Mwanzoni mwa miaka ya sabini kulikuwa na Bendi inaitwa Jamhuri Jazz pale Tanga ambayo ilikuwa na ushindani mkubwa sana na Atomic Jazz. Bendi hiyo ilianzishwa na ndugu wawili: William Kinyonga, na George Kinyonga. Baadaye walimshirikisha mdogo wao Wilison Kinyonga na rafiki yao Omari Shabani (ambaye alikuwa akijulikana kam Profesa Omari). Kati ya nyimbo maarufu sana za Jamhuri Jazz wakati huo ni pamoja na hizi
Walipotoka Tanga walihamia Arusha na kuansiaha Arusha jazz baadaye wakahamia Nairobi na kuanzisha SImba wa Nyika ambayo baadaye iligawanyika na kuwa na tawi lililojulikana ka Les wa Nyika. Sasa angalia mwanamuziki mwazilishi wa bendi hiyo anavyoishi.