Mtatiro: Ufafanuzi wa Elimu yake

Mtatiro: Ufafanuzi wa Elimu yake

Ufipa-Kinondoni

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2012
Posts
4,582
Reaction score
2,783
Mtatiro ni mtu ninayependa sana kusoma maandiko yake kule facebook hata kwenye gazeti la mwananchi. Amekuwa anajitahidi sana kuachambua na kuweka uwazi wa vitu vingi ambavyo tulikuwa hatuvijui. Amefanya hivyo tangu harakati za mchaguzi mkuu uliopita zilipoanza.

Nimeona kwenye Gazeti la Mwananchi leo akionyesha digrii aliyosoma huku ikiwa haitolewi na chuo chochote hapa Tanzania. Ukweli amesoma Mlimani (UDSM) digrii ya kwanza. Na inajulikana yeye ni mwalimu.

Ila anaonyesha kasoma B.A. Elimu (Lugha, Siasa na Utawala). kwa ninanvojua, hakuna digrii hii. Au ni kuonyesha kuwa amebobea kwenye utawala? Hizi zingine sina shida nazo kwa maana najua zinatolewa na vyuo vyetu.

Naomba ufafanuzi kwa mwenye uelewa zaidi.

http://www.mwananchi.co.tz/Makala/-/1597592/2997542/-/rwhsyw/-/index.html
 
Anajikweza, sema kuna eneo labda ali major (Ling) na hizo zingine zikawa minor (PS) ..najaribu kufikiri tu.
 
Unaomba ufafanuzi kwa mwenye uelewa wakati yeye mwenyewe mwisho huweka mawasiliano yake? kwanini usimuulize moja kwa moja? nahisi harufu ya umadereva
 
Hakuna B . A Education au? Maana izo kwenye mabano ni options kwenye digrii iyo. Mfano mtu anaweza kuwa mwanasheria lakini akawa commercial lawyer , au environmentalist nk nk...au mtu akawa mwalimu lakini wa siasa, au lilimo au mathematics.
Si sawa mtu akiwa mwalimu lazma awe mwalimu tu, zipo combine degrees nk nk.

For your information Mtatiro pia amesomea sheria , nakumbuka yeye na jerry slaa at varied events tulishakutana mahala (w)akisoma sheria na nadhani atakuwa amehitimu sasa.

Vinginevo aje pia atueleze maana ni mwanajf!!
 
Una maanisha nini kuwa hakuna B.A Education, ( sidhani mimi nina barchelor of Art with Education) kifupi chake si ndiyo B.A.Education?
 
Mtatiro alisoma Ba with education( siasa na kiswahili) wale walimu wa miaka minne, baadae akafanya Ma in political science udsm, na pia ana degree ya sheria ya tumaini
 
Mtatiro katika makala zake mwisho huwa huweka mawasiliano yake so kama unatakuelewa elimu yake mpigie simu na uzuri wake huwa yuko fast kurespond . Hiki unachotaka kufanya hapa ni umbea
 
Majuzi Mtatiro amehitimu shahada ya sheria pale Tumaini university achilia mbali degree zingine alizonazo ....kwa kifupi Mtatiro ana elimu nzuri tufunge mjadala ....
 
Ni vizuri kupata michango ya watu na wengine wataelewa kama wewe. Sijui kama una ufahamu wa hayo yanayochangiwa na wengine?
Mtatiro katika makala zake mwisho huwa huweka mawasiliano yake so kama unatakuelewa elimu yake mpigie simu na uzuri wake huwa yuko fast kurespond . Hiki unachotaka kufanya hapa ni umbea
 
Itakuwa Political Science and Public Administration (PSPA) na somo mojawapo la lugha!
 
Tuache kujadili vitu vyepesi. JK alikuwa profesa lkn haikutusaidia watz. Bora huyu bachelor inaonekana hata kwenye makala zake.
 
Mtatiro ni mtu ninayependa sana kusoma maandiko yake kule facebook hata kwenye gazeti la mwananchi. Amekuwa anajitahidi sana kuachambua na kuweka uwazi wa vitu vingi ambavyo tulikuwa hatuvijui. Amefanya hivyo tangu harakati za mchaguzi mkuu uliopita zilipoanza.

Nimeona kwenye Gazeti la Mwananchi leo akionyesha digrii aliyosoma huku ikiwa haitolewi na chuo chochote hapa Tanzania. Ukweli amesoma Mlimani (UDSM) digrii ya kwanza. Na inajulikana yeye ni mwalimu.

Ila anaonyesha kasoma B.A. Elimu (Lugha, Siasa na Utawala). kwa ninanvojua, hakuna digrii hii. Au ni kuonyesha kuwa amebobea kwenye utawala? Hizi zingine sina shida nazo kwa maana najua zinatolewa na vyuo vyetu.

Naomba ufafanuzi kwa mwenye uelewa zaidi.

NANI NI NANI SERIKALI YA JPM?: Dk Kigwangalla-Naibu Waziri wa Afya, - Makala | Mwananchi

Huyu jamaa hata mimi ananipa mashaka nilimkuta pale UDSM mwaka mmoja mbele ila alifukuzwa chuo hadi mimi nimemaliza yeye alikua bado sasa sijui kama alikuja kumalizia tena au vipi.
 
Back
Top Bottom