nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,860
- 5,803
[TABLE="width: 879"]
[TR]
[TD="bgcolor: #ffffff"][TABLE="width: 599"]
[TR]
[TD]
[/TR]
[/TABLE]
[/TD]
[TD="width: 140, bgcolor: #FFFFFF"][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][TABLE="width: 599"]
[TR]
[TD]
[/TR]
[/TABLE]
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TR]
[TD="bgcolor: #ffffff"][TABLE="width: 599"]
[TR]
[TD]
na Danson Kaijage, Mtera
[/TD][/TR]
[/TABLE]
[/TD]
[TD="width: 140, bgcolor: #FFFFFF"][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][TABLE="width: 599"]
[TR]
[TD]
WANANCHI wa kijiji cha Igunguli, kata ya Loje, wilayani Chamwino, mkoani Dodoma, wamemshukia mbunge wa jimbo la Mtera, Livingstone Lusinde (CCM), kwa kushindwa kutekeleza ahadi alizozitoa wakati wa kampeni ya kuwania ubunge mwaka 2010 badala yake amekuwa akitumia muda mwingi kutukana.
Wakizungumza na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti kijijini hapo, walisema kuwa mbunge huyo badala ya kutekeleza masuala muhimu amekuwa hodari wa kutukana majukwaani na kufanya ziara mbalimbali za kisiasa nje ya jimbo lake wakati wananchi wake wanakabiliwa na matatizo mengi.
Emanuel John alisema tangu mbunge huyo achaguliwe hajawahi kufika kijijini hapo licha ya kuwaahidi kuwafanyia mambo mengi ya maendeleo.
Alisema kuwa ili kuonyesha ni jinsi gani Lusinde hayuko karibu na wananchi aliahidi kumsomesha mtoto ambaye alifiwa na baba yake na kubakiwa na mama ambaye hana uwezo lakini mpaka sasa hajafanya lolote juu ya mtoto huyo.
"Wakati wa kampeni Lusinde aliahidi kuwasaidia watoto yatima pamoja na wasiojiweza lakini cha kushangaza mpaka sasa hajatimiza jambo hata moja," alisema John.
"Mbaya zaidi ni pale ambapo anapotakiwa kufanya mikutano amekuwa akikwepa hata leo (jana) alitakiwa kufanya mkutano wa hadhara katika kijiji cha Igunguli lakini hadi sasa hakuna kinachoendelea na nasikia ameuahirisha," alisema John.
Alisisitiza kuwa imekuwa aibu kwa mbunge huyo kushindwa kutekeleza ahadi ya mtoto ambaye hana baba na mama yake ni mgonjwa lakini alipofuatwa nyumbani kwake alitoa shilingi 5,000.
Wananchi wengine ambao ni makada wa CCM ambao hawakutaka kutaja majina yao walisema inasikitisha kuona kuwa mbunge huyo amekuwa akizunguka mikoani kutumia majukwaa kutukana badala ya kukaa jimboni kwake kutimiza ahadi ambazo alizitoa wakati wa kipindi cha kampeini mwaka 2010.
Mmoja wao ambaye hakutaka kutaja jina lake gazetini alisema mbunge huyo kwa sasa hawafai kwa jambo lolote na ni bora wangechagua vyama vya upinzani.
"Hapa Mtera hatuna mbunge, angalia leo tulishajipanga kumpokea mbunge wetu kwa ajili ya kumpa kero zetu lakini hakujali na sasa tumepata taarifa kuwa hatakuja katika mkutano wa hadhara.
Alipotafutwa mbunge huyo kwa njia ya simu kujibu malalamiko hayo hakuweza kupatikana badala yake alipatikana katibu wake aitwaye Patrick Nyambua ambaye alikiri bosi wake kutakiwa kufanya mkutano jana katika kijiji cha Igunga lakini kutokana na mwingiliano wa ratiba hakuweza kufanya mkutano huo.
"Siyo kweli kuwa mbunge amekimbia mkutano, bali kilichotokea ni kuwa amepata ratiba ya kwenda Mtwara hivyo isingekuwa rahisi kufanya mkutano huo," alisema katibu wa mbunge.
Kuhusu kutekeleza ahadi za mbunge huyo katibu wake alisema kuwa utekelezaji au kutokutekeleza ni jukumu la mbunge mwenyewe.
[/TD]Wakizungumza na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti kijijini hapo, walisema kuwa mbunge huyo badala ya kutekeleza masuala muhimu amekuwa hodari wa kutukana majukwaani na kufanya ziara mbalimbali za kisiasa nje ya jimbo lake wakati wananchi wake wanakabiliwa na matatizo mengi.
Emanuel John alisema tangu mbunge huyo achaguliwe hajawahi kufika kijijini hapo licha ya kuwaahidi kuwafanyia mambo mengi ya maendeleo.
Alisema kuwa ili kuonyesha ni jinsi gani Lusinde hayuko karibu na wananchi aliahidi kumsomesha mtoto ambaye alifiwa na baba yake na kubakiwa na mama ambaye hana uwezo lakini mpaka sasa hajafanya lolote juu ya mtoto huyo.
"Wakati wa kampeni Lusinde aliahidi kuwasaidia watoto yatima pamoja na wasiojiweza lakini cha kushangaza mpaka sasa hajatimiza jambo hata moja," alisema John.
"Mbaya zaidi ni pale ambapo anapotakiwa kufanya mikutano amekuwa akikwepa hata leo (jana) alitakiwa kufanya mkutano wa hadhara katika kijiji cha Igunguli lakini hadi sasa hakuna kinachoendelea na nasikia ameuahirisha," alisema John.
Alisisitiza kuwa imekuwa aibu kwa mbunge huyo kushindwa kutekeleza ahadi ya mtoto ambaye hana baba na mama yake ni mgonjwa lakini alipofuatwa nyumbani kwake alitoa shilingi 5,000.
Wananchi wengine ambao ni makada wa CCM ambao hawakutaka kutaja majina yao walisema inasikitisha kuona kuwa mbunge huyo amekuwa akizunguka mikoani kutumia majukwaa kutukana badala ya kukaa jimboni kwake kutimiza ahadi ambazo alizitoa wakati wa kipindi cha kampeini mwaka 2010.
Mmoja wao ambaye hakutaka kutaja jina lake gazetini alisema mbunge huyo kwa sasa hawafai kwa jambo lolote na ni bora wangechagua vyama vya upinzani.
"Hapa Mtera hatuna mbunge, angalia leo tulishajipanga kumpokea mbunge wetu kwa ajili ya kumpa kero zetu lakini hakujali na sasa tumepata taarifa kuwa hatakuja katika mkutano wa hadhara.
Alipotafutwa mbunge huyo kwa njia ya simu kujibu malalamiko hayo hakuweza kupatikana badala yake alipatikana katibu wake aitwaye Patrick Nyambua ambaye alikiri bosi wake kutakiwa kufanya mkutano jana katika kijiji cha Igunga lakini kutokana na mwingiliano wa ratiba hakuweza kufanya mkutano huo.
"Siyo kweli kuwa mbunge amekimbia mkutano, bali kilichotokea ni kuwa amepata ratiba ya kwenda Mtwara hivyo isingekuwa rahisi kufanya mkutano huo," alisema katibu wa mbunge.
Kuhusu kutekeleza ahadi za mbunge huyo katibu wake alisema kuwa utekelezaji au kutokutekeleza ni jukumu la mbunge mwenyewe.
[/TR]
[/TABLE]
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]