Mtoto kuzaliwa na meno

thereitis

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
297
41
Mtoto wangu amezaliwa akiwa na meno mawili ya chini. Je hali hii inasababishwa na nini? je nini kinasababisha mtoto kuzaliwa na meno?
 
Habari yako ndugu? Awali nikupe hongera kwa kupata mtoto, ni zawadi adhimu mno!
Kitaalam meno ya mtoto huanza kutengenezwa akiwa tumboni, yaani in intra uterine life, na moja katika hatua zake ni utengenezwaji wa vitu vinavyoonekana kana kwamba ni meno, yaani dental papillae! hizi hazitakiwi kuonekana kinywani, na papillae za meno ya utoto na ukubwa zote hutengenezwa mtoto akiwa tumboni.

Kwa sababu za kimaumbile, baadhi ya watoto dental papillae zao huonekana kinywani na kuonekana kana kwamba ni "meno ya plastiki", ukweli ni kuwa hizi ni dental papillae ambazo huja kutengeneza meno ya utu uzima, yaani permanent teeth ama ya utoto, yaani deciduous au milk teeth.

Baadhi ya makabila huyang'oa meno haya, tena kwa vifaa visivyo salama!Haya ni makosa MAKUBWA ambayo huweza kumsababisha mtoto kukosa meno yake ya sehemu husika ya utoto ama ukubwa ama yote! Pamija na hatari nyinginezo km vile kutoa damu kwa wingi, maambukizi, yaani infections nk!

Kwa kumalizia, meno hayo hayana tatzo kabisa kwa mtoto! Kwa ushauri zaidi mwone daktari wa meno aliye karibu nawe, preferably awe ni Dental surgeon ama assistant Dental officer.

Tunamtakia mtoto makuzi na malezi mema.
Ahsante
 
Habari yako ndugu? Awali nikupe hongera kwa kupata mtoto, ni zawadi adhimu mno!
Kitaalam meno ya mtoto huanza kutengenezwa akiwa tumboni, yaani in intra uterine life, na moja katika hatua zake ni utengenezwaji wa vitu vinavyoonekana kana kwamba ni meno, yaani dental papillae! hizi hazitakiwi kuonekana kinywani, na papillae za meno ya utoto na ukubwa zote hutengenezwa mtoto akiwa tumboni.
Kwa sababu za kimaumbile, baadhi ya watoto dental papillae zao huonekana kinywani na kuonekana kana kwamba ni "meno ya plastiki", ukweli ni kuwa hizi ni dental papillae ambazo huja kutengeneza meno ya utu uzima, yaani permanent teeth ama ya utoto, yaani deciduous au milk teeth.
Baadhi ya makabila huyang'oa meno haya, tena kwa vifaa visivyo salama!Haya ni makosa MAKUBWA ambayo huweza kumsababisha mtoto kukosa meno yake ya sehemu husika ya utoto ama ukubwa ama yote! Pamija na hatari nyinginezo km vile kutoa damu kwa wingi, maambukizi, yaani infections nk!
Kwa kumalizia, meno hayo hayana tatzo kabisa kwa mtoto! Kwa ushauri zaidi mwone daktari wa meno aliye karibu nawe, preferably awe ni Dental surgeon ama assistant Dental officer.
Tunamtakia mtoto makuzi na malezi mema.
AHSANTE
Asante kwa ushauri mzuri!!
 
hayo hayana shida nina kaka yangu alizaliwa na meno ya mbele na sahizi ni mtu mzima na maisha yake
 
Back
Top Bottom