Mtoto afariki kutokana na kusukwa nywele

mourisous

JF-Expert Member
Jan 19, 2016
443
269
TAFADHALI SHARE UJUMBE HUU WA KUSIKITISHA ILI KINA MAMA WOTE WAUSOME NA KUBADILIKA.

Leo tarehe 27-04-2017 kuna dada amefiwa na mwanae wa miaka miwili aliyekuwa amelazwa hospitali kuanzia siku ya Ijumaa Kuu. Hapa Jijini Dar es Salaam.

Chanzo cha kifo cha mtoto huyu ni kutokana na mama yake kumsuka nywele mtindo wa DREAD ambapo nywele zinasukwa kwa kusokotwa sana.

Mtoto alisukwa siku ya kwanza lakini hakumalizwa. Siku ya pili Alhamisi akamaliziwa kusukwa. Siku ya Ijumaa ambayo ndo ilikuwa Ijumaa Kuu mtoto alianza kuumwa mwili mzima.

Walipoona anazidi kuumwa wao wakahisi nywele walivyombana itakuwa chanzo wakaanza kumnyoa haraka. Lakini wakiwa wanaendelea kumyoa hali ikazidi kuwa mbaya wakampeleka hospitali hivyohivyo bila kummalizia kumnyoa.

Walipofika hospitali daktari aliwagombeza sana kwa kumsuka mtoto kwa kumvuta kiasi hicho nywele zake. Alianza matibabu na walimalizia kumnyoa nywele.

Hali iliendelea kuwa mbaya akawekewa mashine ya kumsaidia kupumua. Bahati mbaya mchana wa leo mtoto kafariki.

Chanzo cha kifo kinasemekana misuli ya kichwa ilivutika kwa kiwango kikubwa ikapelekea matatizo mengine yaliyosababisha kifo.

FUNZO: Kina mama acheni kuwafanyia watoto wenu mambo ya watu wazima. Waacheni watayafanya wao kwa muda wao. Waacheni waishi maisha ya kitoto. Madai yenu ya kwenda na wakati ndo matokeo yake haya.

MUNGU ATUSAIDIE.
 
Habari ya uwongo na iko kwa ajili ya mazuzu.
Jina LA mama ni nani?
Jina LA mtoto ni nani?
Jna LA msusi na saluni
Jina LA hospital aliko pelekwa mtoto
Jina LA daktari aliyempokea mtoto
Jina LA daktari aliye thibitisha kifo
Chanzo cha taarifa yako.
Bujibuji kwa usalama wa wahusika mkuu
 
Habari ya uwongo na iko kwa ajili ya mazuzu.
Jina LA mama ni nani?
Jina LA mtoto ni nani?
Jna LA msusi na saluni
Jina LA hospital aliko pelekwa mtoto
Jina LA daktari aliyempokea mtoto
Jina LA daktari aliye thibitisha kifo
Chanzo cha taarifa yako.
Wewe jina lako halisi ni nani?
 
Hii tabia ya kukandika watoto mizigo kichwani hapana,mnakomaza watoto sura,khaaa kusuka hata me mtu mzima machozi hunitoka sembuse mtoto.
 
Habari ya uwongo na iko kwa ajili ya mazuzu.
Jina LA mama ni nani?
Jina LA mtoto ni nani?
Jna LA msusi na saluni
Jina LA hospital aliko pelekwa mtoto
Jina LA daktari aliyempokea mtoto
Jina LA daktari aliye thibitisha kifo
Chanzo cha taarifa yako.
Hata kama itakua ni habari ya uongo kama unavyoiita ila haya yanafanyika sana kwenye jamii zetu, mzazi hasa sisi kina mama unakuta tunawafanyia watoto mambo makubwa yasiyoendana na umri wake, unamkuta mama anampaka mwanae vipodozi vya kiutu uzima na mwisho wa siku ngozi ya mtoto inakomaa kama ya mwanamke wa makamo, tuacheni hii tabia tuwaache watoto waishi katika generation yao
 
Back
Top Bottom