"Mtego" wa teknolojia

"Mtego" wa teknolojia

TheChoji

JF-Expert Member
Joined
Apr 14, 2009
Posts
6,551
Reaction score
20,259
Wadau mi kuna kitu nimegundua. Nadhani hawa watengenezaji wa vifaa mbalimbali vya kielektroniki kama simu, tablet na kompyuta ni WEZI na hawana lengo zuri kabisa na sisi walaji na wanashirikiana kutufilisi bila sababu yoyote kwa kisingizio cha kukua kwa teknolojia.. We hebu jiulize..

Ni kwanini kiila mara watengenezaji wa softiwea za simu na kompyuta wanatoa "vesheni" mpya za softiwea, ambazo zina mahitaji makubwa zaidi ya zile zilizotangulia, huku kukiwa hakuna tofauti yoyote ya kimsingi ya kiutendaji kati ya vesheni ya zamani na ya sasa? Jambo ambalo linatulazimisha sisi walaji kila mara ku- apdeti hadwea au kununua kompyuta/simu mpya, kwa kuwa eti tulizo nazo hazina "spesifikesheni"?

Nitatoa mfano: Mimi nimeanza kutumia kompyuta rasmi mwanzoni mwa miaka ya elfu mbili. Enzi zile, tulikua tunatumia Windows 98, japo windows 95 zilikuwepo kuwepo bado.. Basi bwana kipindi kile "Maikrosofti Wedi" ilikua ni ya 97. Kwa wale ambao hamkuwepo naomba niwaambie tu kwamba.. Microsoft Word 1997 ilikua inafanya kila kitu ambacho Word 2013 inafanya na zaidi!! Ila Windows 98 na Office 97 zote kwa pamoja zilikua zinaenea kwenye kompyuta yenye 1Gb HDD, na nafasi inabaki kuubwa tuu.. hapo una RAM yako ya 32Mb na processor 133Mhz..aah shwari kabisa..

Sasa hivi ku install Windows 8 unatakiwa uwe na minimum ya 16 - 20Gb HDD, 2Gb RAM na processor ya 2Ghz!!
- Windows 8 kazi yake ni kuwasha kompyuta....... Kama ilivyokuwa Windows 98
- Microsoft Word 2013 ni ya kutaipu barua ........... Kama ilivyokua Word 97
- Functions zote zilizoko kwenye Excel 2013 ......... Ni kopi pesti ya Excel 97.. nakadhalika.
- Windows Media Player ni ile ile.. Paint ni ile ile.. Solitaire HAMNA!! Sasa huu kama sio WIZI ni nini?

Kwanini hawa wanaotengeneza kompyuta na software hawatengenezi software bora lakini zenye ujazo mdogo ili kupunguza mzigo wa gharama kwa watumiaji? Au watoe "Windows 7 Lite" au "Mini" au "Windows 8i" kwa sisi watu wa kawaida ili tusinunue kompyuta mpya ndani ya walau miaka kumi? Eeeh!
Hebu jiulize, watengenezaji wa injini za magari wanawezaje ku maintain "aspekt reshio" ya ukubwa wa injini na "Horsepower"? Kama wangekua kama hawa watengeneza softwea, si gari zote V8 zingekua na injini kubwa kama kichwa cha treni?? :thinking:

Wadau hebu niambieni tunaondokaje kwenye huu mtego? Maana naona na kwenye simu trendi ni hiyo hiyo.. Android 2.1, 2.2, 2.3, 3.0, 3.1, 3.2, 3.3, ....4.0, 4.1, 4.2, 4.3.. Bora tena kwenye kompyuta softwea zinakua kubwa huku hadiwea zinapungua ukubwa, sasa kwenye simu softiwea zinakua kubwa NA simu nazo zinakua kubwa!! Mwisho tutakua na simu kubwa kama kompyuta, na kompyuta ndogo kama simu..!!
 
Dah, mkuu umenena vyema ila jua kama hizi ni biashara hivyo wanatubania au wanaumiza vichwa ili kupiga pesa.
 
Dah, mkuu umenena vyema ila jua kama hizi ni biashara hivyo wanatubania au wanaumiza vichwa ili kupiga pesa.

Hawa jamaa washatufanya shamba la bibi..
 
Excellent!! halafu jitu lije kukandia, wakati ukweli ndo huo, PC 690,000 Windows 8 120,000 jumla 810,000 halafu matumiz na function kama za ile ile desktop yangu ya 1999 nilonunua 120,000 (kama 240,000 za sasa), WIZI MTUPU
 
Kuna jamaa yangu nilimkuta anatumia Windows 2000 na word perfect katika zama hizi za Windows 8 na office 2013. Nilipo muuliza kulikoni anatumia programu za zamani akaniambia kuwa haoni tatizo lolote maana zinafanya kazi vizuri.
 
Version za software hulenga pia katika kurekebisha matatizo ya usalama (vulnerability). Pia nahakika ukichunguza MS Word 9 na MS word 2012 utaona nyongeza ya vitu vingi. Kwa mtumiaji wa kawaida yaani kutaipu barua kama ulivyosema huwezi ona utofauti.

Kuhusu simu kuwa kubwa kadiri version ya android inanyoongezeka si sahihi kwa upande wangu. Watu wengi hupenda simu zenye kioo kikubwa kwa sababu mbalimbali. Simu nyingi zinauwezo wa kufanya version update na zikatumia version ya juu zaidi pasipo shida.
 
Umenena mkuu MS na wadau wenzake ni wezi jamaa aliuliza gari zingekuwa zinaenda kama simu au computer sasa tungekuwa na V32 kutoka V8.
 
Kuna jamaa yangu nilimkuta anatumia Windows 2000 na word perfect katika zama hizi za Windows 8 na office 2013. Nilipo muuliza kulikoni anatumia programu za zamani akaniambia kuwa haoni tatizo lolote maana zinafanya kazi vizuri.

Mkuu ukichunguza vizuri utagundua kwamba kwa mazingira yetu kwa mfano ya Kitanzania, kwenye maofisi ofisi humu.. kwenye taasisi mbalimbali ambazo zinadili na vitu vya kawaida, Windows 98 bado ingetosha kabisa kufanikisha kazi za sehemu kama hizo.. Ila ni wizi tu wa hawa jamaa kujidai ku apdeti kila siku kumbe wanataka tuendelee kuwa watumwa wa kununua bidhaa zao milele..!
 
Version za software hulenga pia katika kurekebisha matatizo ya usalama (vulnerability). Pia nahakika ukichunguza MS Word 9 na MS word 2012 utaona nyongeza ya vitu vingi. Kwa mtumiaji wa kawaida yaani kutaipu barua kama ulivyosema huwezi ona utofauti.

Kuhusu simu kuwa kubwa kadiri version ya android inanyoongezeka si sahihi kwa upande wangu. Watu wengi hupenda simu zenye kioo kikubwa kwa sababu mbalimbali. Simu nyingi zinauwezo wa kufanya version update na zikatumia version ya juu zaidi pasipo shida.

Ni kweli mkuu, ila kumbuka watumiaji wengi ni hao wa kutaipu barua! na ndio maana nikasema kwanini wasiwe wanatoa versions ambazo ni "Lite" ili mimi mtumiaji wa kawaida ambaye nina kompyuta yenye 2Gb hard disk, 256Mb RAM niendelee kuitumia hiyo hiyo?
 
Mkuu ukichunguza vizuri utagundua kwamba kwa mazingira yetu kwa mfano ya Kitanzania, kwenye maofisi ofisi humu.. kwenye taasisi mbalimbali ambazo zinadili na vitu vya kawaida, Windows 98 bado ingetosha kabisa kufanikisha kazi za sehemu kama hizo.. Ila ni wizi tu wa hawa jamaa kujidai ku apdeti kila siku kumbe wanataka tuendelee kuwa watumwa wa kununua bidhaa zao milele..!

Ndiyo hivyo mkuu, wasipoupdate watoto hawaendi msalani.
 
Teknology inaenda ikikua jamani pamoja na kwamba ni kweli wanatuibia lakini pia wanafanya kazi kubwa ili kuweza kutushawishi.hata magari kila mwaka wanatoa modeli mpyaa
 
Mkuu TheChoji kwa mtumiaji wa mwisho kwa kweli updates za kila mara hazina mashiko ila kwa watengenezaji zina mashiko maana unazungumzia pesa wanayoingiza, wengi wetu huku tunatumia pirated copies za software ila kwa wanaonunua software ni tatizo mfano serikali ya china imekataa kununua windows 8 badala yake wamesema watakomaa na windows xp ambapo watakuwa wanapata security patches kutoka kwa wataalamu wao wa china,

software na hardware zinaendana sana, ni kama antivirus na virus,
kila hardware manufacturers wanapokuja na hardware mpya inawapa uhuru watengeneza software kuhama kutoka ya zamani kuja kwenye mpya ili ziende sambamba, mfano application nyingi zinazotoka siku izi utaona hata muonekano tu zinakuwa na flat ui, mimi microsoft siwalaumu sana maana kutoka windows xp kwenda windows 7 imechukua muda wa kutosha tu, na wameacha kutoa sapoti ya xp hivi karibuni toka 2002,

tukija kwenye simu mfano windows phone nahisi wanataka wawe wanaenda sambamba na pc editions mfano walitoa wp7, 8 na sasa 8.1 update

ila kwa android daaaaah hapo tatizo hasa kwa watumiaji wa kawaida tu ambao hata ingekuwa inatumia froyo bado wangeendelea kutumia tu,
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli mkuu, ila kumbuka watumiaji wengi ni hao wa kutaipu barua! na ndio maana nikasema kwanini wasiwe wanatoa versions ambazo ni "Lite" ili mimi mtumiaji wa kawaida ambaye nina kompyuta yenye 2Gb hard disk, 256Mb RAM niendelee kuitumia hiyo hiyo?

Kwa hapo nakuunga mkono mkuu, Nadhani mbinu nzuri pia ni kusubmit feedback kwa microsoft. Naamini ni watu wengi sana wataounga mkono wazo hili
 
Ni kwanini kiila mara watengenezaji wa softiwea za simu na kompyuta wanatoa "vesheni" mpya za softiwea, ambazo zina mahitaji makubwa zaidi ya zile zilizotangulia, huku kukiwa hakuna tofauti yoyote ya kimsingi ya kiutendaji kati ya vesheni ya zamani na ya sasa?
Any proof? To the best of my knowledge this is outright lie!
 
Guys nyie ni adui wa maendeleo, huwez fananisha windows za zamani na mpya at all, niachane na games na software za starehe hivi utampa mtu windows 98 afanye graphic design na kuedit video?

nna mashaka hata kama hio office mnaitumia, now sasa hv nablog direct toka office sihitaji kujua code nachora majedwali yangu naeka picha na vitu complicated ambavyo vingehitaji mamia ya mistari ya code. Naweka 3d modal za kwenye excel kwa ajili ya presentation, kuna magraph ya rangi yanayopendeza na vitu vingi.

all in all hujalazimishwa ku upgrade computer ni mahitaji tu yanatuforce
 
Back
Top Bottom