Wewe mleta Mada kula vizuri na ufanye mazoezi Nina ushuhuda.
Kuna kaka nilikutana nae 2015 yesuuu na maria, alikuwa mrefuuu sana , mwembaaaa alikuwa anakuja offisin kutafuta Wateja ndo alikuwa ameanza kazi kama sales, baada ya hapo sikumuona tena. Ila nilikuwa mawasiliano nae Mara moja moja, nikipa Wateja nawadirect kwake, yaan tukawa kama ndugu, najua lugha yake so ananichukulia kama Dada, na mm namuona kama kaka .
Nilikuja kukutana na face to face mwisho ni mwa mwaka Jana yesuuuuuu jamani kajaa vizuriii aisee nikisema vizuri sina utani, hana kitambi , anajua kuvaaaa na vile ashakuwa na cheo dah naomba niishie hapa.
Mashoga zangu wakiniona nae kila MTU anataka no yake, MTU mwenyewe ana gf, sijui niwape no zake wapambane nae😁😁😁😁
Mleta Mada fanya kula misosi ya maana kama pesa haikusumbui utuletee mrejesho, utendee haki urefu wako loh!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.