Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikisikia na kuona katika vyombo vya habari mbalimbali ukiwa unatoa matamko, kusifia na wakati fulani kukosoa vyama vya upinzani kupitia JUKWAA LA WAZALENDO!
Aidha umekuwa ukitajwa kama katibu wa jukwaa hilo. Sijawahi kusikia mwenyekiti wa jukwaa hilo, sijui kama kuna wajumbe, sifahamu kama jukwaa hilo lina uongozi kama ulivyo kwenye vyama au majukwaa mengine.
Jukwaa huru la wazalendo, mimi nina maswali yafuatayo:
1. Alianzisha nani jukwaa hilo?
2. Kwa malengo gani??
3. Lilisajiliwa lini??
4. Je, siyo jukwaa la kusaka vyeo na umaarufu ili waonekane??
5. Nani mwenyekiti wa jukwaa hili??
6. Ofisi za jukwaa hilo ziko wapi??
7. Jukwaa hilo linatusaidia vipi sisi watanzania??
8. Kwanini Mtela Mwampamba anaye dhaniwa kuusaka ukuu wa Wilaya na vyeo awe katibu mkuu wa jukwaa hilo??
9. Kwanini kinara wa matamko katika jukwaa hilo ni Mtela Mwampamba peke yake??
10. Jukwaa hilo lilifanya uchaguzi wa viongozi wake lini?? Au lina Mfumo kama wa Ccm kwenye ngazi ya uenyekiti yaani kupokezana??
"MAJUKWAA YA MATAMKO"!!
NB: Anaye fahamu na anaweza kujibu maswali haya naomba anisaidie pia kufahamu.