Msigwa: Mangula ni ndege chichidodo

Watu wanakula nguruwe wakati nguruwe anakula mavi halafu wala nguruwe hawataki hata kuyagusa mavi...ha haa haaa.

Hata wenzio wanamtafuna sana mkuu wa meza! Wakifunga mauzo huwa yanashuka sana!
 
Msigwa umenikumbusha mbali sana mkuu koz hiyo novel ya ghana nilikuwa naipenda sana na ndio ilionifanya mimi leo niwe nakula boom la wazee.....,
 
ahahaa... Ila yeye mbona anakula kuku ..kuku hali wadudu?

Ivuga bwana!! Fikiria Mangula anajisikiaje kufananishwa na chichidodo. Fikiria kula maggots wanaotoka moja kwa moja kwenye kinyesi unachokiona.
 


kweli wewe ni GREAT THINKER - nakugongea LIKES x 1,000
 
Yaani huyu 2015 atamjua mwakalebela ni nani.Ngoja apayuke msimu wake huu hakuna tena cha ubunge
 
hivi bado analima viazi! au zuga, mfupa uliomshinda fisi mangula ni janga la kitaifa....
 
Nyie kidhungu chenu mmejifunzia kwenye sekondari za kata au?, hiyo ni Beautiful na sio Beautyful

no research,no right to speak...ile ni fasihi ...huwezi kuelewa kama sio mwanafasihi
 

Mkuu,

Naona wewe ndio wale mnaofaidi hiyo unayosema "modern times" ndio big time mkuu unafaidi kila kitu.

Kwenye hicho kitabu ambacho nami nilikisoma nikiwa sekondari, Ayi Kweyi Ama anazungumzia Ghana baada ya kupata uhuru jinsi ambayo RUSHWA ilistawi na anaangalia vitu vitatu PESA, UWEZO WA MTU KWENYE JAMII na NGUVU aliyo nayo mtu kwenye jamii.

Anazungumzia jinsi serikali ya Kwame Nkruma jinsi ilivyovuja pesa na kuharibu uchumi wakati ndio ilitakiwa kwa waafrika kuwaonyesha walokuwa wakoloni kwamba tuna kila sababu ya kuwa uhuru na tunaweza kusimama wenyewe bila msaada wa mtu yoyote.

Pia anaonyesha muanguko wa jamii nzima kwenye eneo la kuwajibika kama jamii na kuna sehemu huwa naikumbuka alipoongelea kumomony'oka kwa maadili katika jamii.

Nakuuu- "Sounds arise and kill all smells as the bus pulls into the dormitory town. Past the big public lavatory the stench claws inward to the throat. Sometimes it is understandable that people spit so much, when all around decaying things push inward and mix all the body's juices with the taste of rot . . . . Hot smell of caked s--- split by afternoon's baking sun, now touched by still evaporating dew. The nostrils, incredibly, are joined in a way that is most horrifying direct to the throat itself and to the entrails right through to their end."-mwisho wa kunukuu.

Halafu kuna mtu anaitwa "The Man" kuna kazi kwelikweli kumtambua anagundulika yumo kwenye basi, ni mtu muhimu sana kwenye kitabu hicho kwani hilo basi limo safarini.

Tanzania yetu ya leo bado imo kwenye ukoloni mamboleo na ni watanzania wenyewe kwa wenyewe wanakulana mumo kwa mumo bila hata huruma, wenye nafasi wanaiba na kujilimbikizia na wale wasio nacho wanazidi kudidimia.

Mwalimu Msigwa nampa zote 5, duuh ndege Chichidodo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…