Mtaji wangu umeongezeka Hadi milioni 20

Mtaji wangu umeongezeka Hadi milioni 20

Anko Kong

Senior Member
Joined
Jul 3, 2020
Posts
130
Reaction score
72
Wasalaam wakuu?

Natumaini wote hamjambo,wale wanaoumwa Mungu atawasaidia. Kama kichwa cha habari kinavyojieleza kwanza namshukuru mwenyezi Mungu mtaji wangu umeongezeka hadi kufikia hapo, juzi kati nilikuwa kuomba msaada wa mawazo nilikuwa na 10milion lakini sasa hivi imefika 20milion.

Sina biashara yoyote ila nafikiria kufungua duka la vifaa vya ujenzi naomba mwenye ujuzi na hii biashara anijuze faida na hasara zake, sina uzoefu wowote, nipo Mwanza.

NB: Kama unakuja na utani please usichangie chochote asanteni.
 
Anzisha biashara ya vyakula, huwa haichuji, haina msimu. Watu wanakula siku zote. Vyakula vibichi au vilivyopikwa.

Pia unaweza kufungua biashara ya pesa- Tigopesa, Mpesa, Halopesa, wakala wa mabenki n.k.......tafuta centre nzuri, weka mfumo imara, pata mashine na msimamizi mzuri
 
Nisiwe muongo wala mnafiki, huku jamiiforums kumejaa waongo, matapeli wa kila namna... tukipitia thread yako umesema umekuza mtaji from 10 mil to 20 mil, then ukasema huna biashara.. umekuzaje?? Kwann usikuze pia hy 20 iwe 40
 
Kujikweza kwingi sana humu yaani uwe na shughuli inayokuza mtaji kwa haraka hivyo halafu utake kubadilisha?
 
Back
Top Bottom