Msanii gani angalau amemkaribia Capt. John Komba mpaka Sasa?

Mrisho mpoto anaweza sema sijaisikiaa nyimbo aliyoimba mwenyewe naona nyingi ameshirikishwa kwenye huu msiba ila akiimba mwenyewe anaweza akafanya kitu kizuri kama alivyofanya kwa ruge
 
Captain John Comba . Alijua anafanya nini aliiitoa ile tone ya nyimbo za jeshini(Chenja) lakini za vitani akaileta uraiani . Ukisikiliza nyimbo zake unasikia msisimko mwilini (too emotional song) alikuwa ana sauti ya ajabu sana.
Huwezi mlimganisha na hawa wasanii wetu wanaodhani kuimba ni kuimba tu. Bila kujali aina ya nyimbo na mazingira. Nyimbo hazina hisia hata kidogo utadhani ni kelele za vyombo kabatini.
 
Wakuu nimesikiliza baadhi ya nyimbo za maombolezo zilizotolewa na wasanii mbalimbali Kama vile, Rayvan, Konde Boy, Msechu n.k..

Nikarudi kumsikiliza tena Capt. Komba kwenye nyimbo zake enzi zile za kumuaga Mwl. Nyerere aisee sijaona msanii aliyemfunika hadi Sasa.

Embu tujadili hapa mbadala was Capt. Komba ni nani? Au ndio pengo lake halizibiki?
Msechu anamkaribia kwa mwili tu
 
Unajua hata ule wimbo aliomuimbia nyerere inavyosemekana alishapata taarifa muda murefu kuwa Nyerere kafariki na ndiyo maana watu walijiuliza huyu mtu alitunga saaa ngapi wimbo manaake walivyotangaza tuu kesho yake kitu kwa hewa.
 
Back
Top Bottom