ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 43,076
- 49,775
Binafsi Huwa najiuliza hivi kazi ya Wizara ya Ustawi wa Jamii na Makundi Maalumu anayoisimamia Dr.Dorothy Gwajima ni ipi ikiwa Makundi ya watu maalumu hayasaidiwi Kwa lolote la Maana?
-Wazee wanaonyanyasika mahospitali hawatibiwa
-Watoto Yatima Wanazidi kuongezeka mitaani hakuna hatua ya usaidizi.
-Ndoa zinazidi kuvunjika hakuna hata ushauri wa kisaikolojia na tiba kwenye jamii
-Walemavu hawapati usaidizi si Kuwajengea uwezo walakuwanunulia vifaa mwendo wanavyohitaji.
-Watu wenye Magonjwa Sugu Wanazidi kuteseka mitaani hakuna hatua za kuwasaidia.
Sasa naishauri Serikali Kupitia hiyo Wizara ya Ustawi wa jamii na Makundi Maalumu kwamba fanyeni Zoezi la kuwatambua watu wote wenye mgonjwa Sugu kwenye Jamii ambayo yameshindikana Kwa sababu mbalimbali ikiwemo vipago duni kulinganisha na complicity ya ugonjwa.
Idadi hao ikitambulika anzisheni kampeni ya Jamii kuwasaidia Ili zipatikane pesa Hawa ndugu zetu wapone.Igeni mfano wa Marathon Huwa zinafanywa na chama Cha madaktari wanawake au wale wanaokusanyaga pesa za kuwasaidia Watoto wenye shida za Moyo nk.
Shirikianeni na Wizara ya Afya Ili ku gauge Magonjwa makubwa ambayo yanahitaji pesa nyingi.Jamii kwa.pamoja na mataasisi tutaweza kuchangia na watu watapata tiba.
Watanzania ni waungwana sana ila nyie mlioko kwenye maofisi hamna akili za ubunifu hata kidogo.Walau vyombo vya habari Huwa vinajitahidi kuwasaidia kwa.wale ambao watajitokeza na kunijulisha jamii,Sasa nyie wa Serikali mnashindwa vipi kuandaa kampeni za hivyo?
Pole sana ndugu Kwa haya masahibu,nimeumia sana Kwa huu ugonjwa wa huyu mtoto👇👇👇
My Take
Kwa kuwa mada hii sio ya Kisiasa ya kutukana Serikali wengi watapita kimya kimya kana kwamba hawajaona.
=====
Mtoto Baltazari Mkina mkazi wa kijiji cha Mtoni kata ya Nakatunguru wilaya ya Ukerewe mkoa wa Mwanza amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan amsaidie ili aweze kupata huduma za matibabu.
Diwani wa kata ya Nakatunguru Mataba Stostenence amesema Baltazari alianza kuugua mwezi Desemba mwaka 2020, ambapo alipatwa na uvimbe (upele) katika taya la mkono wa kulia ya shavu, na walifika katika hospitali ya Bugando kwa ajili ya matibabu lakini wazazi wake walishindwa kuendelea kutokana na kukosa shilingi Milioni 3 za kugharamia huduma hizo.
Amesema wazazi wa mtoto huyo hawana uwezo na wanaendelea kumuhudumia kwa kutumia dawa za miti shamba.
View: https://www.instagram.com/p/C24aHRQtCuA/?igsh=MWNlcGJiOW9lNTQ3YQ==
-Wazee wanaonyanyasika mahospitali hawatibiwa
-Watoto Yatima Wanazidi kuongezeka mitaani hakuna hatua ya usaidizi.
-Ndoa zinazidi kuvunjika hakuna hata ushauri wa kisaikolojia na tiba kwenye jamii
-Walemavu hawapati usaidizi si Kuwajengea uwezo walakuwanunulia vifaa mwendo wanavyohitaji.
-Watu wenye Magonjwa Sugu Wanazidi kuteseka mitaani hakuna hatua za kuwasaidia.
Sasa naishauri Serikali Kupitia hiyo Wizara ya Ustawi wa jamii na Makundi Maalumu kwamba fanyeni Zoezi la kuwatambua watu wote wenye mgonjwa Sugu kwenye Jamii ambayo yameshindikana Kwa sababu mbalimbali ikiwemo vipago duni kulinganisha na complicity ya ugonjwa.
Idadi hao ikitambulika anzisheni kampeni ya Jamii kuwasaidia Ili zipatikane pesa Hawa ndugu zetu wapone.Igeni mfano wa Marathon Huwa zinafanywa na chama Cha madaktari wanawake au wale wanaokusanyaga pesa za kuwasaidia Watoto wenye shida za Moyo nk.
Shirikianeni na Wizara ya Afya Ili ku gauge Magonjwa makubwa ambayo yanahitaji pesa nyingi.Jamii kwa.pamoja na mataasisi tutaweza kuchangia na watu watapata tiba.
Watanzania ni waungwana sana ila nyie mlioko kwenye maofisi hamna akili za ubunifu hata kidogo.Walau vyombo vya habari Huwa vinajitahidi kuwasaidia kwa.wale ambao watajitokeza na kunijulisha jamii,Sasa nyie wa Serikali mnashindwa vipi kuandaa kampeni za hivyo?
Pole sana ndugu Kwa haya masahibu,nimeumia sana Kwa huu ugonjwa wa huyu mtoto👇👇👇
My Take
Kwa kuwa mada hii sio ya Kisiasa ya kutukana Serikali wengi watapita kimya kimya kana kwamba hawajaona.
=====
Mtoto Baltazari Mkina mkazi wa kijiji cha Mtoni kata ya Nakatunguru wilaya ya Ukerewe mkoa wa Mwanza amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan amsaidie ili aweze kupata huduma za matibabu.
Diwani wa kata ya Nakatunguru Mataba Stostenence amesema Baltazari alianza kuugua mwezi Desemba mwaka 2020, ambapo alipatwa na uvimbe (upele) katika taya la mkono wa kulia ya shavu, na walifika katika hospitali ya Bugando kwa ajili ya matibabu lakini wazazi wake walishindwa kuendelea kutokana na kukosa shilingi Milioni 3 za kugharamia huduma hizo.
Amesema wazazi wa mtoto huyo hawana uwezo na wanaendelea kumuhudumia kwa kutumia dawa za miti shamba.
View: https://www.instagram.com/p/C24aHRQtCuA/?igsh=MWNlcGJiOW9lNTQ3YQ==