Msuguano mkali kati ya UEFA na FIFA

Msuguano mkali kati ya UEFA na FIFA

Bujibuji Simba Nyamaume

Platinum Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
78,144
Reaction score
166,077
FIFA imepanga kuunda kampuni mpya ya kibiashara iitwayo FIFA Forward Enterprise, yenye thamani ya takribani $20 Bilioni (karibu TZS Trilioni 50) kisha itauza 20% ya hisa za kampuni hiyo kwa wawekezaji binafsi ikiwemo kampuni ya uwekezaji Thrive Eternal na benki ya J.P. Morgan.

Kupitia mpango huo kila chama cha soka (kati ya vyama 211 vilivyopo) kitapokea $40 Milioni (Kama Bilioni 100) kwa kipindi cha miaka mitatu 2027–2030 kisha $8 Milioni kila mwaka (sawa na TZS 20 Bilioni).

Mpango huo umepigwa vikali na mashirikisho matatu ya soka ambayo ni Shirikisho la Soka Ulaya (UEFA), Shirikisho la Soka Amerika Kaskazini, Kati na Carebean (CONCACAF) na Shirikisho la Soka Amerika Kusini (CONMEBOL). UEFA imetoa msimamo mkali kupinga mpango huo ikisema "FIFA is not for sale" na kutishia kujitoa FIFA ikiwa haitabadili mpango huo.

Kati ya mashirikisho 6 ya soka duniani yanayounda FIFA, mashirikisho matatu tayari yametoa msimamo wa kupinga mpango huo. Mashirikisho mengine matatu yapo kimya yanasubiri. Mashirikisho hayo ni Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Shirikisho la Soka Asia (AFC) na Shirikisho la Soka Oceania (OFC).

Ukiangalia vizuri hapa utakumbuka ile kauli ya wahenga kwamba maskini hana kauli. Mashirikisho matatu yaliyotangaza msimamo wa kupinga mpango huo wa FIFA ni yale yanayojiweza (Ulaya na Amerika). Na mashirikisho ambayo yamekaa kimya ni ya nchi maskini (Afrika, Asia na Oceania).

Kwa wale msiojua Oceania ni vile visiwa vidogo hapo Pacific kama Fiji, Tuvalu, Kiribati, Vanuatu n.k. Ni nchi maskini sana na ndogo kieneo. Nchi moja inaweza kuwa sawa na kata ya Dumila 😂. Nchi pekee yenye afadhali huko Oceania ni New Zealand. Lakini wengine wote wapo hoi.

Sasa hao Oceania wameungana na maskini wenzao wa Afrika na Asia kupiga kimya. Ikumbukwe kwa sasa FIFA inatoa $10 (Kama TZS Bilioni 25) kwa kila mwanachama kwa miaka mitatu kwa ajili ya maendeleo ya soka. Hii ni sawa na TZS Bilioni 8 kwa mwaka.

Sasa ikiwa FIFA itafanikiwa katika mpango wake wa kuuza hisa, wanachama watapata kwa mkupuo $40 Milioni (Kama Bilioni 100) ndani ya miaka mitatu, kisha wataanza kupokea $8 Milioni kila mwaka (sawa na TZS 20 Bilioni).

Sasa nchi maskini zinaona kabisa hiyo ni fursa ya kupiga hela. Kutoka kupata TZS Bilioni 8 kwa mwaka hadi Bilioni 20 kwa mwaka sio jambo dogo. Hiyo ndiyo sababu imefanya wakae kimya.

Ama kweli ukiwa maskini wa kipato unakuwa hadi maskini wa akili. Ulaya, na Amerika wameshatoa msimamo. Sisi tunaogopa kutoa msimamo ili tusipoteze hela. What a shame?

UEFA inasema ikiwa FIFA itaunda kampuni ya kibiashara itakuwa imetoka kwenye misingi yake kwa sababu FIFA ni shirikisho lisilojiendesha kwa faida (Non-profit organization).

Pili UEFA inasema FIFA ikiendelea na mpango wake wa kuuza hisa itapoteza udhibiti wa Kombe la Dunia, kwa sababu watakaonunua hisa watakuwa na uwezo wa kuathiri michuano ya Kombe la Dunia. Pia wanasema ni kuingiza maslahi ya kibiashara kwenye maamuzi ya michezo, na hiyo itadhoofisha uhalali wa FIFA kama chombo cha kimataifa cha umma.!
 
Infatino hii proposal yake anaweza kwenda na maji maana mshauri mkuu wa FIFA jana kajiuzuru na pia uefa,Asia na shirikisho la America ya kusini wamepinga huo mpango CAF wana kikao siku za karibuni sitegemei Motsepe na jopo lake kumpinga Infatino.
 
Infatino hii proposal yake anaweza kwenda na maji maana mshauri mkuu wa FIFA jana kajiuzuru na pia uefa,Asia na shirikisho la America ya kusini wamepinga huo mpango CAF wana kikao siku za karibuni sitegemei Motsepe na jopo lake kumpinga Infatino.
Tanzania 🇹🇿 sioni kama wana nguvu za kuupinga mpango huu, wao kwao kikubwa ni pesa tu
 
Mpango wa FIFA wa kuuza sehemu ya umiliki katika kampuni mpya ya kibiashara yenye thamani ya dola bilioni 20 umezua mjadala mkubwa kuhusu uendeshaji na uwajibikaji katika soka duniani.

Pendekezo hilo linaeleza kuwa FIFA itaunda kampuni mpya itakayokuwa ikisimamia Kombe la Dunia na mashindano mengine makubwa, huku ikiuzwa hadi asilimia 20 ya hisa kwa wawekezaji binafsi.

Wanaounga mkono mpango huo wanasema unaweza kusaidia kupata mabilioni ya fedha kwa ajili ya maendeleo ya soka, lakini wakosoaji wanadai kuwa mashindano makubwa zaidi ya soka duniani hayapaswi kamwe kuwa mali ya wawekezaji wa nje.

Haya ndiyo yanayopendekezwa na FIFA, sababu zinazoifanya baadhi ya mashirikisho ya soka kupinga mpango huo, na hatua zinazotarajiwa kuchukuliwa baadaye.
1.
FIFA inataka kuanzisha kampuni ya kibiashara yenye thamani ya dola bilioni 20 ili kusimamia Kombe la Dunia na mashindano mengine makubwa, huku ikiuza hadi asilimia 20 ya hisa kwa wawekezaji binafsi.

2.
Chini ya mpango huo, FIFA itaendelea kuwa na udhibiti wa kampuni hiyo mpya huku ikikusanya hadi dola bilioni 4.2 kwa kuuza hisa chache kwa wawekezaji wa nje.

3.
Wakosoaji wana hofu kuwa wawekezaji binafsi wanaweza kuwa na ushawishi katika mashindano makubwa ya soka, jambo linalozua wasiwasi kuhusu utawala bora na uwazi.

4.
UEFA imeonya kuwa pendekezo hilo “limevuka mstari”, ikisema kuwa uendeshaji wa soka na roho yake “si mali ya kuuzwa.”

5.
Meya wa Greater Manchester, Andy Burnham, ameonya kuwa soka halipaswi kamwe kuwa mali ya kifedha, akiitaka FIFA kulinda mustakabali wa mchezo huo.
 
FIFA imepanga kuunda kampuni mpya ya kibiashara iitwayo FIFA Forward Enterprise, yenye thamani ya takribani $20 Bilioni (karibu TZS Trilioni 50) kisha itauza 20% ya hisa za kampuni hiyo kwa wawekezaji binafsi ikiwemo kampuni ya uwekezaji Thrive Eternal na benki ya J.P. Morgan.

Kupitia mpango huo kila chama cha soka (kati ya vyama 211 vilivyopo) kitapokea $40 Milioni (Kama Bilioni 100) kwa kipindi cha miaka mitatu 2027–2030 kisha $8 Milioni kila mwaka (sawa na TZS 20 Bilioni).

Mpango huo umepigwa vikali na mashirikisho matatu ya soka ambayo ni Shirikisho la Soka Ulaya (UEFA), Shirikisho la Soka Amerika Kaskazini, Kati na Carebean (CONCACAF) na Shirikisho la Soka Amerika Kusini (CONMEBOL). UEFA imetoa msimamo mkali kupinga mpango huo ikisema "FIFA is not for sale" na kutishia kujitoa FIFA ikiwa haitabadili mpango huo.

Kati ya mashirikisho 6 ya soka duniani yanayounda FIFA, mashirikisho matatu tayari yametoa msimamo wa kupinga mpango huo. Mashirikisho mengine matatu yapo kimya yanasubiri. Mashirikisho hayo ni Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Shirikisho la Soka Asia (AFC) na Shirikisho la Soka Oceania (OFC).

Ukiangalia vizuri hapa utakumbuka ile kauli ya wahenga kwamba maskini hana kauli. Mashirikisho matatu yaliyotangaza msimamo wa kupinga mpango huo wa FIFA ni yale yanayojiweza (Ulaya na Amerika). Na mashirikisho ambayo yamekaa kimya ni ya nchi maskini (Afrika, Asia na Oceania).

Kwa wale msiojua Oceania ni vile visiwa vidogo hapo Pacific kama Fiji, Tuvalu, Kiribati, Vanuatu n.k. Ni nchi maskini sana na ndogo kieneo. Nchi moja inaweza kuwa sawa na kata ya Dumila 😂. Nchi pekee yenye afadhali huko Oceania ni New Zealand. Lakini wengine wote wapo hoi.

Sasa hao Oceania wameungana na maskini wenzao wa Afrika na Asia kupiga kimya. Ikumbukwe kwa sasa FIFA inatoa $10 (Kama TZS Bilioni 25) kwa kila mwanachama kwa miaka mitatu kwa ajili ya maendeleo ya soka. Hii ni sawa na TZS Bilioni 8 kwa mwaka.

Sasa ikiwa FIFA itafanikiwa katika mpango wake wa kuuza hisa, wanachama watapata kwa mkupuo $40 Milioni (Kama Bilioni 100) ndani ya miaka mitatu, kisha wataanza kupokea $8 Milioni kila mwaka (sawa na TZS 20 Bilioni).

Sasa nchi maskini zinaona kabisa hiyo ni fursa ya kupiga hela. Kutoka kupata TZS Bilioni 8 kwa mwaka hadi Bilioni 20 kwa mwaka sio jambo dogo. Hiyo ndiyo sababu imefanya wakae kimya.

Ama kweli ukiwa maskini wa kipato unakuwa hadi maskini wa akili. Ulaya, na Amerika wameshatoa msimamo. Sisi tunaogopa kutoa msimamo ili tusipoteze hela. What a shame?

UEFA inasema ikiwa FIFA itaunda kampuni ya kibiashara itakuwa imetoka kwenye misingi yake kwa sababu FIFA ni shirikisho lisilojiendesha kwa faida (Non-profit organization).

Pili UEFA inasema FIFA ikiendelea na mpango wake wa kuuza hisa itapoteza udhibiti wa Kombe la Dunia, kwa sababu watakaonunua hisa watakuwa na uwezo wa kuathiri michuano ya Kombe la Dunia. Pia wanasema ni kuingiza maslahi ya kibiashara kwenye maamuzi ya michezo, na hiyo itadhoofisha uhalali wa FIFA kama chombo cha kimataifa cha umma.!
CAF hawawezi kupinga na siyo kwa sababu ya umaskini bali tatizo ni ule ule ugonjwa wa u-nyani au u-kima, wa kupenda mdebwedo na starehe bila kufanya kazi,
 
FIFA imepanga kuunda kampuni mpya ya kibiashara iitwayo FIFA Forward Enterprise, yenye thamani ya takribani $20 Bilioni (karibu TZS Trilioni 50) kisha itauza 20% ya hisa za kampuni hiyo kwa wawekezaji binafsi ikiwemo kampuni ya uwekezaji Thrive Eternal na benki ya J.P. Morgan.

Kupitia mpango huo kila chama cha soka (kati ya vyama 211 vilivyopo) kitapokea $40 Milioni (Kama Bilioni 100) kwa kipindi cha miaka mitatu 2027–2030 kisha $8 Milioni kila mwaka (sawa na TZS 20 Bilioni).

Mpango huo umepigwa vikali na mashirikisho matatu ya soka ambayo ni Shirikisho la Soka Ulaya (UEFA), Shirikisho la Soka Amerika Kaskazini, Kati na Carebean (CONCACAF) na Shirikisho la Soka Amerika Kusini (CONMEBOL). UEFA imetoa msimamo mkali kupinga mpango huo ikisema "FIFA is not for sale" na kutishia kujitoa FIFA ikiwa haitabadili mpango huo.

Kati ya mashirikisho 6 ya soka duniani yanayounda FIFA, mashirikisho matatu tayari yametoa msimamo wa kupinga mpango huo. Mashirikisho mengine matatu yapo kimya yanasubiri. Mashirikisho hayo ni Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Shirikisho la Soka Asia (AFC) na Shirikisho la Soka Oceania (OFC).

Ukiangalia vizuri hapa utakumbuka ile kauli ya wahenga kwamba maskini hana kauli. Mashirikisho matatu yaliyotangaza msimamo wa kupinga mpango huo wa FIFA ni yale yanayojiweza (Ulaya na Amerika). Na mashirikisho ambayo yamekaa kimya ni ya nchi maskini (Afrika, Asia na Oceania).

Kwa wale msiojua Oceania ni vile visiwa vidogo hapo Pacific kama Fiji, Tuvalu, Kiribati, Vanuatu n.k. Ni nchi maskini sana na ndogo kieneo. Nchi moja inaweza kuwa sawa na kata ya Dumila 😂. Nchi pekee yenye afadhali huko Oceania ni New Zealand. Lakini wengine wote wapo hoi.

Sasa hao Oceania wameungana na maskini wenzao wa Afrika na Asia kupiga kimya. Ikumbukwe kwa sasa FIFA inatoa $10 (Kama TZS Bilioni 25) kwa kila mwanachama kwa miaka mitatu kwa ajili ya maendeleo ya soka. Hii ni sawa na TZS Bilioni 8 kwa mwaka.

Sasa ikiwa FIFA itafanikiwa katika mpango wake wa kuuza hisa, wanachama watapata kwa mkupuo $40 Milioni (Kama Bilioni 100) ndani ya miaka mitatu, kisha wataanza kupokea $8 Milioni kila mwaka (sawa na TZS 20 Bilioni).

Sasa nchi maskini zinaona kabisa hiyo ni fursa ya kupiga hela. Kutoka kupata TZS Bilioni 8 kwa mwaka hadi Bilioni 20 kwa mwaka sio jambo dogo. Hiyo ndiyo sababu imefanya wakae kimya.

Ama kweli ukiwa maskini wa kipato unakuwa hadi maskini wa akili. Ulaya, na Amerika wameshatoa msimamo. Sisi tunaogopa kutoa msimamo ili tusipoteze hela. What a shame?

UEFA inasema ikiwa FIFA itaunda kampuni ya kibiashara itakuwa imetoka kwenye misingi yake kwa sababu FIFA ni shirikisho lisilojiendesha kwa faida (Non-profit organization).

Pili UEFA inasema FIFA ikiendelea na mpango wake wa kuuza hisa itapoteza udhibiti wa Kombe la Dunia, kwa sababu watakaonunua hisa watakuwa na uwezo wa kuathiri michuano ya Kombe la Dunia. Pia wanasema ni kuingiza maslahi ya kibiashara kwenye maamuzi ya michezo, na hiyo itadhoofisha uhalali wa FIFA kama chombo cha kimataifa cha umma.!
 
Jumla ya vyama vya mpira kwa kila bara hawa wakiukataa huu mpango wa Infatino wanaweza kupiga kura ya kutokua na Imani nae ajiuzuru na kuweza kuchunguzwa kama kuna rushwa..
CONCACAF mashirikisho 41..
Asian vyama vya mpira 47
Uefa mashirikisho 55 na
Africa wakiungana na hao jamaa kwa sababu mshauri mkuu wa FIFA kuhusu uwekezaji kasema hii proposal imekua ya kificho sana haina uwazi nae ajadhirikishwa kaamua kuijiuzuru ni mbaya sana kwa Rais wa FIFA kwa sasa wakati ni muamuzi mzuri tusubiri tu.
 
FIFA imepanga kuunda kampuni mpya ya kibiashara iitwayo FIFA Forward Enterprise, yenye thamani ya takribani $20 Bilioni (karibu TZS Trilioni 50) kisha itauza 20% ya hisa za kampuni hiyo kwa wawekezaji binafsi ikiwemo kampuni ya uwekezaji Thrive Eternal na benki ya J.P. Morgan.

Kupitia mpango huo kila chama cha soka (kati ya vyama 211 vilivyopo) kitapokea $40 Milioni (Kama Bilioni 100) kwa kipindi cha miaka mitatu 2027–2030 kisha $8 Milioni kila mwaka (sawa na TZS 20 Bilioni).

Mpango huo umepigwa vikali na mashirikisho matatu ya soka ambayo ni Shirikisho la Soka Ulaya (UEFA), Shirikisho la Soka Amerika Kaskazini, Kati na Carebean (CONCACAF) na Shirikisho la Soka Amerika Kusini (CONMEBOL). UEFA imetoa msimamo mkali kupinga mpango huo ikisema "FIFA is not for sale" na kutishia kujitoa FIFA ikiwa haitabadili mpango huo.

Kati ya mashirikisho 6 ya soka duniani yanayounda FIFA, mashirikisho matatu tayari yametoa msimamo wa kupinga mpango huo. Mashirikisho mengine matatu yapo kimya yanasubiri. Mashirikisho hayo ni Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Shirikisho la Soka Asia (AFC) na Shirikisho la Soka Oceania (OFC).

Ukiangalia vizuri hapa utakumbuka ile kauli ya wahenga kwamba maskini hana kauli. Mashirikisho matatu yaliyotangaza msimamo wa kupinga mpango huo wa FIFA ni yale yanayojiweza (Ulaya na Amerika). Na mashirikisho ambayo yamekaa kimya ni ya nchi maskini (Afrika, Asia na Oceania).

Kwa wale msiojua Oceania ni vile visiwa vidogo hapo Pacific kama Fiji, Tuvalu, Kiribati, Vanuatu n.k. Ni nchi maskini sana na ndogo kieneo. Nchi moja inaweza kuwa sawa na kata ya Dumila 😂. Nchi pekee yenye afadhali huko Oceania ni New Zealand. Lakini wengine wote wapo hoi.

Sasa hao Oceania wameungana na maskini wenzao wa Afrika na Asia kupiga kimya. Ikumbukwe kwa sasa FIFA inatoa $10 (Kama TZS Bilioni 25) kwa kila mwanachama kwa miaka mitatu kwa ajili ya maendeleo ya soka. Hii ni sawa na TZS Bilioni 8 kwa mwaka.

Sasa ikiwa FIFA itafanikiwa katika mpango wake wa kuuza hisa, wanachama watapata kwa mkupuo $40 Milioni (Kama Bilioni 100) ndani ya miaka mitatu, kisha wataanza kupokea $8 Milioni kila mwaka (sawa na TZS 20 Bilioni).

Sasa nchi maskini zinaona kabisa hiyo ni fursa ya kupiga hela. Kutoka kupata TZS Bilioni 8 kwa mwaka hadi Bilioni 20 kwa mwaka sio jambo dogo. Hiyo ndiyo sababu imefanya wakae kimya.

Ama kweli ukiwa maskini wa kipato unakuwa hadi maskini wa akili. Ulaya, na Amerika wameshatoa msimamo. Sisi tunaogopa kutoa msimamo ili tusipoteze hela. What a shame?

UEFA inasema ikiwa FIFA itaunda kampuni ya kibiashara itakuwa imetoka kwenye misingi yake kwa sababu FIFA ni shirikisho lisilojiendesha kwa faida (Non-profit organization).

Pili UEFA inasema FIFA ikiendelea na mpango wake wa kuuza hisa itapoteza udhibiti wa Kombe la Dunia, kwa sababu watakaonunua hisa watakuwa na uwezo wa kuathiri michuano ya Kombe la Dunia. Pia wanasema ni kuingiza maslahi ya kibiashara kwenye maamuzi ya michezo, na hiyo itadhoofisha uhalali wa FIFA kama chombo cha kimataifa cha umma.!
Mkuu Una nyuzi za kibabe Sana

Usimuliaji mzuri, uandishi mzuri na kuweka vitu Kwa uwazi , hongera.
 
Back
Top Bottom