gfsonwin
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 18,274
- 20,673
Wanajamvi poleni sana kwa majukumu ya kujenga taifa.
Leo kama kawaida baada ya kukagua jukwaa hili pendwa nimeona nije na huu uzi. Kila mwana MMU akiulizwa swali kwamba nini kinachomsukuma kufanya tendo la ndoa naamini atakuja na jibu kati ya haya hapa. Na ndio maana nikaona niiweke bayana hapa.
1) HAKI YA MSINGI KATIKA NDOA.
Katika ndoa swala la ufanyaji tendo la ndoa limehalalishwa na likawekwa kama sehemu ya kustareheshana na pia kama njia ya kuendeleza vizazi. Wanandoa wafanyapo kamwe hawahesabiwi kuwa wadhambi ama wakosa kwani ndio msingi wa umoja wao.
2) RUSHWA
Baadhi ya watu hufanya ngono kwasababua ya kutaka kununua huduma fulani ama kulipa fadhila fulani. Hii hutokana na ugumu ambao muhusika anao katika jambo husika. ugumu huo waweza kukuta ni wa kifedha, ugumu wa maisha, kazi, cheo, nk. Vijana wengi wa kike kwa wa kiume huanguka katika mtego huu na kujikuta wale wa kiume wakiwa na ma sugar mamy na wakike wakiwa na mabuzi.
3) TABIA
Kuna baadhi ya watu hufanya ngono kwasababu ya tabia tu. Hawa huwakuti na shida ama hitaji lolote lakin bado wanaanguka katika mtego wa kufanya ngono hovyo. wengi wao ni watu walioko kenye ndoa ambao kwao haijalisha kama ana mke ama mume basi lazima tu atakuwa mtu wa kutembea nje ya ndoa yake.
4) BIASHARA
Wapo watu ambao wameamua kuuza miili yao ili kuweza kukidhi haja za kimaisha. wengi wa hawa wawe wakike ama wakiume wapo kwenye uzinzi ili waweze kupata pesa za kujikimu kimaisha. Haijalisha anauza mwili wapi na kwa gharama gani ila wote ni wafanya biashara wa miili yao.
5) STAREHE
Kuna baadhi ya watu ambao hufanya ngono kama moja ya starehe zao. mara nyingi sana hawa ni wale ambao wakoa katika uchumba ama urafiki ambao hujikuta wanahitaji kuliwazana hivyo huliwazana kwa namna ya kufanya ngono.
6) UDADISI
Vijana wadogo wengi hasa school childrens huanguka katika kundi hili. Hawa hutaka kudadisi inafanywaje, inaraha kiasi gani na ikoje. kwao hakuna commitment zaid ya kugundua what is inside it.
HITIMISHO
Tendo la ndoa iwe limefanywa kwa msukumo gani nyuma yake laweza kuishia kupata mimba ama kupata ukimwi. Ingawa wengi husema heri mimba utazaa mtoto kuliko ukimwi, mimi huwa nasema heri ukimwi utakuwa ndani yako wewe uliyeutafuta kuliko mimba ambayo utazaa watoto ambao huwatarajii na hivyo kuongeza idadi ya watoto wanaokosa malezi stahiki.
alwayz
Mwl-gfsonwin
Leo kama kawaida baada ya kukagua jukwaa hili pendwa nimeona nije na huu uzi. Kila mwana MMU akiulizwa swali kwamba nini kinachomsukuma kufanya tendo la ndoa naamini atakuja na jibu kati ya haya hapa. Na ndio maana nikaona niiweke bayana hapa.
1) HAKI YA MSINGI KATIKA NDOA.
Katika ndoa swala la ufanyaji tendo la ndoa limehalalishwa na likawekwa kama sehemu ya kustareheshana na pia kama njia ya kuendeleza vizazi. Wanandoa wafanyapo kamwe hawahesabiwi kuwa wadhambi ama wakosa kwani ndio msingi wa umoja wao.
2) RUSHWA
Baadhi ya watu hufanya ngono kwasababua ya kutaka kununua huduma fulani ama kulipa fadhila fulani. Hii hutokana na ugumu ambao muhusika anao katika jambo husika. ugumu huo waweza kukuta ni wa kifedha, ugumu wa maisha, kazi, cheo, nk. Vijana wengi wa kike kwa wa kiume huanguka katika mtego huu na kujikuta wale wa kiume wakiwa na ma sugar mamy na wakike wakiwa na mabuzi.
3) TABIA
Kuna baadhi ya watu hufanya ngono kwasababu ya tabia tu. Hawa huwakuti na shida ama hitaji lolote lakin bado wanaanguka katika mtego wa kufanya ngono hovyo. wengi wao ni watu walioko kenye ndoa ambao kwao haijalisha kama ana mke ama mume basi lazima tu atakuwa mtu wa kutembea nje ya ndoa yake.
4) BIASHARA
Wapo watu ambao wameamua kuuza miili yao ili kuweza kukidhi haja za kimaisha. wengi wa hawa wawe wakike ama wakiume wapo kwenye uzinzi ili waweze kupata pesa za kujikimu kimaisha. Haijalisha anauza mwili wapi na kwa gharama gani ila wote ni wafanya biashara wa miili yao.
5) STAREHE
Kuna baadhi ya watu ambao hufanya ngono kama moja ya starehe zao. mara nyingi sana hawa ni wale ambao wakoa katika uchumba ama urafiki ambao hujikuta wanahitaji kuliwazana hivyo huliwazana kwa namna ya kufanya ngono.
6) UDADISI
Vijana wadogo wengi hasa school childrens huanguka katika kundi hili. Hawa hutaka kudadisi inafanywaje, inaraha kiasi gani na ikoje. kwao hakuna commitment zaid ya kugundua what is inside it.
HITIMISHO
Tendo la ndoa iwe limefanywa kwa msukumo gani nyuma yake laweza kuishia kupata mimba ama kupata ukimwi. Ingawa wengi husema heri mimba utazaa mtoto kuliko ukimwi, mimi huwa nasema heri ukimwi utakuwa ndani yako wewe uliyeutafuta kuliko mimba ambayo utazaa watoto ambao huwatarajii na hivyo kuongeza idadi ya watoto wanaokosa malezi stahiki.
alwayz
Mwl-gfsonwin