Mtandao wa Tigo acheni hizi

Mtandao wa Tigo acheni hizi

mtoto wa kibopa

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
5,362
Reaction score
6,480
Wahusika wa huu mtandao naomba mjirekebishe kwa kweli mnatuumiza sasa wananchi wenye vipato vya chini.

Tatizo lenyewe ni huu wizi wa kuwaunganisha wateja wenu vifurushi bila wahusika kujiunga yaani mkiona tu mteja amebakiza salio kwenye simu yake mtafanya kila njia muichukue.

karibia miezi minne mimi nilikuwa nashindwa kuacha salio kwenye simu yangu kwa hofu ya kukatwa salio langu kila nikiwapigia tigo wanadai nitakuwa nimejiunga kifurushi ukweli sijawahi jiunga na hivo vifurushi vyao vya ajabu ajabu.

juzi nikawapigia tena ndipo katika kuangaliangalia huko wakadai nimejiunga kifurushi cha HADITHI nusura nimtukane yule customer care.simu mda wote ninayo mwenyewe iweje nijiunge kwenye huo upuuzi?!

Ukizingatia sijawahi ona hadithi yoyote kwa simu yangu.nikapunguza hasira nikamwomba anipe njia ya kujitoa kwenye huo upuuzi nikafanikiwa kujitoa jana nakuta wameniunga tena automatic huu so mtu kama haupo makini utalia kila
siku.
8ae6472ea1eafbb65879dbaa0a6aa40b.jpg
fcc525991425195abc74c061c849b190.jpg
ab8bc0e40bcbea71150abe61224a011b.jpg
 
Sio tigo tu hata voda ... Alafu na ninyi halotel tunawaangalia tu ninyi jifanyeni.
 
Tigo wanakera balaa aisee...TCRA wamulike huku zaidi
Hii ni hatari kwa mwenzangu na mimi asiye jus kusoma si kila siku ataliwa pesa yake hapa au mtu ambaye wa kupuuzia sms naye atalia huu ni wizi.mimi nilikuwa kila nikiacha hela nakatwa aisee
 
Wahusika wa huu mtandao naomba mjirekebishe kwa kweli mnatuumiza sasa wananchi wenye vipato vya chini.
Tatizo lenyewe ni huu wizi wa kuwaunganisha wateja wenu vifurushi bila wahusika kujiunga yaani mkiona tu mteja amebakiza salio kwenye simu yake mtafanya kila njia muichukue.karibia miezi minne mimi nilikuwa nashindwa kuacha salio kwenye simu yangu kwa hofu ya kukatwa salio langu kila nikiwapigia tigo wanadai nitakuwa nimejiunga kifurushi ukweli sijawahi jiunga na hivo vifurushi vyao vya ajabu ajabu.juzi nikawapigia tena ndipo katika kuangaliangalia huko wakadai nimejiunga kifurushi cha HADITHI nusura nimtukane yule customer care.simu mda wote ninayo mwenyewe iweje nijiunge kwenye huo upuuzi?! Ukizingatia sijawahi ona hadithi yoyote kwa simu yangu.nikapunguza hasira nikamwomba anipe njia ya kujitoa kwenye huo upuuzi nikafanikiwa kujitoa jana nakuta wameniunga tena automatic huu so mtu kama haupo makini utalia kila siku.
8ae6472ea1eafbb65879dbaa0a6aa40b.jpg
fcc525991425195abc74c061c849b190.jpg
ab8bc0e40bcbea71150abe61224a011b.jpg
Hata mimi hii imenikuta sana mkuu.Hivi unaunganishwaje kwenye huduma ambayo hukuiomba?Ajabu sana.Halafu wanang'ang'ania kwa nguvu zote kwamba umejiunga,inakera sana kwa kweli.
 
Hii ni hatari kwa mwenzangu na mimi asiye jus kusoma si kila siku ataliwa pesa yake hapa au mtu ambaye wa kupuuzia sms naye atalia huu ni wizi.mimi nilikuwa kila nikiacha hela nakatwa aisee
na wana ile tabia ya kukata salio bila taarifa asee wanaboa
 
Hata mimi hii imenikuta sana mkuu.Hivi unaunganishwaje kwenye huduma ambayo hukuiomba?Ajabu sana.Halafu wanang'ang'ania kwa nguvu zote kwamba umejiunga,inakera sana kwa kweli.
Ndipo na mimi niliposhangaa hapo sasa.huu ni uhuni TCRA naomba na hili mlichunguze tunaumia kuna siku nimeweka 2000 ili nijiunge kifurushi cha kuongea nikachelewa kidogo tu nakuta washakata halafu ilikuwa ni muhimu kuongea na huyo mtu.daaah halafu wanakata bila kipimo leo hii kesho hii inategemeana umebakiza kiasi gani kwa simu yako
 
..Ili swala lishanikera hadi nikaamua kukausha tu. Ukiacha salio wanadukua 150.

Ukitulia tena wanadukua 150.
 
Kweli wanakera asee, utakuta mtu unasubiria call ya maana unakitax namba inapigwa ukipokea unakuta mi hadithi yao mtu anaanza kulia asee, nna namba zao karibia 3, huwa wanabadilisha na wanatumia no hizi za kawaida asee, yani mpaka mimesevu nani ,waache hii tabia ya kulazimisha watu kujiunga na huduma zao za hadithi[emoji15] [emoji15] [emoji15]
 
Tigo wizi sana, walishawahi kuchukua 10, 000 hivi hivi.
Eti kww maisha haya tuliyonayo, mi nna hela ya kujiunga na kifurushi cha internet cha 10,000?
Walikula hela yangu kwenye tigo pesa, na kusema eti nimejiunga na kifurushi cha internet.
 
Nilitumia namba yangu toka tigo inaitwa buzz mwaka jana nimeitupa chooni
 
Back
Top Bottom