Mtikila azuia Muswada wa Mahakama ya Kadhi Kujadiliwa

Standalone

JF-Expert Member
Nov 15, 2014
676
576
MCHUNGAJI Christopher Mtikila, leo amefungua kesi ya kikatiba namba 14 ya mwaka 2015 katika Mahakama Kuu ya Tanzania kupinga muswada wa mabadiliko ya sheria kwa ajili ya kuitambua rasmi Mahakama ya Kadhi.Muswada huo umepangwa kuwasilishwa, kujadiliwa na kupitishwa katika kikao cha Bunge litakaloanza vikao vyake Jumanne wiki hii mjini Dodoma.

Katika mashtaka yake, Mchungaji Mtikila aliye Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Democratic (DP), anaitaka mahakama kuu kufanya mambo makuu matatu.

Kwanza, anaitaka imwadhibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju, kwa kumpa kifungo kisichopungua miaka mitano kutokana na kitendo chake cha jaribio la kuvunja ibara ya 19 ya Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977.

Pili, anaitaka itamke kwamba ni kinyume cha sheria kwa serikali kujihusisha katika masuala yoyote yanayohusu Mahakama ya Kadhi au Shirika la Waislamu Duniani (OIC).

Na tatu, anaitaka Mahakama Kuu itamke kwamba adhabu zinazotolewa na Mahakama ya Kadhi kwa mujibu wa sheria za Kiislam (sharia), kama vile viboko, kupondwa mawe hadi kufa, kukata kichwa, na kukata mikono, zinapingana na utu wa binadamu, na ni kinyume cha Tamko la Umoja wa Mataifa Kuhusu Haki za Binadamu.
 
nampenda Mtikila kwani ndiye mpinzani wa kwlei ingawa kwakukosa mass sapoti huwa anaishia kushindwa.
namuombe akila la heri manake amethubutu
 
Maneno hayavunji mfupa jama tena kwetu wanasema kinywa hakikumbuki kilichotoka. Nnani atazuia Bunge letu tukufu kujadili jambo hilo? Ni nani yumo mle mjengoni wa kusimama na kuomba mwongozo wa Spika wakati majority ni ccm nao wana kiu ya kuwapa rushwa wenye huo mswada ili kupata kura zao?
Hii, nasema ni rahisi sana kupeleka mahakamani, lakini hiyo mahakama ikijua kuwa wapo kwenye mtego wa Escrow sidhani watapenda kusumbuana na bunge. Haipiti mahakamani
 
WELL done Mtikila! Siyo kila siku tunaishia kulalamika! Huwa ananifurahisha kwa kuchukua hatua kama hizi dhidi miungu watu nchi hii!
 
Maneno hayavunji mfupa jama tena kwetu wanasema kinywa hakikumbuki kilichotoka. Nnani atazuia Bunge letu tukufu kujadili jambo hilo? Ni nani yumo mle mjengoni wa kusimama na kuomba mwongozo wa Spika wakati majority ni ccm nao wana kiu ya kuwapa rushwa wenye huo mswada ili kupata kura zao?
Hii, nasema ni rahisi sana kupeleka mahakamani, lakini hiyo mahakama ikijua kuwa wapo kwenye mtego wa Escrow sidhani watapenda kusumbuana na bunge. Haipiti mahakamani

Tuungane kumpongeza walau jamaa kwa kuonyesha wazi wazi kuupinga mswada huo.
 
Mtikila awe mkweli.....hii ni dhamira yake au imetengenezwa baada ya mambo kuonekana magumu ili muswada usijadiliwe kwa kisingizio mambo yapo mahakamani???Kama ni hivyo itabidi walioahidiwa mahakama wachukuwe maamuzi magumu.
 
Ipo siku kafiri akaitambua njia iliyo sahihi.Haya mambo ya haki za binadamu imepelekea sasa kanisa kukubali kufungisha ndoa za jinsia.Huku ustaarabu wote wa maisha yasiyo na wizi,ufisadi,mwanamke kudhalilishwa kufanywa chombo cha matangazo ya biashara upo ktk nchi zinazofuata taratibu za maisha ya kiislam
 
Ipo siku kafiri akaitambua njia iliyo sahihi.Haya mambo ya haki za binadamu imepelekea sasa kanisa kukubali kufungisha ndoa za jinsia.Huku ustaarabu wote wa maisha yasiyo na wizi,ufisadi,mwanamke kudhalilishwa kufanywa chombo cha matangazo ya biashara upo ktk nchi zinazofuata taratibu za maisha ya kiislam
BONGOLALA unataka mahakama ya kadhi ihudumiwe na kodi za wakristo?

Unataka kuleta mambo ya dini kwenye serikali yenye jamii ya watu dini mbalimbali ?

Hebu amka mkuu usifanane na jina lako.
 
Ipo siku kafiri akaitambua njia iliyo sahihi.Haya mambo ya haki za binadamu imepelekea sasa kanisa kukubali kufungisha ndoa za jinsia.Huku ustaarabu wote wa maisha yasiyo na wizi,ufisadi,mwanamke kudhalilishwa kufanywa chombo cha matangazo ya biashara upo ktk nchi zinazofuata taratibu za maisha ya kiislam

Akhi wala usisumbuke... ni swala la muda tu,,, by the way hii mahkama ya kadhi ya kisanii hakuna muislam anashida nayo wanasumbuka bure,, tumeamrishwa kusimamishe sheria ya Allah yote na sio kuchagua vipande vipande .. kama haiwezekani basi hakuna haja ya kusema tuna mahkama wakati ni dhihaka ,, mimi naipinga kwa mantiki hiyo hatuitaki
 
Back
Top Bottom