PAYE
JF-Expert Member
- Jun 19, 2025
- 419
- 553
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amewasilisha salamu za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuelekea pambano la Knockout ya Mama Season 6 ambayo itafanyika kesho Viwanja vya Posta Kijitonyama Jijini Dar es Salaam.
Katika salamu hizo Ndugu Gerson Msigwa amesema kuwa Dkt Samia Suluhu Hassan anataka mabondia wetu wakapigane katika mataifa makubwa kama vile Marekani,China,Japan huku Serikali itahakikisha kuwa inaendelea kuungana mkono michezo ili vijana watimize ndoto zao.
Katibu Mkuu Gerson Msigwa amezungumza na waandishi Jijini Dar es Salaam na kuipongeza Mafia boxing promotion ambao wameendelea kuinua mchezo wa masumbwi nchini.
Katika salamu hizo Ndugu Gerson Msigwa amesema kuwa Dkt Samia Suluhu Hassan anataka mabondia wetu wakapigane katika mataifa makubwa kama vile Marekani,China,Japan huku Serikali itahakikisha kuwa inaendelea kuungana mkono michezo ili vijana watimize ndoto zao.
Katibu Mkuu Gerson Msigwa amezungumza na waandishi Jijini Dar es Salaam na kuipongeza Mafia boxing promotion ambao wameendelea kuinua mchezo wa masumbwi nchini.