Kuna jamaa ana demu wake, kila mmoja ana mtoto mmoja, na kila mmoja anaishi kwake na mtoto wake, (mtoto wa mwanamke anamuita jamaa uncle na mtoto wa mwanaume anamuita demu aunt). Kutokana na mazingira inabidi kila wanapotaka kukutana mwanaume aenda kwa mwanamke, sasa jamaa analalamika mwanamke ana mdekeza sana mtoto wake(kike), kila wanapokuwa wamekaa mama na uncle mtoto anatakaa kukaa katikati, na inafikia hadi kulala usiku mtoto anataka kulala katikati (mtoto ni wa umri wa miaka 7 anasikia na anaelewa vyote vinavyoongelewa) mama kwa kuwa hataki kumuudhi mtoto wake anamkubalia vyote anavyotaka, kilachomfanya mpaka akaleta kwenye jamvi hili ni siku moja alienda kulala ilipofika usiku mtoto akalilia kulala na mama yake na uncle atoke, uncle kwa kutotaka asimuudhi demu wake maana mtoto akilia na mama anakuwa hana raha then uncle ikabidi atoke ampishe mtoto na uncle akalala sehemu nyingine. Tutoe ushauri kuhusu haya mahusiano, ushauri uegemee sana kisaikolojia na kimahusiano.