. haiwezekani mtoto wa miaka 14, mgeni kwenye familia , aje kuleta vurugu nyumbani. Baba asimame mbele ya familia, aeleze kila kitu, mambo yaendelee. Ikishindikana arudishwe kwa mama yake aishi kwa amani, mradi baba anapeleka pesa za matumizi.
 
Arudishwe hukohuko alikozaliwa na kulelewa, hawezi kuja tibua maisha ya wenzake eti kuhoji na kutembea na Dada zake
Mi kwangu ni kutimua tu kwani kwake kupo na akamuulize Mama yake baba ni yupi wakati anadai nilishakufa!!!
 
Mmmh...nimeipenda hii,kwa mtiririko ulivyo ni kwamba watoto wa kike wa bi mkubwa ndo walitangulia kuliona jua so far bwana mkubwa alijipenyeza kwa bi mdogo baada ya kufunga kazi kwa bi mkubwa...point of view,ni kwa nini tusiwe na mtazamo huru kuwa hawa mabinti ndo walim-entertain huyu bwana mdogo? Thereinafter bwana mdogo alitoka kijiji gani hadi umri huu hajui 'aa' na 'bee'? Ingekua enzi zetu huyu ni wa kuitia wazee...
 
Dah!! Siku hizi story za kufirikika zimekuwa nyingi.
 
huyo si mtoto ni firauni tu, arudishwe kwa mama yake! then huduma zimfuate hukohuko
 
Hebu tueleze kinagaubaga, kijana wa miaka 14 kampa mimba binti wa miaka mingapi? maana kwa haraka kutokana na mtiririko wa tamthiliya yako inaonesha hao mabinti ni wakubwa kumzidi huyo kijana...
 
Mambo ya kutunga, maana mtoto wa miaka 14 hajuhi kwanini yuko kwenye familia hii mpya? Zaidi ya hapo arudishwe alikotoka.
 
Back
Top Bottom