Mtikila amefichua mipango ya wafugaji kushika hatamu?

Mtikila amefichua mipango ya wafugaji kushika hatamu?

meningitis

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2010
Posts
8,464
Reaction score
4,828
Ukifuatilia mtiririko wa shutuma za mtikikila dhidi ya lowassa utaona kuna ujumbe uliojificha!
UJUMBE HUU unaweza kuwagawa wapiga kura na pengine ukachukuliwa serious na wanausalana,wanasiasa na hatimaye wapiga kura.

Ina maana kuna mkakati uliosukwa na wakulima ili kumpitisha mtu wao na baadaye wafanye yao?

Je kuna ukweli wowote kwamba EL hajaongelea mikakati yoyote ya kuwakwamua wakulima?

Je kuna mgombea yoyote kupitia ccm ameligusia suala la migogoro ya wakulima na wafugaji?

Je kuna mgombea yoyote ni pro-wakulima au pro-wafugaji.

Siasa zinatupeleka pabaya sana iwapo suala hili litaachwa kumea.

Usalama wa Taifa ni lazima waingilie kati ili kuepusha aina yoyote ya kupolarize jamii ya kitanzania.

Wagombea kupitia midahalo wajiweke wazi juu ya swala hili kabla ya kukutana na mvutano unaofanania na ule wa kidini 2010.

Ni maoni ya tahadhari tu.tusiweke siasa mbele.
 
Ubaguzi wa rangi,dini au kabila usipewe nafasi katika uchaguzi huu.
 
Mtikila kajisemea kweli tu kwamba lowasa hafai hata kwa kachumbari.
 
nakumbuka arusha wakati lowasa anatangaza nia mwenyekiti wa wafugaji Tanzania nzima alisema kuwa kuna wafugaji milioni 17 nchi nzima ambao wote watamuunga mkono Lowasa, hii ni hatari kabisa lazima usalama wa taifa waliangalie hili kwa makini, kuna maeneo ambayo kuna wafugaji wengi wa kimasai wanasema kabisa mtu wao Lowasa alikamata nchi waswahili watakopma, waswahili kwa maana ya wakulima.

hii leo kuna wilaya kuna mikoa kama morogoro wakul;ima wameshindwa kulima kutokana na vurugu za hawa jamaa, wilaya zingine kama wakulima wanalazimika kuvuna usiku na mchana na mchana kutokana na wafugaji wanaingiza mifugo mashambani kwa makusudi kabisa, hofu yangu kwamba mtuwao hajapa nchi imekuwa hivi na wanajitapa je wakipata itakuwaje?

Tanzania tunamtaka rais ambaye, si mdini, mkabila wala aliyeegemea upande wowote wote. vyombo vya usalama vifuatilie hili nendeni mkoa mmoja wa kasakazini kaangalie mtapata ukweli juu ya hili la mtikila. ingawa anajulika mlopokaji lakini wakati mwingine anakuwa sahihi
 
Ukifuatilia mtiririko wa shutuma za mtikikila dhidi ya lowassa utaona kuna ujumbe uliojificha! UJUMBE HUU unaweza kuwagawa wapiga kura na pengine ukachukuliwa serious na wanausalana,wanasiasa na hatimaye wapiga kura. Ina maana kuna mkakati uliosukwa na wakulima ili kumpitisha mtu wao na baadaye wafanye yao? Je kuna ukweli wowote kwamba EL hajaongelea mikakati yoyote ya kuwakwamua wakulima? Je kuna mgombea yoyote kupitia ccm ameligusia suala la migogoro ya wakulima na wafugaji? Je kuna mgombea yoyote ni pro-wakulima au pro-wafugaji. Siasa zinatupeleka pabaya sana iwapo suala hili litaachwa kumea. Usalama wa Taifa ni lazima waingilie kati ili kuepusha aina yoyote ya kupolarize jamii ya kitanzania. Wagombea kupitia midahalo wajiweke wazi juu ya swala hili kabla ya kukutana na mvutano unaofanania na ule wa kidini 2010. Ni maoni ya tahadhari tu.tusiweke siasa mbele.
Kwanza kabisa Bw.Lowasa kiasilia siyo Mmasai (mfugaji) bali ni Mmeru kam vile Bw.Slaa!
 
Watu wengi hawafahamu.lowasa akichukua madaraka ya nchi hii ng'ombe watachunga mpaka viwanja vya ikulu.
 
Mtikila njaa inamsumbua nilicheka sana alikuwa anaenda kwa Rostam kupiga mizinga Rostam alivyokuwa muhuni alikuwa anamsainisha kila akimpa pesa, Mtikila akajisahu akaanza kumponda Rostam kwenye media Rostam akaweka wazi Mtikila alivyokuwa anakwenda Caspian kuvuta pesa, Mtikila akajitetea eti alikopa.

Teh teh teh!!
 
Ebanaee. Kwahyo Maasai kasikia jamaa akishika nchi atakuwa anachunga kwenye mashamba ya watu ndo maana anamkubali jamaa? Heh.

Anyway, watu wakikosa mvuto kwa watu ndo wanaingiza mambo ya kipuuzi kama hayo
 
Mtikila njaa inamsumbua nilicheka sana alikuwa anaenda kwa Rostam kupiga mizinga Rostam alivyokuwa muhuni alikuwa anamsainisha kila akimpa pesa, Mtikila akajisahu akaanza kumponda Rostam kwenye media Rostam akaweka wazi Mtikila alivyokuwa anakwenda Caspian kuvuta pesa, Mtikila akajitetea eti alikopa.

Teh teh teh!!

Nakumbuka mtikila alivyopigwa Tarime kwa kuwatetea ccm lakini siwezi kudharau baadhi ya maneno yake.
 
Umakini unaitajika apa kuna ukweli fulani ivi
 
Ukiona Mtikila anapewa dakika Karibu 10 Taarifa ya habari TBC ambayo Sikumbuki Mara ya mwisho habari gani ya upinzani sembuse Mtikila ilipewa umuhim ujuwe kuna kitu hapo !!
 
Mtikila ni chombo cha system cha kuwayumbisha wa TZ lakini mwisho wake atafikia pabaya na yeyote anaye muunnga mkono mtikila namuonea huruma sana , kwani ni upuuzi mtupu yanayo toka kinywani mwake. ..... !
 
Mtikila njaa inamsumbua nilicheka sana alikuwa anaenda kwa Rostam kupiga mizinga Rostam alivyokuwa muhuni alikuwa anamsainisha kila akimpa pesa, Mtikila akajisahu akaanza kumponda Rostam kwenye media Rostam akaweka wazi Mtikila alivyokuwa anakwenda Caspian kuvuta pesa, Mtikila akajitetea eti alikopa.

Teh teh teh!!

Huu ni uongo wa wazi kabisa! unaweza kuthibitisha?
 
Back
Top Bottom