Mtikisiko CCM Kahama, Kishimba atishia kujitoa!

Mtikisiko CCM Kahama, Kishimba atishia kujitoa!

magode

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2014
Posts
2,204
Reaction score
3,338
Wakuu hali ni tete jimbo la kahama mkoani Shinyanga. Mgombea wake ambae ni mfanyabiashara wa jijini Dar bw.Jumanne kishimba,ametishia kujitoa kuendelea na kampeni kutokana na ukweli kwamba hawezi kushinda!

Kishimba amelalamika kuwa ameachiwa kila kitu afanye mwenyewe na viongozi wa ccm wa wilaya na kata wanaambatana nae mchana,lkn usiku wapo kwa James Lembeli.

Tajiri huyo ambae pia ni mmiliki wa maduka makubwa ya imalaseko amegoma kabisa kuendelea kutapanya fedha zake wakati anajua hatashinda!

Wakati huo huo,mgombea ubunge wa jimbo hilo kupitia chadema James Lembeli amechafua hali ya hewa ktk majimbo jirani ya Ushetu na Msalala kwa kufanya kampeni na chopa ili kusaidia harakati za ukombozi ktk majimbo hayo yaliyo chini ya halimashauri ya mji wa kahama.
 
tatizo la kishimba,analack strategy,hana watu waliobobea kimkakati wa kupiga kampeni...japo pesa anazo angeweza kupata watu wazuri kumwongoza,lakini nahisi kaweka weka wapambe tu katika kampeni na si wazoefu wa kampeni..
 
tatizo la kishimba,analack strategy,hana watu waliobobea kimkakati wa kupiga kampeni...japo pesa anazo angeweza kupata watu wazuri kumwongoza,lakini nahisi kaweka weka wapambe tu katika kampeni na si wazoefu wa kampeni..
Unazikubali story za vijana wa BAVICHA?

Katika majimbo ya kanda ya ziwa ambayo CCM wana uhakika ni pamoja na Kahama. Mark my word.
 
Mkapa ndio anambembeleza asijitoe.... Ila yeye juzi alishaandika barua kwa Kinana

nasikia hata matajiri wa kahama hawamtaki kishimba,eti kisa ni boss wao,karibu wote wametajirikia kupitia mikononi mwake,sasa wanaona akishinda ubunge,atarudi kahama na atawabana,hawataki kukaa karibu na boss wao.
 
tatizo la kishimba,analack strategy,hana watu waliobobea kimkakati wa kupiga kampeni...japo pesa anazo angeweza kupata watu wazuri kumwongoza,lakini nahisi kaweka weka wapambe tu katika kampeni na si wazoefu wa kampeni..
Mkuu makosa alifanya ktk kuchagua jimbo. Jimbo la kahama kwa jinsi James lembeli alivyojiimarisha hata km wangechuana ndani ya ccm,kishimba asingeshinda. Kwa majimbo hayo ya kahama,angeenda jimbo la ushetu au jimbo la msalala. Kishimba hayo maeneo yote anajulikana na wagombea wake ni dhaifu..! Kwa jimbo la kahama anapoteza fedha tu.
 
Kishimba Kahama hawezi kushinda hata kama amelipa madeni ya akina Mama wanayodaiwa Finca na Baypot kahama na Pikipiki 48 alizotoa bado hawezi kushinda kwani lembeli ni strategist mzuri mno na ana kura nyingi za wanawake wa Kahama kwani alianzisha vikoba na kuvifadhili toka zamani na wao wanakueleza kua kura za Lembeli zitakua nyingi sana na hivi ameanza kampeni na chopa ili kuyafikia maeneo mengi zaidi ndio basi tena na atabadilisha upepo wa kanda ya Ziwa na ccm hawatoamini
 
WATANZANIA WAMEAMKA SASA:CCM PEKEE NDIO TEGEMEO


1.-Wamegundua CCM hakuna UDINI
-Ukawa ni UDINI dhehebu la EL na Maaskofu 2 ndio VINARA wao


2.-Wamegundua CCM hakuna UKANDA
-Ukawa sasa UBAGUZI wa KIKANDA unashamiri sana.


3.-Wamegundua CCM tunaongozwa na SERA SAHIHI
-Ukawa ni MAHABA yasiyoeleweka,watu wanalipwa kuhudhuria
mikutano.


4.-Wamegundua CCM inafanya siasa za ki-staaarabu.
-Ukawa makundi ya FUJO yamejitokeza sana,hakuna ustaarabu.


5.-Wamegundua GESI,Utawala BORA utainua UCHUMI wetu
-Ukawa kuna Matajiri 5, watagawana NCHI ili kurudisha pesa
zao.


KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

utaamka tu tar 25 kwa mara ya kwanza mtakapokuwa wapinzani
 
Ushetu CHADEMA walimsimika Bw. Isaya Bukakiye (Mzaliwa wa Kabingo - Kakonko) huyu yuko sawa kwa maneno jukwaani na fedha. Hope kama Lembeli ataendelea kumsaidia anaweza kushinda
 
Ushetu CHADEMA walimsimika Bw. Isaya Bukakiye (Mzaliwa wa Kabingo - Kakonko) huyu yuko sawa kwa maneno jukwaani na fedha. Hope kama Lembeli ataendelea kumsaidia anaweza kushinda

yule jamaa sijui kama atashinda maana wenyewe wanasema sio mzaliwa wa usukumani
 
Back
Top Bottom