Msamaha kwa walaka wa wazee

Msamaha kwa walaka wa wazee

MITOCHONDRIA

Senior Member
Joined
Feb 21, 2013
Posts
147
Reaction score
34
Mh Joseph Pombe Magufuli mutu ya watu umefanya mambo mengi sana ambayo mengine hata halaiki ilishindwa kuamini kama ungeweza kuyafanya.

  1. Umewasamehe babu seya na wenzake
  2. Umewasamehe askari waliohusika kutorosha dhahabu
  3. Umesamehe mahabusu zaid ya mia nne waliokuwa magerezani
  4. Umemrudisha kazini mkurugenzi wa TPDC ambaye alishafanyiwa figusu na hayupo kazini kwa miak mitatu sasa
Hayo yote sio rahisi kuyafanya, bali ni kwa hekima na huruma uliyonayo ambayo inaongozwa na roho wa Mungu. Wapo watu wanabeza hatua ulizochukua. Binafsi naungana na wewe.

OMBI LANGU KWAKO
Naomba kwa hekima zilizokuongoza kufanya hayo yote. Pia roho wa Mungu aendelee kukuongoza kuwasehe hawa vikongwe wetu wa chama cha mapinduzi. Kwa kuwa wamekengeuka tu. Walisahau kuwa wao hawapo tena kwenye dola. Pengine walizoea kuwaendesha waliopita wakadhani remote bado wanayo kumbe uliondoka nayo pamoja na moto wa kuwabatiza. wasemehe tu wala wasichukuliwe hatua. kwa hatua ulizozichukua kuwanyang'anya mali za ccm ambazo walijimirikisha zinatosha sana. Yangu ni hayo tu.
 
Hakuna msamaha kwa wahaini,haiwezekani wamkwamishe Rais wetu halafu waachwe hivi hivi. Chinjilia baharini wahaini wote.

Kweni hawa mnaowaita wahain wa CCM & kina Babu Seya, Mahabusu wa kesi za ajabu ajabu, wafungwa waliowahi kuhukumiwa kwa kuua na wakasamehewa ni nani mbaya au hatari zaidi kama watumishi hewa ambao hadi leo wanaosota mtaani na hawastahili msamaha wake?
 
Wamekutuma hawataki msamaha wowote ,wanataka haki itendeke ,usijeshangaa Jiwe wako ndio akaomba msamaha si unakumbuka alishaomba kuongea na wastaafu wakati mwanzoni aliwaambia wanawashwawashwa baadaye akasalimu amri .
 
Wewe umeambiwa uwaombee msamaha? kwa kosa lipi? wao ndiyo wanataka ufafanuzi nani anamtuma huyo kijana kuwachafua? hili nafikiri ndilo linatakiwa kujibiwa na Katibu Mkuu wa chama na bado hajafanya hivyo...

Sababu Balaza la wazee hata kama halitakaa kuujadili waraka sababu ya moto wake ulivyo sasa - still ule waraka ni lazima katibu mkuu aujibu ili mambo yaishe - tuna uchaguzi wa serikali za mitaa jamani...tunahitaji kuwa wamoja.
 
Hakuna msamaha kwa wahaini,haiwezekani wamkwamishe Rais wetu halafu waachwe hivi hivi. Chinjilia baharini wahaini wote.
I think I have to re-born; hizi tafsiri mpya mpya za vijana wa sasa zinanishinda, hivi kutokukubaliana na maamuzi ya raisi katika mambo yake au utendaji wake ni UHAINI!? Nadhani naishi dunia nyingine kabisa kama sio Tanzania nyingine. Kumbe hata boss wangu nae nisipokubaliana nae hata kwenye mazungumzo ya simu nako ni kukaidi maamuzi ya boss!? Uncle Tom sijui bado yupo hai, maanake wale ndio walitakaga kufanya uhaini, hu uhaini wa sasa hivi cheche kabisa.
 
Mh Joseph Pombe Magufuli mutu ya watu umefanya mambo mengi sana ambayo mengine hata halaiki ilishindwa kuamini kama ungeweza kuyafanya.

  1. Umewasamehe babu seya na wenzake
  2. Umewasamehe askari waliohusika kutorosha dhahabu
  3. Umesamehe mahabusu zaid ya mia nne waliokuwa magerezani
  4. Umemrudisha kazini mkurugenzi wa TPDC ambaye alishafanyiwa figusu na hayupo kazini kwa miak mitatu sasa
Hayo yote sio rahisi kuyafanya, bali ni kwa hekima na huruma uliyonayo ambayo inaongozwa na roho wa Mungu. Wapo watu wanabeza hatua ulizochukua. Binafsi naungana na wewe.

OMBI LANGU KWAKO
Naomba kwa hekima zilizokuongoza kufanya hayo yote. Pia roho wa Mungu aendelee kukuongoza kuwasehe hawa vikongwe wetu wa chama cha mapinduzi. Kwa kuwa wamekengeuka tu. Walisahau kuwa wao hawapo tena kwenye dola. Pengine walizoea kuwaendesha waliopita wakadhani remote bado wanayo kumbe uliondoka nayo pamoja na moto wa kuwabatiza. wasemehe tu wala wasichukuliwe hatua. kwa hatua ulizozichukua kuwanyang'anya mali za ccm ambazo walijimirikisha zinatosha sana. Yangu ni hayo tu.
Hiyo mbona walishasamehewa? Wametulia tu saivi mambo yaendelee.
 
Hakuna msamaha kwa wahaini,haiwezekani wamkwamishe Rais wetu halafu waachwe hivi hivi. Chinjilia baharini wahaini wote.
Watanzania hawa wazee wametukana na Musiba kosa lao ni kulalamika?Mie nilidhani wanaccm wangejiuliza kwanini Musiba kawatukana? Mbona aliyetukana hasemwi wanasemwa waliotukanwa?
 
Unamzungmzia Mwenyekiti? Hahaahaa tulia kwanza huu ndio mnara wa Babeli halisi sasa, miaka ya nyuma walikua wanafanya site clearance, sasa wameanza ujenzi rasmi wa mnara. Dadeeeeeki ngoja ninywe kwa raha zangu, shenzi kabisa. PUMZIKENI kwa Amani wote mliotangulia mbele za haki kwa mapenzi ya watu...
 
Kweni hawa mnaowaita wahain wa CCM & kina Babu Seya, Mahabusu wa kesi za ajabu ajabu, wafungwa waliowahi kuhukumiwa kwa kuua na wakasamehewa ni nani mbaya au hatari zaidi kama watumishi hewa ambao hadi leo wanaosota mtaani na hawastahili msamaha wake?
Watoswe tu haiwezekani wamsumbue Rais wetu kipenzi. Mzee baba hakuna kutoa msamaha hapa, piga chini wote wasumbufu hata marais wastaafu kama wanawashwa washwa piga chini kureeee.
 
Back
Top Bottom