Mh Joseph Pombe Magufuli mutu ya watu umefanya mambo mengi sana ambayo mengine hata halaiki ilishindwa kuamini kama ungeweza kuyafanya.
- Umewasamehe babu seya na wenzake
- Umewasamehe askari waliohusika kutorosha dhahabu
- Umesamehe mahabusu zaid ya mia nne waliokuwa magerezani
- Umemrudisha kazini mkurugenzi wa TPDC ambaye alishafanyiwa figusu na hayupo kazini kwa miak mitatu sasa
Hayo yote sio rahisi kuyafanya, bali ni kwa hekima na huruma uliyonayo ambayo inaongozwa na roho wa Mungu. Wapo watu wanabeza hatua ulizochukua. Binafsi naungana na wewe.
OMBI LANGU KWAKO
Naomba kwa hekima zilizokuongoza kufanya hayo yote. Pia roho wa Mungu aendelee kukuongoza kuwasehe hawa vikongwe wetu wa chama cha mapinduzi. Kwa kuwa wamekengeuka tu. Walisahau kuwa wao hawapo tena kwenye dola. Pengine walizoea kuwaendesha waliopita wakadhani remote bado wanayo kumbe uliondoka nayo pamoja na moto wa kuwabatiza. wasemehe tu wala wasichukuliwe hatua. kwa hatua ulizozichukua kuwanyang'anya mali za ccm ambazo walijimirikisha zinatosha sana. Yangu ni hayo tu.