Nadhani msomi, ni yule aliye ktk mchakato mzima wa kusoma. Tofautisha na mhitimu. Kubwa kabisa. Yule aliejaaliwa kuwa msomi wa kiwango cha kutukuka huwa na sifa ya kutokuwa na dharau. Hususan kwa watu ambao hayuko nao ktk taasisi yake anayofanyia mchakato wake wa kusoma, akitambua kuwa kusoma kwa kiasi kikubwa ni kujifunza kwa kuishi.
Anayetambua, msomi ni yule anaeishi maisha yake yote, akijifunza. Hususan mwenyewe, na akiheshimu wasomi wengine wanaojifunza wenyewe na kazi zao. Shaaban Robert wa Tanzania, ni mfano mmoja, na wengine wengi wapo, msomi hana kibri. Ana heshima, ana ushujaa wa kuukubali ukweli. Kinyume cha hapo, ni kinyume cha msomi. Tuseme ni limbukeni wa kitu kidogo alichomaliza kujifunza na nachobakia anakimiliki kwenye mawazo yake tu.