Nakapanya
JF-Expert Member
- May 22, 2012
- 2,096
- 709
Kesho ndio kesho,mtani jembe inakamilika,Simba na Yanga ndani ya uwanja wa Taifa.
Niseme wazi,mashabiki wa Yanga wanajiaminisha kwa kiasi kikubwa kuwa kesho anaenda kuibuka na ushindi mkubwa dhidi ya mpinzani wao Simba.Mataumaini hayo yanjengeka kutokana na sababu kuu mbili au tatu:-
a)Gogoro lililopo ndani ya Simba,mashabiki na wanachama pamoja na baadhi ya viongozi hawamtaki Mwenyekiti wa klabu bwana Rage,hivyo wanaona gogoro hilo liawaathiri Simba na kuruhusu kichapo cha magoli mengi ikiwezekana kurudisha zile goli tano.
b)Ujio wa Emmanuel Okwi ndani ya klabu ya Yanga,Yanga wanaamini Okwi ndio atakuwa goal machine yao ndani ya klabu na hivyo kuwawezesha kuwapiga simba kirahisi kupitia kwa Okwi ambaye amewahi kuichezea simba.
c)Yanga wanajiamini kuwa wanakikosi bora zaidi ya Simba,hivyo wataingia uwanjani kwa kujiamini na huenda yakwakuta kama yale yaliyowakuta kwenye mechi ya mwisho pale uwanja wa taifa.
Ukiangalia hapo juu utagundua tu kuwa Yanga wanajipa asilimia kubwa ya kushinda mechi ya kesho.Lakini niseme mechi itakuwa ngumu sana na huenda mwisho wa siku Yanga wakatoka uwanjani vichwa chini huku wenzao wa simba wakipuliza mavuvuvzela....eeeeh...kidedeaaa
KAZI ILIYOMSHINDA KIIZA ATAIWEZA OKWI?
MFUPA ALIOUSHINDWA BARTHEZ ATAUWEZA KASEJA?
Niseme wazi,mashabiki wa Yanga wanajiaminisha kwa kiasi kikubwa kuwa kesho anaenda kuibuka na ushindi mkubwa dhidi ya mpinzani wao Simba.Mataumaini hayo yanjengeka kutokana na sababu kuu mbili au tatu:-
a)Gogoro lililopo ndani ya Simba,mashabiki na wanachama pamoja na baadhi ya viongozi hawamtaki Mwenyekiti wa klabu bwana Rage,hivyo wanaona gogoro hilo liawaathiri Simba na kuruhusu kichapo cha magoli mengi ikiwezekana kurudisha zile goli tano.
b)Ujio wa Emmanuel Okwi ndani ya klabu ya Yanga,Yanga wanaamini Okwi ndio atakuwa goal machine yao ndani ya klabu na hivyo kuwawezesha kuwapiga simba kirahisi kupitia kwa Okwi ambaye amewahi kuichezea simba.
c)Yanga wanajiamini kuwa wanakikosi bora zaidi ya Simba,hivyo wataingia uwanjani kwa kujiamini na huenda yakwakuta kama yale yaliyowakuta kwenye mechi ya mwisho pale uwanja wa taifa.
Ukiangalia hapo juu utagundua tu kuwa Yanga wanajipa asilimia kubwa ya kushinda mechi ya kesho.Lakini niseme mechi itakuwa ngumu sana na huenda mwisho wa siku Yanga wakatoka uwanjani vichwa chini huku wenzao wa simba wakipuliza mavuvuvzela....eeeeh...kidedeaaa
KAZI ILIYOMSHINDA KIIZA ATAIWEZA OKWI?
MFUPA ALIOUSHINDWA BARTHEZ ATAUWEZA KASEJA?