Mtoto afungiwa ndani kwa miaka miwili Iringa

Mtoto afungiwa ndani kwa miaka miwili Iringa

Dotto Mnzava

R I P
Joined
Mar 6, 2014
Posts
864
Reaction score
427
Kuna mtu wangu wa karibu yuko Iringa ameniambia kuwa kuna Mtoto aliyepatikana asubuhi ya leo akiwa amefungiwa ndani ya nyumba (haijafahamika mara moja kuwa ndiko anako ishi au la!)kwa miaka miwili katika eneo la Kihesa Iringa.

Amesema mtoto huyo alifungwa kwa kutumia mnyororo na kufungwa kwenye kitanda cha chuma.......msichana wa kazi muhusika wa tukio.

Mtoa taarifa hajaweza kudodosa kuwa mtoto anamiaka mingapi na baadhi ya facts ambazo zinaweza kuwepo kwenye hii taarifa, ameweza kunitumia picha tu.

Mwenye taarifa zaidi juu ya hili tukio tunaomba atusaidie tafadhali.


attachment.php


Tukio hilo limetokea jana Iringa Mjini maeneo ya Kihesa,baada ya majirani kutoa taarifa kwenye serikali ya mtaa kuwa kuna babu anamfungia ndani na kumnyima chakula mtoto wake mwenye miaka kumi ambaye ni mlemavu wa akili.

Picha kama mnavyoiona hapo, dada wa kazi wa binti babu huyo sasa bado yupo kituo cha polisi hapa mjini kwa mahijiano zaidi.
 

Attachments

  • MtotoJF.jpg
    MtotoJF.jpg
    21.9 KB · Views: 15,482
Nadhani msichana wa kazi hana kosa hapo. Ifike mahala tuukubali ukweli na tuuseme.

Kama mimi ndio nashughulikia hii issue nitaanza kuwakamata wazazi wa mtoto huyu wajieleze kwa nini miaka miwili wao hawakuwa wanafuatilia maisha ya mtoto wao? walikuwa wapi miaka yote miwili mtoto kafungwa mnyororo wa chuma?

Wazazi wamekuwa wanakwepa malezi ya watoto na kuwatelekeza kisha wanakuja ibuka na kushusha lawama kwa msaidizi wa kazi za ndani. Nawaza tofauti. KILA MTU NA ABEBE MZIGO WAKE.
 
Hivi kama mtu kakukosea si umuache aende kwao? Ni ajabu watu wanatafuta watoto wakati wenye ano wanawatesa. Nitafurahi kama tutapata story kamili!
 
Afadhali imetokea Iringa ingekuwa Dar yangesemwa mengi sana ikiwemo " watu wa DAR wana roho mbaya sana ndio maana hatutaki watoto wetu wakafanye kazi huko"
 
Imani potofu... Iringa kuna ma imani ya fedha za kishetani shetani sana.
 
Kuna mtu wangu wa karibu yuko Iringa ameniambia kuwa kuna Mtoto aliyepatikana asubuhi ya leo akiwa amefungiwa ndani ya nyumba (haijafahamika mara moja kuwa ndiko anako ishi au la!)kwa miaka miwili katika eneo la Kihesa Iringa.

Amesema mtoto huyo alifungwa kwa kutumia mnyororo na kufungwa kwenye kitanda cha chuma.......msichana wa kazi muhusika wa tukio.

Mtoa taarifa hajaweza kudodosa kuwa mtoto anamiaka mingapi na baadhi ya facts ambazo zinaweza kuwepo kwenye hii taarifa, ameweza kunitumia picha tu.

Mwenye taarifa zaidi juu ya hili tukio tunaomba atusaidie tafadhali.


attachment.php


Huo Mkoa Unaabudu Mno Na Sana USHIRIKINA Hivyo Sishangai Kihiiiiiiiiiivyoooooooo! Kesha Waingizia Mno Pesa Huyo!
 
Back
Top Bottom